• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Same District Council
Same District Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala Za Mikoa na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Same

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idaraya Elimu Sekondari
      • Rasili Mali Watu na Utawala
      • Ardhi Maliasili na Utalii
      • Fedha Na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Kazi na Zimamoto
      • Maji
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi.
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo Cha TEHAMA
      • Kitengo Cha Nyuki
      • Kitengo Cha Uchaguzi
      • Kitengo Cha Manunuzi
      • Kitengo Cha Sheria
    • Kata
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Mipango
      • Elimu,Afya na Maji
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
      • TAMKO LA VIONGOZI WA UMMA KUHUSU RASILIMALI NA MADENI
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Stoo Ya Picha

Historia

HALMASHAURI YA WILAYA YA SAME

HISTORIA YA WILAYA YA SAME.

UTANGULIZI

Halmashauri ya Wilaya ya Same ilianzishwa rasmi kwa Sheria ya Bunge Sura ya 287 (Mamlaka za Wilaya) ya Sheria za Tanzania na ilianza kutekeleza majukumu yake tarehe 01 Januari 1984. Aidha Halmashauri ina Idara 13 na vitengo 6 ambavyo vinatekeleza majukumu mbalimbali kama ambavyo imeanishwa hapo chini:-

 

1.0  IDARA YA AFYA  

1.1 Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF)

Asilimia 30.6 ya kaya za Wilaya ya Same zimejiunga na CHF. Kwa Mkoa wa Kilimanjaro Wilaya ya Same ni ya 3 Kati ya Wilaya saba za Mkoa.

1.1.1 Mipango/Mikakati Iliyopo kufikisha 80%

  1. Kuhakikisha     walengwa wanaopata Fedha kupitia mpango wa Kaya maskini-TASAF wanajiunga     na mfuko wa CHF 
  2. Kutumia     wanafunzi wa shule wakiwa kwenye makundi ya watu sita kujiunga na CHF kwa     mfano Same Sekondari.
  3. Bodi ya     Afya ya Wilaya kufanya ziara ya uhamasishaji kwa kamati za vituo vya Afya     kujiunga na CHF.
  4. Kamati za     Afya za vituo kufanya uhamasishaji kwa jamii kupia mikutano ya vijiji na     CHF kuwa Agenda ya kudumu kwenye vikao vya vijiji.

 

Jedwali 1.1: Vituo Vya Kutolea Huduma Za Afya Wilayani

                                                                                         
 

S/No

 
 

AINA YA KITUO

 
 

IDADI

 
 

 

 
 

 

 
 

SERIKALI

 
 

MASHIRIKA YA DINI

 
 

BINAFSI

 
 

JUMLA

 
 

1

 
 

Hospitali

 
 

1

 
 

1

 
 

-

 
 

2

 
 

2

 
 

Vituo vya Afya

 
 

6

 
 

1

 
 

1

 
 

8

 
 

3

 
 

Zahanati

 
 

39

 
 

15

 
 

9

 
 

62

 
 

 

 
 

Jumla

 
 

46

 
 

17

 
 

10

 
 

72

 

Chanzo: Idara ya Afya

1.3 Hali ya upatikanaji wa dawa na vifaa tiba

Upatikanaji wa dawa na vifaa tiba katika vituo vya kutolea huduma ni wa wastani, hii imesababishwa na upungufu wa dawa na vifaa tiba kutoka bohari ya dawa (msd), pia msd kutotoa ruhusa ya kununua dawa na vifaa tiba mapema kutoka kwa wazabuni wengine. Vifaa vilivyopo kwenye Hospitali ya Wilaya ni X-ray, Ultrasound, Anaesthetic machine, Autoclave, Washing mashine, Generator, Microscope, Votex, Diathermy na Pima Machine.

1.4 Mkakati makini wa zoezi la usafi na Mipango ya kuwafanya watu wajenge tabia ya usafi

1.      Kila kitongoji kuwa na siku moja ya usafi itakayoshirikisha kila mwananchi tofauti na siku ya jumamosi ya mwisho wa mwezi ya usafi kitaifa

2.      Kuunnda/kuwa na vikundi kazi kwa kila kata vitakavyotokana na jamii , vitakavyohusika kusimamia usafi kwa kila kata na watakao kaidi watatozwa faini. Aidha asilimia kadhaa ya faini itakuwa ya vikundi/kikundi kutegemeana na makubaliano

3.      Kila kata kuwa na Afisa afya atakayeshirikiana na wataalamu wengine waliopo kwenye kata. Kata ambayo haina Afisa afya ateuliwe afisa maendeleo ya jamii kukaimu nafasi ya Afisa afya

4.      Kuchukua hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kuwafikisha mahakamani wote watakaokiuka sheria na kanuni za afya ya mazingira

5.      Kuwa na dampo la taka ngumu na taka maji katika Halmashauri

6.      Kuwa na vitendea kazi, gari rasmi la kusomba taka na ada za uzoaji taka zitumike kwa makusudi ya uzoaji taka

7.      Kuwezesha walezi wa kata siku 5 kila robo mwaka kwa ajili ya kutembelea kata na kuhamasisha jamii juu ya usafi wa mazingira

8.      Kila biashara/ kaya kuwa na chombo/vyombo vya kuhifadhia taka

9.      Kushinadanisha kitongoji au mtaa, kata na kata ili kuleta ushindani na kuboresha usafi

10.   Kujenga vizimba vya taka katika maeneo yatakayo ainishwa Elimu ya usafi na mazingira ikaziwe shuleni (shule za msingi, sekondari na vyuo) mahali pa kazi yao.

 

 

 

1.5 Idadi ya Watumishi waliopo, Ikama na Pungufu ndani ya Idara 

Idara ya afya inahitaji jumla ya watumishi 1114 waliopo ni 462, idara ina upungufu wa watumishi 689. Sawa na 61.8%. Hospitali ya Wilaya inahitaji Watumishi kwa kada kama ifuatavyo:-

Jedwali 1.1: Idadi ya Watumishi waliopo, Ikama na Pungufu ndani ya Idara

                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                             
 

FANI YA MTUMISHI

 
 

HITAJIKA

 
 

WALIYOPO

 
 

PUNGUFU

 
 

Medical Doctor 

 
 

23

 
 

4

 
 

19

 
 

Assistant Medical officer

 
 

39

 
 

3

 
 

36

 
 

Assistant Dental officer

 
 

1

 
 

-

 
 

1

 
 

Dental therapist

 
 

2

 
 

1

 
 

1

 
 

Pharmacist

 
 

2

 
 

1

 
 

1

 
 

Pharmaceutical Technologist 

 
 

 

 
 

5

 
 

 

 
 

AssistantPharmaceutical Technologist

 
 

8

 
 

-

 
 

8

 
 

Social welfare

 
 

3

 
 

-

 
 

3

 
 

Environmental  officer Health officer

 
 

2

 
 

1

 
 

1

 
 

Wauguzi

 
 

99

 
 

71

 
 

28

 
 

Laboratory scientist

 
 

1

 
 

1

 
 

-

 
 

Health laboratory technologist

 
 

4

 
 

4

 
 

-

 
 

AssistantHealth   laboratory technologist

 
 

4

 
 

1

 
 

3

 
 

Occupational therapist

 
 

2

 
 

1

 
 

1

 
 

Physiotherapist

 
 

2

 
 

2

 
 

-

 
 

Medicall attendants

 
 

59

 
 

44

 
 

15

 
 

Health secretary

 
 

1

 
 

1

 
 

-

 
 

Medical recoder 

 
 

5

 
 

1

 
 

4

 
 

Radiology scientist

 
 

1

 
 

-

 
 

1

 
 

Radiographer technologist

 
 

3

 
 

-

 
 

3

 
 

Nutritionist

 
 

1

 
 

1

 
 

-

 
 

Ophthalmologist

 
 

