Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Mji Mdogo Same Bw. Uledi Lusasi amewakumbusha Wenyeviti wa Vitongoji kuhakikisha kuwa wanafanya mikutano ya Vitongoji ili kujadili masuala ya Maendeleo ikiwa ni pamoja n a kusikiliza kero za wananchi na kuzipatia ufumbuzi.
Bw.Lusasi alitoa ushauri huo kwenye kikao cha Baraza la Mamlaka ambapo alisema vikao hivyo ambavyo vipo kisheria ni muhimu vifanyike kwani ndivyo vinavyowaunganisha wananchi na Serikali yao.
Aidha amewataka Wenyeviti hao kusimamia Amani na utulivu katika maeneo yao na iwapo atatokea mtu wanayemtilia shaka watoe taarifa mapema kwenye Mamlaka husika ili hatua stahili ziweze kuchukuliwa.
“Nyie ni walinzi wa Amani kwenye maeneo yenu, hivyo basi kwenye Mtaa wako akiingia mgeni ambaye mnamtilia shaka hakikisheni mnatoa taarifa ili hatua stahili ziweze kuchukuliwa” alisema
Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Same.Haki zote zimehifadhiwa.