1

 
 

1

 
 

-

 
 

Optometrist

 
 

3

 
 

-

 
 

3

 
 

Economist

 
 

1

 
 

-

 
 

1

 
 

Biomedical technologist

 
 

4

 
 

-

 
 

4

 
 

Motury attendants

 
 

5

 
 

-

 
 

5

 
 

Computer system analysit

 
 

1

 
 

-

 
 

1

 
 

Computer operator

 
 

1

 
 

-

 
 

1

 
 

Accountant

 
 

1

 
 

-

 
 

1

 
 

Assistant Accountants 

 
 

2

 
 

-

 
 

2

 
 

Supplier officer

 
 

1

 
 

-

 
 

1

 
 

Assistant supplier officer

 
 

1

 
 

1

 
 

-

 
 

Electrical Technician

 
 

4

 
 

-

 
 

4

 
 

Personal secretary 

 
 

1

 
 

1

 
 

-

 
 

Plumber 

 
 

1

 
 

-

 
 

1

 
 

Security guard

 
 

4

 
 

2

 
 

2

 
 

Cooker

 
 

4

 
 

-

 
 

4

 
 

Dhobi

 
 

4

 
 

-

 
 

4

 
 

Driver

 
 

5

 
 

2

 
 

3

 





Chanzo: Idara ya Afya

Kwa upande wa Hospitali ya Wilaya, kutokana na staffing level 2014-2018 Hospitali ya wilaya ina upungufu wa watumishi 97.

1.6 Magonjwa Kumi yanayoongoza kwa Idara ya Wagonjwa wa Nje ni:

Magonjwa ya njia ya hewa, Nimonia, Malaria, Magonjwa ya kuhara, Minyoo ya tumbo, Magonjwa ya ngozi, Magonjwa mengine, Upasuaji wa dharura, Upungufu wa damu na Magonjwa ya macho.

 

1.7 Magonjwa Kumi yanayoongoza kwa Idara ya Wagonjwa wa Ndani ni: Nimonia, Magonjwa ya njia ya hewa, Magonjwa mengine, Malaria kali, Upungufu wa damu, Magonjwa ya kuhara, Watoto waliozaliwa na uzito mdogo, Upasuaji wa dharura, Ukimwi na Majeraha mbalimbali.

 

1.8 Vifo Vya Watoto Umri Chini Ya Siku 28

Mwaka 2015 vilitokea vifo 5 katika vizazi hai 1000

 

1.9 Vifo Vya Watoto Chini Ya Miaka 5

Mwaka 2015 vilitokea vifo 8 katika vizazi hai 1000

 

 

 

1.10 Hali Ya Maambukizi Ya Virusi Vya UKIMWI

Kiwango cha maambukizi ni 1.4%, Watu wanaoishi na VVU ni 6,181, wanaotumia dawa ni WAVIU 4, 688, vituo vinavyotoa huduma kwa WAVIU ni 8, na huduma kwa njia ya kliniki ya mkoba ziko 9.

 

1.11 Changamoto

Idara ya afya inapambana na Changamoto zifuatazo: -

1.      Upungufu wa watumishi wenye taaluma mbalimbali kwa asilimia 61.4% 

2.       Kuchelewa kupokea fedha za mfuko wa pamoja na kutokupokea kabisa fedha za kutokana na kutokupata fedha za matumizi mengineyo (OC) ruzuku kutoka serikali kuu tangu mwezi Januari 2016

3.      Wodi zilizopo ni ndogo hazikidhi mahitaji.

4.      Upungufu na uchakavu wa nyumba za watumishi katika ngazi zote za vituo vya huduma.

5.      Maabara ya Hospitali ya wilaya ni ndogo, Halmashauri imeanza funya mawasiliano na marafiki wake wa Tillburg Partnership Uholanzi ili kupata fedha za ujenzi wa Maabara mpya.

6.      Kutokupokea fedha ya kulipa watumishi walioitwa kazini (on call allowance) tangu mwezi Janauri 2016.

 

1.12 Mikakati ya kupambana na Changamoto 

Ili kupambana na changamoto hizo, idara imeweka mikakati ifuatayo:

        i.            Kuomba vibali vya ajira na kuweka vivutio kwa waajiriwa wapya na watumishi kwa ujumla (Staff attraction and Retention strategies)

      ii.            Kushirikiana na Bohari ya dawa (MSD) kuboresha upatikanaji wa dawa na vifaa tiba, kwa kuhakikisha kwamba kila kituo kinaandaa na kutuma taarifa na maombi ya dawa na vifaa – tiba kwa wakati kwenda MSD, na Idara kufuatilia maombi hayo ili yafanyiwe kazi na makasha kusambazwa vituoni kwa wakati muafaka. 

    iii.            Halmashauri tayari imeomba mkopo wa dawa kutoka Mfuko wa Taifya wa Bima ya Afya na inakarabati chumba kwa ajili ya duka la dawa ndani ya hospitali ya Wilaya ili kukabiliana na changamoto ya wagonjwa kununua dawa na vifaa tiba nje ya hospitali.

    iv.            Kushirikisha wadau wengine wa sekta ya Afya katika upatikanaji wa          Vifaa tiba na vitendea kazi Muhimu vya kutolea huduma bora za afya. Hadi sasa Idara imewashirikisha Tillburg Partnership (Uholanzi), PSPF, CRDB na NMB. Bado Idara inatafuta wadau wengine.

      v.            Kuwashirikisha wadau mbalimbali ili kupata fedha za kujengea jengo la kusubiria wajawazito na wodi za wagonjwa katika Hospitali ya wilaya.

    vi.            Kuendelea kuomba fedha serikali kuu kwa ajili ya ruzuku, posho za kuitwa kazini na posho ya kujikimu kwa waajiriwa wapya.

2.0 IDARA YA ELIMU MSINGI

2.1 Utangulizi

Halmashauri ina jumla ya shule za Msingi 192 kati ya hizo shule 185 ni za Serikali na 7 ni za binafsi. Shule hizi ziko katika Kata za Kiutawala 34 na Kata 1 ya Kielimu.. Shule hizi zina jumla ya wanafunzi 59833 kati yao wasichana ni 30613 na wavulana ni 2920. 

2.2 Ufaulu wa Wanafunzi

Kiwango cha kufaulu kwa Mtihani wa Taifa darasa la Saba Kimkoa na Kitaifa ni kama ifuatavyo:-

Jedwali 2.1: Ufaulu wa Mtihani wa Taifa darasa la Saba Kimkoa na Kitaifa

                                   
 

MWAKA

 
 

KIWANGO CHA UFAULU (%)

 
 

NAFASI KIMKOA

 
 

NAFASI TAIFA

 
 

2014

 
 

63.48

 
 

7

 
 

52

 
 

2015 

 
 

75.94

 
 

6

 
 

51

 

Chanzo: Idara ya Elimu Msingi

2.3 Malengo Ya Kuongeza Ufaulu

Ili kufikia malengo ya asilimia themanini na tano ya ufaulu (85%), Halmashauri kupitia idara ya Elimu Msingi imeweka mikakati ya kukabiliana na tatizo la ufaulu duni katika mitihani ya ndani na ya kitaifa kama ifuatavyo: 

o    Kufuatiliaji utendaji kazi wa walimu katika Uongozi na Utawala na Utekelzaji wa Mtaala. Zoezi lilianza kwa kufuatilia shule 35 zilizofanya vibaya zaidi

o    Kuomba walimu toka TAMISEMI ili tuweze kupunguza upungufu mkubwa wa walimu.

o    Kuhamashisha wazazi na walezi kuchangia chakula cha mchana ili wanafunzi wapate chakula cha mchana shuleni.

o    Shule zote zimepewa maagizo ya kutekeleza Ratiba ya ufundishaji wa muda wa ziada ili kurekebisha mapungufu yaliyojitokeza kipindi kilichopita.

o    Halmashauri kwa kushirikiana na wadau mbali mbali wa elimu itaendelea kutoa mafunzo ya mbinu za ufundishaji kwa walimu mfano semina ya somo la Lugha na Hisabati.

o    Idara inaendelea na mpango wa kusoma na kutafisiri mpango wa kuinua taaluma ya Mkoa wa  Katavi ujulikanao kama “ Katavi model” ili uweze kuhawilishwa na kutumika katika wilaya ya Same kwa lengo la kuinua na kuboresha taaluma.

o    Kuhimiza na kusimamia mazoezi ya mwisho wa wiki, mwezi, mitihani ya utamirifu na ile ya Mwisho wa mihula ili kuchochea ushindani katika ngazi ya darasa, shule, Kata, Tarafa, Wilaya na Mkoa.

o    Kupitia na kutekeleza Ushauri na Mapendekezo Mthibiti Ubora wa Elimu shuleni.

o    Kutoa motisha chanya kwa walimu, wanafunzi na shule zilizofanya vizuri katika mitihani ya utamirifu Wilaya, Mkoa na Mitihani ya Kitaifa.

Jedwali 2.2: Miundo Mbinu Ya Shule: Samani Na Majengo

                                                                                                                                   
 

SAMANI

 
 

MAHITAJI

 
 

VILIVYOPO

 
 

UPUNGUFU

 
 

MADAWATI

 
 

26389

 
 

32775

 
 

6387

 
 

MEZA

 
 

2914

 
 

1719

 
 

1195

 
 

VITI

 
 

3211

 
 

1692

 
 

1519

 
 

KABATI

 
 

1714

 
 

523

 
 

1191

 
 

MAJENGO

 
 

 

 
 

 

 
 

 

 
 

NYUMBA ZA WALIMU

 
 

1463

 
 

368

 
 

1095

 
 

MADARASA

 
 

1551

 
 

1298

 
 

253

 
 

VYOO

 
 

2602

 
 

1599

 
 

1003

 
 

STOO

 
 

370

 
 

93

 
 

277

 
 

OFISI

 
 

372

 
 

295

 
 

77

 

Chanzo: Idara ya Elimu Msingi

2.4 Hali Ya Walimu Katika Shule Za Msingi:

Hali ya walimu ni kama ifuatavyo:-

 Jedwali 2.3: Walimu wa Shule Za Msingi Kwa Madaraja

                                                                         
 

SIFA

 
 

MAHITAJI

 
 

WALIOPO

 
 

PUNGUFU

 
 

ME

 
 

KE

 
 

JML

 
 

DARAJA IIIA

 
 

1999

 
 

558

 
 

846

 
 

1404

 
 

 

 

 

 

581

 
 

STASHAHADA

 
 

7

 
 

7

 
 

14

 
 

SHAHADA

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

JUMLA

 
 

565

 
 

853

 
 

1418

 

Chanzo: Idara ya Elimu Msingi

  Jedwali 2.4: Idadi Ya Walimu Katika Shule Za Msingi (Angalia Kiambatisho)

                           
 

MAHITAJI

 
 

WALIOPO

 
 

ASILIMIA

 
 

UPUNGUFU

 
 

ASILIMIA

 
 

1999

 
 

1418

 
 

70.9

 
 

581

 
 

29.1

 

Chanzo: Idara ya Elimu Msingi

2.5 Utoaji wa Chakula Shuleni

 Idadi ya shule zinazotoa chakula katika wilaya Same ni 17 kati ya 185 shule hizo Nasuro, Daghaseta, Mughungani, Mkanyeni, Mwembe, Mshewa, Kafingiro, Goma, Kwizu Mrindi, Manka, Kweresha ,Kiomande, Parane, Ivuga, Mpinji na Tae.

 

2.6 Hali Ya Mimba

Hakuna taarifa ya mwanafunzi aliyepata mimba toka mwezi Januari hadi sasa

 

2.7 Changamoto Mbalimbambali Zilizopo 

Shule za Msingi Wilaya ya Same zinakumbana na changamoto mbali mbali, ambazo zinasababisha ufaulu wa wanafunzi kuwa wa kiwango cha chini. Baadhi ya changamoto hizo ni : 

o    Uhaba wa nyumba za walimu katika maeneo ya shule.

o    Kukosekana kwa chakula cha mchana kwa wanafunzi shuleni.

o    Upungufu mkubwa wa Walimu. 

o    Upungufu wa rasilimali fedha na vifaa kwa ajili ya ufuatiliji utendaji kazi wa walimu

3.0 IDARA YA ELIMU SEKONDARI 

3.1 Utangulizi

Halmashauri ya Wilaya ya Same ina jumla shule 51 za sekondari, kati ya shule hizo 36 ni za serikali na 15 ni za binafsi. Mwaka 2015 shule 47 za sekondari ndizo zilikuwa na watahiniwa wa shule wa Mtihani Taifa kidato cha nne. Shule moja ya Hedaru Sekondari haikufanikiwa kupata matokeo mpaka tathmini hii inafanyika kutokana na kutokuwasilisha nyaraka muhimu Baraza kwa wakati.

3.2 Idadi ya Wanafunzi, kabla na baada ya Uhakiki

Idadi ya Wanafunzi, kabla na baada ya Uhakiki ni kama ilivyoainishwa katika Majedwali hapa chini;

 

 

 

 


Jedwali 3.1: Idadi ya Wanafunzi kabla ya Uhakiki

                       

Chanzo: Idara ya Elimu Secondari

 

Jedwali 3.2: Idadi ya Wanafunzi baada ya Uhakiki

                                                                                                                                                     
 

IDADI YA WANAFUNZI ILIVYO MWEZI  AGOSTI, 2016 BAADA YA UHAKIKI

 

 

KID I

 
 

KID II

 
 

KID III

 
 

KID IV

 
 

KID V

 
 

KID VI

 
 

JUMLA KUU

 

 

ME

 
 

KE

 
 

JML

 
 

ME

 
 

KE

 
 

JML

 
 

ME

 
 

KE

 
 

JML

 
 

ME

 
 

KE

 
 

JML

 
 

ME

 
 

KE

 
 

JML

 
 

ME

 
 

KE

 
 

JML

 
 

ME

 
 

KE

 
 

JML

 

 

2133

 
 

2553

 
 

4686

 
 

1748

 
 

2142

 
 

3890

 
 

1162

 
 

1293

 
 

2455

 
 

1568

 
 

1865

 
 

3433

 
 

438

 
 

0

 
 

438

 
 

459

 
 

0

 
 

459

 
 

7508

 
 

7853

 
 

15361

 


Chanzo: Idara ya Elimu Secondari

 

 

 

 


3.3 Hali ya Ufaulu Katika Mitihani ya Kitaifa

Watahiniwa waliosajiliwa kufanya mtihani huo walikuwa 5044, kati yao wasichana ni 2816 na wavulana ni 2228.watahiniwa waliofanya mtihani walikuwa ni 4958 na waliopata daraja la ufaulu kuanzia daraja I-IV ni 2809 sawa na asilimia 56.6 ya waliofanya mtihani huo, ambapo watahiniwa 2149 walifeli, sawa na asilimia 43.4. Aidha, ufaulu huu umeshuka kwa asilimia 1.6 ukilinganisha na ufaulu wa mwaka 2014 ambapo ulikuwa ni asilimia 58.2.

Aidha, matokeo ya kidato cha pili, 2015, Watahiniwa waliosajiliwa kufanya mtihani wa upimaji walikuwa 4977, kati yao watahiniwa waliofanya mtihani walikuwa 4720 sawa na aslimia 94.8 ya waliosajiliwa. Kati ya Watahiniwa 4720 waliofanya Mtihani wa upimaji wa Taifa kidato cha pili, Watahiniwa waliopata madaraja ya ufaulu walikuwa 3856 sawa na asilimia 82 ya waliofanya mtihani. Watahiniwa waliofeli walikuwa 864 sawa na asilimia 18 ya waliofanya mtihani. 

3.2.1 Mchanganuo wa Ufaulu Kidato cha Nne 

Kufuatia utaratibu ambao  Baraza la Mitihani la Tanzania limetumia kutunuku matokeo ya mtihani wa taifa wa kidato cha nne 2015 kwa kutumia madaraja ya ufaulu kama ilivyokuwa mwaka 2013 na kurudi nyuma, matokeo ya kila shule yameainishwa katika madaraja matano ambayo ni “daraja la kwanza, pili, tatu, nne na waliofeli. Ufaulu huo kimadaraja ni kama ifuatavyo;

Jedwali 3.3: Hali ya ufaulu kimadaraja

Chanzo: Idara ya Elimu Secondari

 

 

 

 

3. 2.2 Nafasi Ya Wilaya Kimkoa Na Kitaifa

Katika mtihani wa taifa wa kidato cha nne (CSEE) mwaka 2014 wilaya ilishika nafasi ya 96. Kwa mwaka 2015 wilaya imeshika nafasi 7 kati ya wilaya 7 kimkoa na nafasi ya 102 kitaifa. Aidha, katika mtihani wa upimaji wa kidato cha pili (FTNA) kwa mwaka 2014, wilaya ilishika nafasi ya 47, na mwaka 2015 wilaya imeshika nafasi ya 57.

3.3  Mikakati ya Kuinua Taaluma Kiwilaya

  1. Kuendelea kufanya ufuatiliaji wa ufundishaji na     ujifunzaji mashuleni katika      kuhamasisha   walimu na     wanafunzi kutimiza wajibu na majukumu yao      ipasavyo
  2. Fomu ya mahdhurio ya walimu darasani na     mahudhurio ya walimu kwa mwezi zimeandaliwa na zinatumika. Ambapo kila     mwisho wa mwezi inawasilishwa ofisi ya Afisa  Elimu ili kujiridhisha namna ufundishaji     na ujifunzaji unavyoendelea shuleni
  3. Mawasiliano yamefanyika  kuiomba serikali kupanga walimu wa     sayansi kwa shule za serikali ambazo zinaupungufu mkubwa
  4. Walimu kuendelea kuandaa na kutumia nyaraka     muhimu za ufundishaji kama inavyoelekezwa na mamlaka husika
  5. Walimu     kufanya tathmini ya mitihani mbalimbali inayofanyika shuleni      

vi.  Wakuu wa shule wameagizwa kushirikiana na waratibu Elimu Kata kudhibiti utoro wa           wanafunzi ambao hawahudhurii masomo badala yake wanakuja siku za mitihani tu.

  1. kutoa     motisha kwa walimu na wanafunzi wanaofanya vizuri katika mitihani ya     taifa.
  2. Kupitia     vikao vya wazazi, WDC bodi za shule msisitizo ni  kwamba wazazi kushirikiana na walimu     pamoja na jamii nzima kutoa malezi mfungamano yatakayosaidia kuboresha     taaluma na kuwafanya wanafunzi kuwa na nidhamu nzuri.
  3. Idara inaendelea na mpango wa kusoma na kutafisiri     mpango wa kuinua taaluma ya Mkoa wa      Katavi ujulikanao kama “ Katavi model” ili uweze     kuhawilishwa na kutumika katika wilaya ya Same kwa lengo la kuinua na     kuboresha taaluma. Aidha, baada ya kusoma na kutafsiri, idara itaandaa     mpango wake na kuwasilishwa kama ilivyoelekezwa.

 

 

 

3.4  Hali ya Madarasa/ Vyoo/ Nyumba za Walimu/Maabara na Mikakati ya ukamilishaji

Kwa upande wa hali ya Madarasa, Vyoo na Nyumba za Walimu ni kama ilivyoainishwa katika jedwali lifuatalo;

Jedwali 3.4: Madarasa, Vyoo, Nyumba za Walimu

Chanzo: Idara ya Elimu Secondari

3.5  Idadi ya Walimu ukilinganisha na Ikama

Kwa upande wa Idati ya Walimu, tuna uhaba mkubwa kwa upande wa Walimu wa Masomo ya Sayansi ukilinganisha na Walimu wa Masomo ya sanaa ambao wapo wakutosha na baadhi ya masomo wamezidi. Mfano katika somo la Kiswahili kuna zidio la Walimu 32 na somo la Kingereza kuna zidio la Walimu 13 kama inavyoonekana katika jedwali hapa chini;

Jedwali 3.5: Idadi ya Walimu Wanaohitajika, Waliopo na Pungufu kwa kila somo

Chanzo: Idara ya Elimu Secondari

3.6 Ukamilishaji wa Maabara

Idara imejitahidi kusimamia ujenzi wa maabara katika shule zote 36, kama ambavyo iliagizwa na Mh. Rais wa awamu iliyopita. Ambapo jumla ya vyumba vya maabara vilivyotakiwa ni 108. Kwa sasa vyumba ambavyo havijakamilika ni vinne (04), vyumba vilivyokamilika ni 104. Ambayo havijakamilika ni katika shule za sekondari Lugulu na Masheko ambazo zote ni shule mpya. Aidha katika baadhi ya shule samani za maabara hazijakamili pia bado kuna upungufu wa vifaa vya ufundishiaji na ujifunzaji kwa masomo ya sayansi.

3.7 Mikakati ya Ukamilishaji

Mikakati iliyopo katika kukamilisha ujenzi wa maabara hizo ni;

  1. WDC kupitia     vikao vyao wameagizwa kuwa ukamilishaji wa ujenzi wa vyumba vya maabara     iwe agenda ya vikao vyao kila wanapokutana.
  2. Wananchi kuendelea kuchangia michango ya     fedha/vifaa vya ujenzi ili kukamilisha ujenzi na kuweka samani katika     vyumba ambavyo bado havina samani.
  3. Wakuu wa shule kuendelea kununua vifaa vya     kufundishia masomo ya sayansi kupita fedha ya ruzuku ya uendeshaji ambayo     hutolewa na serikali kila mwezi.

3.8  Utoaji Wa Chakula Cha Mchana Kwa Wanafunzi wa Kutwa

Hali ya utoaji chakula katika shule za kutwa za serikali kwa sasa siyo nzuri, baada ya tangazo la Elimu bila malipo ambapo shule zote za sekondari zilikuwa zinatoa chakula cha mchana. Aidha, kwasasa idadi ya wanafunzi wanaopata chakula cha mchana ni kama ifuatavyo;  wanafunzi 8445 wanapata chakula na ambao hawapati chakula ni 6916.

Aidha, ofisi imepokea waraka wa Elimu Na. 3 wa mwaka 2016, ambao unawataka wajumbe wa bodi na wazazi kuhakikisha wanafunzi wote wa shule za sekondari za kutwa wanapata chakula cha mchana. Waraka huu umeshapelekwa shuleni kwa ajili ya utekelezaji.  Kama ilivyoelezwa katika kifungu cha 3.7 kamati / bodi za shule za serikali (iii) kushirikiana na wazazi/jamii kuweka utaratibu wa chakula cha mchana au chakula na huduma za hosteli katika shule za kutwa kulingana na mazingira yao, na kutuma mapendekezo kwa MkurugenziMtendaji wa Halmashauri.

 

 

3.9 Mikakati Ya Kudhibiti Utoro Na Mimba Shuleni

Hali ya utoro limekuwa tatizo sugu kwa baadhi ya wanafunzi, hii ni kutokana na baadhi ya wanafunzi kushiriki katika biashara za kuendesha boda boda na shughuli nyingine zinazofanywa na wazazi / walezi.

  1. Watendaji kata na Waratibu Elimu Kata na Wakuu wa     shule wameandikiwa barua kuwachukulia hatua za kisheria wzazi/walezi ambao     aidha kwa kujua au kuto jua watoto wao hawahudhurii masomo bila sababu     zozote.  Barua zilizo andikwa ni za     tarehe 02/06/2016 yenye Kumb. Na. WS/EL/UT.I7/VOL.VI/133. Barua ya     waratibu Elimu Kata yenye Kumb. Na.     WS/EL/UT.17/VOL.180 ya tarehe 22/08/ 2016
  2. Watendaji kata kuwa wachukulia hatua na     kuwafungulia kesi Mahakamani wale wote wanaobainika kuwapa mimba wanafunzi.     
  3. Jamii imehamasishwa kujenga hosteli kwa ajili ya     wanafunzi wanaotembea umbali mrefu, ili wanafunzi wake wakae katika     mabweni rafiki yanayoendeshwa na wazazi.
  4. Walimu kuendelea kutoa ushauri nasaha na unasihi     kwa wanafunzi ili wasome kwa bidii bila kuathiriwa na mazingira ya nje ya     shule. 

Kupitia vikao vya bodi, wazazi /walezi, jamii kutoa malezi mfungamano, basipo kuangalia na kubagua watoto ili kuboresha nidhamu na kuwajengea uwezo wa kujitambua kama sehemu ya jamii wanayoishi.

 

 

 

 

 

 

 

 

Jedwali 3.6: Taarifa za Wanafunzi Watoro, Waliopata Mimba, Waliohama Na Kuhamia pamoja na Wanaopata na Wasiopata Chakula

                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                             
 

S/N

 
 

SHULE

 
 

MIMBA

 
 

WATORO

 
 

WALIOHAMA

 
 

WALIOHAMIA

 
 

WANAOPATA CHAKULA

 
 

WASIOPATA CHAKULA

 


 

ME

 
 

KE

 
 

JML

 
 

ME

 
 

KE

 
 

JML

 
 

ME

 
 

KE

 
 

JML

 

 

1

 
 

BANGALALA

 
 

4

 
 

6

 
 

7

 
 

13

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

106

 
 

81

 

 

2

 
 

BEMKO

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

408

 
 

0

 

 

3

 
 

BOMBO 

 
 

2

 
 

3

 
 

4

 
 

7

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

46

 
 

310

 

 

4

 
 

CHALAO

 
 

3

 
 

3

 
 

2

 
 

5

 
 

2

 
 

3

 
 

 

 
 

3

 
 

0

 
 

3

 
 

539

 
 

0

 

 

5

 
 

CHANJAGAA

 
 

1

 
 

3

 
 

5

 
 

8

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

100

 
 

112

 

 

6

 
 

GONJA

 
 

3

 
 

27

 
 

9

 
 

36

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

835

 

 

7

 
 

KASEMPOMBE

 
 

2

 
 

10

 
 

8

 
 

18

 
 

4

 
 

2

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

180

 
 

171

 

 

8

 
 

KAZITA 

 
 

3

 
 

3

 
 

2

 
 

5

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

183

 
 

0

 

 

9

 
 

KIBACHA

 
 

2

 
 

13

 
 

15

 
 

28

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

765

 
 

0

 

 

10

 
 

KIGANGO

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

160

 
 

0

 

 

11

 
 

KIHURIO

 
 

2

 
 

2

 
 

4

 
 

6

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

193

 
 

349

 

 

12

 
 

KIMALA

 
 

1

 
 

7

 
 

9

 
 

16

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

491

 
 

0

 

 

13

 
 

KIRANGARE

 
 

1

 
 

4

 
 

2

 
 

6

 
 

4

 
 

1

 
 

0

 
 

0

 
 

6

 
 

0

 
 

50

 
 

363

 

 

14

 
 

KISIWANI

 
 

4

 
 

2

 
 

0

 
 

2

 
 

2

 
 

0

 
 

0

 
 

3

 
 

3

 
 

6

 
 

730

 
 

0

 

 

15

 
 

KWAKOKO

 
 

4

 
 

7

 
 

10

 
 

17

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

405

 
 

0

 

 

16

 
 

KWIZU

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

1

 
 

0

 
 

1

 
 

1

 
 

0

 
 

1

 
 

375

 
 

0

 

 

17

 
 

LUGULU

 
 

3

 
 

2

 
 

2

 
 

4

 
 

13

 
 

26

 
 

39

 
 

11

 
 

18

 
 

29

 
 

78

 
 

124

 

 

18

 
 

MABILIONI

 
 

1

 
 

2

 
 

1

 
 

3

 
 

2

 
 

7

 
 

9

 
 

2

 
 

16

 
 

18

 
 

140

 
 

306

 

 

19

 
 

MADIVENI

 
 

1

 
 

11

 
 

18

 
 

29

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

300

 
 

0

 

 

20

 
 

MAKANYA

 
 

1

 
 

13

 
 

6

 
 

19

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

497

 
 

0

 

 

21

 
 

MALINDI

 
 

0

 
 

2

 
 

0

 
 

2

 
 

1

 
 

1

 
 

2

 
 

2

 
 

0

 
 

2

 
 

153

 
 

117

 

 

22

 
 

MASHEKO

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

130

 
 

75

 

 

23

 
 

MKOMBOZI

 
 

3

 
 

22

 
 

0

 
 

22

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

48

 
 

1091

 

 

24

 
 

MOIPO

 
 

1

 
 

23

 
 

12

 
 

35

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

219

 
 

143

 

 

25

 
 

MTII

 
 

3

 
 

3

 
 

2

 
 

5

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

100

 
 

213

 

 

26

 
 

MVUREKONGEI

 
 

4

 
 

2

 
 

3

 
 

5

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

184

 

 

27

 
 

MYAMBA

 
 

0

 
 

1

 
 

0

 
 

1

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

245

 
 

321

 

 

28

 
 

NDUNGU

 
 

3

 
 

4

 
 

0

 
 

4

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

687

 

 

29

 
 

NTENGA

 
 

2

 
 

2

 
 

4

 
 

6

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

618

 

 

30

 
 

PARENI

 
 

2

 
 

1

 
 

2

 
 

3

 
 

3

 
 

4

 
 

7

 
 

0

 
 

0

 
 

 

 
 

274

 
 

0

 

 

31

 
 

SAME 

 
 

0

 
 

2

 
 

0

 
 

2

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

756

 
 

0

 

 

32

 
 

SAWENI

 
 

0

 
 

6

 
 

12

 
 

18

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

252

 
 

0

 

 

33

 
 

TAE

 
 

0

 
 

6

 
 

8

 
 

14

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

145

 
 

72

 

 

34

 
 

VUDEE

 
 

1

 
 

6

 
 

4

 
 

10

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

198

 
 

58

 

 

35

 
 

VUMARI

 
 

0

 
 

7

 
 

8

 
 

15

 
 

6

 
 

4

 
 

10

 
 

4

 
 

5

 
 

9

 
 

96

 
 

459

 

 

36

 
 

VUNTA

 
 

0

 
 

9

 
 

5

 
 

14

 
 

0

 
 

2

 
 

2

 
 

0

 
 

0

 
 

0

 
 

83

 
 

227

 

 

 

 
 

JUMLA

 
 

57

 
 

214

 
 

164

 
 

378

 
 

38

 
 

50

 
 

88

 
 

26

 
 

48

 
 

68

 
 

8445

 
 

6916

 

4.0              IDARA YA MAJI

4.1              Upatikanaji wa Huduma ya maji 

Upatikanaji wa maji vijijini ni 70% na Vijiji vyenye maji ni 75

4.2 Mpango uliopo kwa mji wa Same

Mradi wa Maji wa Same – Mwanga – Korogwe unalenga kuhudumia watu 456,931 ifikapo mwaka 2038 katika Wilaya za Same (watu 264,793), Mwanga (watu 177,085) na watu 15,053 katika Wilaya ya Korogwe, kwenye vijiji 38 na miji ya Same na Mwanga. Mifugo na viwanda vidogo pia vitanufaika na mradi huu.

 Katika Vijiji 38 vitakavyonufaika Vijiji vya Same ni Hedaru, Mabilioni, Gavao, Makanya, Mgwasi, Bangalala, Chajo, Mwembe, Njoro, Ishinde, Ruvu Mferejini, Ruvu Jiungeni, Majengo, Bendera, Mkonga Ijinyu, Mgandu (vijiji 16 katika Wilaya ya Same) 

4.3 Utekelezaji wa Mradi

  1. Kwasasa awamu ya kwanza imeshaanza ambayo ni ujenzi     wa wa chanzo na mitambo ya kutibu maji eneo la nyumba ya mungu (     Kisangara) na itakamilika ifikapo may 2017

      ii.            Awamu ya nne ambayo ni kulete maji katika Mji wa Same, Mkandarasi ameshapatikana, anaitwa Badri East Africa Limited na alishafika eneo la kazi kujitambulisha. Ataanza kazi mara baada ya kusaini Mkataba na kulipwa malipo ya awali. Pia ataweka kambi (Camp Site) maeneo ya Same Mjini na Kijiji cha Njoro. Gharama za awamu hii ni  USD 52 milion sawa na shilingi 104 bilioni


5.0              KITENGO CHA ARDHI

Sekta ya ardhi ni mojawapo ya sekta iliyopo chini ya idara ya ardhi na maliasili inayosimamia masuala yote ya ardhi. Sekta ina sehemu 4 ambazo ni ardhi utawala, mipango miji, upimaji na ramani na uthamini. Idadi ya Vijiji vilivyopimiwa Ardhi, Idadi ya Vijiji vilivyofanyiwa Matumizi bora ya Ardhi, Idadi ya Migogoro Sugu ya Ardhi Mjini na Vijiji, Sababu za kutokea kwa Migogoro ya Ardhi na kusababisha migogoro hiyo kuwepo kwa muda mrefu, Mipango/Mikakati ya kumaliza Migogoro ya Ardhi, Mipango/Mikakati ya kuboresha Mji/Master plan, Hali ya Ukusanyaji wa Kodi za Viwanja na Nyumba pamoja na Idadi ya Miji yenye Sifa ya kuwa Miji Midogo ni kama ilivyoainishwa katika jedwali hapa chini;

 

 


Jedwali 5.1: Hali ya Utekelezaji wa Shughuli za Kitengo cha Ardhi

                                                   
 

S/N

 
 

VIJIJI  VILIVYOPIMWA

 
 

VIJIJI  VILIVYOGAWANYIKA

 
 

VIJIJI  VYENYE MATUMIZI BORA YA ARDHI

 
 

MIGOGORO  SUGU

 
 

MIGOGORO  YA KAWAIDA

 
 

SABABU ZA  MIGOGORO

 
 

MIKAKATI  YA KUMALIZA MIGOGORO

 
 

MIPANGO  YA KUBORESHA MJI

 
 

UKUSANYAJI  WA KODI ZA ARDHI/MAJENGO

 
 

MIJI  YENYE SIFA YA KUWA MIJI MIDOGO

 
 

1

 
 

Halmashauri ya Wilaya ya  Same ina jumla ya vijiji 100 kati ya Vijiji hivyo vilivyopimwa vilikuwa ni  vijiji  84, kati ya vilivyokuwa  vimepimwa vijiji saba (7) vimegawanyika kati ya Vijiji hivyo sasa  vilivyogawanyika vimezaliwa Vijiji 16

 
 

-Chajo kimegawanyika  na kuwa Kijiji cha Chajo na Nasuro.

 

-Tae  kimegawanyika na kuwa Kijiji cha Tae, Heikonti  na Rikweni.

 

-Njoro  kimegawanyika na kuwa Kijiji cha Njoro na Emuguri.

 

-Gavao Saweni  kimegawanyika na kuwa Kijiji cha Gavao Ngarito na Saweni.

 

-Mabilioni kimegawanyika  na kuwa Kijiji cha Mabilioni, Ruvu mbuyuni na Chekereli.-Hedaru kimegawanyika na kuwa Kijiji cha Hedaru, Kijomu na  Gundusine. Bangalala kimegawanyika  na kuwa Kijiji cha Bangalala na Mkanyeni.

 
 

Duma, Lugulu, Kanza na  Mtii, Makanya, Hedaru na Gavao Saweni.

 

 

 

Kutokana na ufinyu wa  bajeti Halmashauri imefanikiwa kuandaa mpango wa matumizi bora ya ardhi ya  vijiji saba (7) kupitia ufadhili wa wadau wa maendeleo kama TFCG na Ongawa.

 
 

-Kijiji cha Makanya na  Ruvu

 

 

 

- Kijiji cha Mgwasi na  Makanya, 

 

 

 

Kitongoji cha Kavambughu  Ishinde. 

 

 

 

-Maore na Mheza.

 

 

 

-Migogoro ya wakulima na  wafugaji kata ya Ruvu.

 
 

Migogoro ya kawaida  haiwezi kuhesabika kwani huibuka na kupatiwa ufumbuzi.

 

 

 

Baadhi ya wananchi wanadai  kuchukuliwa maeneo yao bila kulipwa fidia.

 
 

Kukosewa mipaka ya vijiji  katika ramani zilizopimwa na Wizara ya Ardhi

 

Wananchi kujenga bila  vibali vya ujenzi kutoka mamlaka husika.

 
 

Kukagua vijiji vyenye  migogoro ya mipaka na kuiandikia Wizara barua ili waje warekebishe mipaka  hiyo. 

 

Kuandaa mipango ya  matumizi bora ya ardhi ili kumaliza migogoro ya wakulima na wafugaji.

 

 

 

Kubaini na kuhakiki  uhalali wa madai ya wananchi ambao wanadai maeneo yao kuchukuliwa bila  kulipwa fidia.

 

Halmashauri  kutafuta eneo kwa ajili ya kulipima ili  kuwafidia wananchi hao. 

 
 

Maandalizi yanafanyika ili  kutenga fedha katika bajeti ijayo ili kuandaa master plan (Mpango kamambe) wa  mji wa Same.

 
 

Ukusanyaji wa kodi za  ardhi unaendelea vizuri. 

 

Kodi ya majengo ndani ya  Mamlaka ya Mji mdogo hukusanywa na mamlaka ya   Mji mdogo wa Same kama mapato ya ndani.

 
 

Katika Halmashauri ya  Wilaya ya Same ipo miji ya kibiashara ambayo inakuwa kwa kasi na ina sifa ya  kuwa miji midogo ambayo ni Hedaru,

 

 

 

Makanya, 

 

 

 

Kisiwani, 

 

 

 

Maore na 

 

 

 

Ndungu.

 

Chanzo: Kitengo cha Ardhi


6.0              IDARA YA KILIMO

6.1              Eneo la  Kilimo na Mazao yanayolimwa

Eneo linalofaa kwa shughuli za kilimo katika Wilaya ya Same linakadiriwa kuwa na jumla ya hekta 45,000. Eneo linalofaa kwa kilimo cha umwagiliaji ni takriban hekta 20,000 ambazo kati ya hizo ni hekta 12,200 zinazotumika kwa umwagiliaji wa kisasa na wa asili. 

 

Fursa zilizopo Wilayani kwa ajili ya shughuli za kilimo ni pamoja na kuwa na bonde zuri lenye maji ya mito upande wa Same Mashariki ukanda wa tambarare. Eneo hili lina Skimu za umwagiliaji ambapo mazao mbalimbali ya chakula na biashara huzalishwa kama vile Mpunga, mahindi, maharage na mbogamboga. Upande wa Magharibi hutegemea zaidi Mto Pangani ambapo kuna kilimo cha umwagiliaji wa mazao ya mahindi, mpunga na mbogamboga. Upande huu ndio wenye eneo kubwa la malisho kwa upande wa ufugaji. 

Mazao ya biashara yanayolimwa katika Wilaya yetu ni Tangawizi, Pamba, Fiwi na Kahawa, na Iliki. Mazao ya chakula ni pamoja na mahindi, mpunga na mtama. Mazao aina ya mikunde ni pamoja na maharage na fiwi, mazao mengine ni viazi vikuu, viazi mviringo na mihogo. Aidha Wilaya inazalisha pia aina kadhaa za mbogamboga na matunda ikiwemo ndizi, matango, tikitimaji, na nyanya.

 

6.2              Malengo ya Kilimo na Matarajio ya mavuno

Wilaya hii ni mojawapo ya Wilaya zinazokabiliwa na upungufu wa chakula mara kwa mara. Hali hii inasababishwa na mvua chache zinazosababishwa na mabadiliko ya tabia nchi ambayo huathiri ustawi wa mazao ya kilimo hasa maeneo ya tambarare. 

Katika msimu wa kilimo wa mwaka 2016/2017 halmashauri ya wilaya ya same imeweka malengo ya kulima hekta 39,700 ambapo kiasi cha tani 208,297 cha mazao mbalimbali kinatarajiwa kuzalishwa, ambapo tani 155,668 ni mazao ya chakula, tani 3,289 ni mazao ya biashara, tani 26,403 ni mbogamboga, tani 7,440 ni matunda na tani 15,506 ni Viungo.

 

 

 

 

 

 

 

 

               Jedwali 6.1: Malengo ya kilimo na utekelezaji wa mazao muhimu  

                                                                                                                                                                                                                                                                                                           

 

2015/2016

 
 

2016/2017

 
 

LENGO

 
 

UTEKELEZAJI

 
 

LENGO

 
 

Ha

 
 

Tani

 
 

Ha

 
 

Tani

 
 

Ha

 
 

Tani

 
 

MAZAO YA CHAKULA

 
 

Mahindi

 
 

20,500

 
 

48,000

 
 

19,781

 
 

63,299

 
 

15,200

 
 

50,000

 
 

Mpunga

 
 

3,200

 
 

19,200

 
 

3,300

 
 

16,500

 
 

3,200

 
 

24,000

 
 

Mtama

 
 

500

 
 

500

 
 

100

 
 

80

 
 

500

 
 

800

 
 

Maharage

 
 

1,500

 
 

1,320

 
 

1,250

 
 

1,100

 
 

1,500

 
 

1,400

 
 

Muhogo

 
 

3,140

 
 

31,400

 
 

3,140

 
 

29,400

 
 

3,140

 
 

32,000

 
 

Ndizi

 
 

3,200

 
 

32,000

 
 

3,200

 
 

31,100

 
 

3,200

 
 

32,000

 
 

Viazi Vitamu

 
 

600

 
 

3,000

 
 

550

 
 

2,750

 
 

600

 
 

3,000

 
 

Viazi Mviringo

 
 

350

 
 

3,500

 
 

300

 
 

3,000

 
 

350

 
 

3,500

 
 

JUMLA

 
 

32,990

 
 

138,920

 
 

31,621

 
 

147,229

 
 

27,690

 
 

146,700

 
 

MAZAO YA BIASHARA

 
 

Pamba

 
 

80

 
 

120

 
 

50

 
 

60

 
 

80

 
 

120

 
 

Tangawizi

 
 

1,200

 
 

13,500

 
 

1,250

 
 

14,500

 
 

1,350

 
 

15,500

 
 

Kahawa

 
 

1,650

 
 

660

 
 

1,500

 
 

320

 
 

1,650

 
 

660

 
 

Fiwi

 
 

4,000

 
 

8,000

 
 

3,500

 
 

5,250

 
 

4,200

 
 

8000

 
 

JUMLA

 
 

6,930

 
 

22,280

 
 

6,300

 
 

20,130

 
 

7,280

 
 

24,280

 

                Chanzo: Idara ya Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika

6.3 Hali ya Chakula na mikakati ya kumaliza njaa

Kwa mwaka 2015/16 hali ya chakula Wilayani Same ilikuwa ya kuridhisha kutokana na mvua kunyesha kiasi cha kutosha. Kimsingi mahitaji ya chakula (nafaka) kwa mwaka ni tani 81,101 ambapo kila mtu mzima anastahili kiasi kisichopungua gunia 3 za mahindi kwa mwaka, makadirio haya ni kutokana na idadi ya watu iliyopo ndani ya Wilaya (Watu 269,807), na hii ni kwa mujibu wa Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012.  Uzalishaji wa chakula katika maeneo ya skimu za umwagiliaji za Ndungu, Maore, Kisiwani na sehemu za Kata ya Bendera nao umeongezeka kutokana na jitihada kubwa zilizofanyika za kuongeza uzalishaji katika maeneo ya umwagiliaji.

6.4  Mipango ya Wilaya  wa kuongeza uzalishaji na kabiliana na upungufu wa chakula

·      Kuhakikisha elimu ya uvunaji maji ya mvua, matumizi bora ya maji  na hifadhi ya ardhi na udongo imetolewa kwa wakulima.

·      Kutoa elimu kwa wakulima juu ya kuzuia/kupunguza upotevu wa

     mazao ya nafaka na mikunde wakati wa kuvuna na kuhifadhi    

     (Post harvest loss handling).

·      Kuhakikisha elimu ya ukadiriaji wa mahitaji ya mazao ya chakula kwa wakulima ngazi ya kaya imetolewa.

·      Kutoa elimu kwa wakulima juu ya hifadhi na matumizi bora ya mazao ya chakula kwa maeneo ambayo yamepata mavuno mazuri msimu wa vuli hasa maeneo ya kilimo cha umwagiliaji.

·      Kutoa ushauri kwa wakulima kutekeleza kilimo cha mazaoyanayostahimili ukame na yanayotumia kiasi kidogo cha unyevu hadi kukomaa kama  mazao jamii ya mizizi na mikunde na Mtama.

·      Kuhakikisha uimarishaji wa matumizi bora ya maji katika  miundombinu ya umwagiliaji iliyopo na kuhakikisha kunakuwepo na ongezeko la uzalishaji wa mazao ya chakula kwa misimu miwili na wakulima wanazingatia ushauri wa wataalam waliopo vijijini.

·      Kwa kuwatumia Maafisa Ugani waliopo kuhakikisha wakulima wanatumia teknolojia bora na sahihi za uzalishaji mazao ya chakula na biashara kwa ajili ya uhakika na usalama wa chakula ngazi ya kaya.

·      Kuhimiza wafugaji walio na mifugo kuuza wakati bado ikiwa na hali nzuri ya kiafya na kununua chakula na kuhifadhi kwa ajili ya matumizi ya familia.

·      Kuhimiza wakulima waliopo maeneo ya umwagiliaji kulima mazao yenye thamani na ubora kwa uhakika wa kuongeza kipato hatimaye kumudu kujinunulia chakula cha kutosha.

·      Kuhamasisha wafanyabiashara wenye uwezo  kununua chakula Katika maeneo yenye chakula cha ziada na kuleta kuuza katika maeneo yenye upungufu kwa bei nafuu/elekezi.

 

 

 

 

6.5  Mikakati ya mnyororo wa thamani wa mazao

Halmashauri ya Wilaya iliteua kuendeleza mnyororo wa thamani kwa mazao mawili ya biashara ambayo ni Tangawizi na Mpunga.

 

Kwa zao la tangawizi Halamashauri ikishirikia na wadau wengine imekuwa na mikakati ya kuboresha miundo mbinu ya umwagiliaji katika maeneo yanayozalisha tangawizi ili kuimarisha kilimo cha umwagiliaji kwa zao hilo. Vilevile kwa kupitia mradi wa MIVARF Halmashauri imekuwa na mikakati ya kuboresha miundo mbinu ya mawasiliano katika maeneo yanayolimwa zao hilo, pia kujengea uwezo wakulima wa tangawizi kwa kuwapa mafunzo ya kilimo bora cha tangawizi na kuwaunganisha na masoko.

Kwa zao la mpunga Halmashauri imekua na mikakati ya kuboresha miundo mbinu ya umwagiliaji katika maeneo yanayolimwa mpunga na kutoa mafunzo kwa wakulima wa mpunga kwa kuanzisha mashamba ya mfano na mashamba darasa. Aidha Halmashauri imekua na mikakati ya kufufua na kuhakikisha kinu cha kukoboa mpunga katika skimu ya Ndungu kinafanya kazi ili kuongeza thamani ya zao la mpunga.

 

6.6  Uendelezaji viwanda

6.6.1 Kiwanda cha Tangawizi

Wilaya ya Same ni miongoni mwa Wilaya zinazozalisha Tangawizi kwa wingi hapa nchini, ambapo inakadiriwa kuwa zaidi ya tani 14,500 zinazalishwa kila mwaka. Wakulima wengi hasa wa maeneo ya milimani hutegemea na kutumia zao hili kama zao la biashara. Kutokana na hali hiyo Ushirika wa wakulima wa Tangawizi Mamba Myamba uliamua kujenga kiwanda ili kuongeza thamani ya zao la Tangawizi. Kiwanda kilizinduliwa na Mhe. Rais Mstaafu mnamo mwaka 2012. Baada ya kuzinduliwa kiwanda kiliweza kusindika zaidi ya tani 100 za Tangawizi na kuziuza.

Katika uendeshaji baadhi ya mitambo ilieonekana kutofanya kazi vizuri na hivyo kuhitaji kuboreshwa. Hali hii ilipelekea kiwanda kusimama kwa muda na hivyo Shirika la SIDO wametakiwa kutengeneza na kuirekebisha mitambo hiyo.  SIDO ndio waliosanifu na kutengeneza mitambo yote ya kiwanda hicho na wanaendelea kushirikiana na ushirika pale mitambo inapoleta hitilafu.

Soko la Tangawizi mbichi na iliyosindikwa lipo la kutosha nje na ndani ya nchi. Serikali kupitia Mradi wa uboreshaji miundo mbinu ya masoko na uongezaji thamani (MIVARF) kwa kushirikiana na Shirika la Faida Mali inaendelea kusaidia ushirika huo kutafuta na kuwaunganisha na masoko ya uhakika. Tayari masoko yafuatayo yameshapatikana Kampuni ya Afri Tea, kampuni ya Tausi, TAQWA, Kampuni ya India market na Kampuni ya lion wattle.  Wanunuzi waliopatikana wapo tayari kununua tangawizi iliyosindikwa mara tu kiwanda kitakapoanza tena kufanya kazi.Kwa sasa bei ya Tangawizi ni Tshs. 1300 – 1500 kwa kilo ya tangawizi mbichi.

Zipo Changamoto za msingi zinazokabili ushirika kwa sasa, ambazo zinasababisha kiwanda kisifanye kazi vizuri. Changamoto hizo ni pamoja Uelewa mdogowa viongozi wa ushirika waliopo kwa sasa juu ya usimamizi na uendeshaji wa kiwanda, na Ukosefu wa mtaji wa kutosha kununua malighafi (Tangawizimbichi) kuajiri na kulipa watumishi na kulipia gharama za uendeshaji.

Hatua zinaendelea kuchukuliwa ili kuhakikisha kiwanda kinafanya kazi vizuri. Hatua hizo ni pamoja na Kuimarisha na kujengea uwezo viongozi wa ushirika na wanachama ili kuweza kujipanga na kuepuka bei zisizokuwa na maslahi zinazopangwa na wafanyabiashara. Aidha mafunzo yametolewa juu ya usimamizi na utunzaji wa fedha ili baada ya kuwa na uelewa wa kutosha waweze kuomba na kupata mkopo kutoka kwenye taasisi za fedha na hatimaye kuendesha kiwanda. 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

7.0              KITENGO CHA MALIASILI NA MAZINGIRA

7.1              Maliasili zilizopo Wilayani

7.1.1 Misitu Iliyopo

Wilaya ya Same ina jumla ya hakari 256,503 za misitu ambayo ni sawa na asilimia 20.3 (20.3%) ya eneo lote la Wilaya ya Same ambalo ni Kilomita za mraba 5,186 (5,186Km2). Misitu hii ni ya aina mbalimbali kama kama misitu ya Kupandwa, Mataji wazi (Miombo Woodland), Hifadhi za Serikali (Cathment Forests), Hifadhi za Vijiji na Hifadhi za kimila (Itasio).

7.1.2 Wanyamapori

Kitengo cha wanyamapori kina dhamana ya kuhifadhi rasilimali wanyamapori iliyoko kwenye maeneo ya wazi yenye wanyamapori kama vile Ruvu, kuwarudisha wanyamapori watoka nje ya na hifadhi ya taifa ya Mkomazi. Maeneo yaliyohifadhiwa yanachangia uhifadhi wa bioanuai mbalimbali ili zisitoweke kama vile tembo, nyani, kiboko, nyati, simba, mbwa mwitu pamoja na aina mbalimbali za ndege.

7.2              Utunzaji wa Maliasili zilizopo Wilayani

Wilaya ya Same ina jumla ya Misitu ya Hifadhi 17 ambayo kati ya misitu hiyo, Misitu minne (4) ipo chini ya Serikali kuu, Misitu tisa (9) chini ya Halmashauri na Misitu (4) ipo chini ya Vijiji. 

Usimamzi wake unategemea na mmiliki ambapo Misitu ya Serikali kuu husimamiwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Misitu ya halmashauri husimiwa na Halmashauri ya Wilaya kupitia Kitengo cha Maliasili na Misitu ya Vijiji inasimamiwa na Vijiji kupitia Kamati za Maliasili za Vijiji. Misitu hii husimamiwa kupitia mipango ya usimamizi ya misitu husika ambapo shughuli za Doria, Upandaji wa Misitu, kulinda mipaka ya hifadhi na kuzuia matukio ya moto hufanyika.

Kitengo hiki kinatunza rasilimali wanyamapori kwa kuwalinda dhidi ya majangili kwa kufanya doria mara kwa mara kwenye maeneo yenye wanyamapori  ili kuwalinda dhidi na ujangili.  Rasilimali hii pia inatunzwa kwa kuhakikisha kuna udhibiti na usimamizi wa umilikaji wa nyara kama vile kutoa kibali kwenye ukamataji wa ndege kama vile kanga. 

Endapo wanyamapori watatoka nje ya hifadhi ya taifa ya Mkomazi au maeneo ya wazi na kwenda kwenye makazi na mashamba ya wananchi, ni jukumu la watumishi wa kitengo cha wanyamapori kuwarudisha kwenye hifadhi.

Pia hufanyika udhibiti wa wanyamapori waharibifu hususani viboko ambao huvamia maeneo ya wananchi na wakati mwingine kusababisha vifo au madhara kwa watu na mazao mashambani kwa kuwarudisha katika makazi yao. Aidha kumekuwa pia na udhibiti wa wanyamapori kama tembo na simba wanaotoka katika hifadhi ya taifa Mkomazi. Zoezi la kuwarudisha hifadhini hufanyika haraka iwezekanavyo ili wasilete madhara kwa wananchi na mali zao. Viongozi wa kata au vijiji husika huimizwa kutoa taarifa pindi wanyamapori hao watakapoonekana katika maeneo yao. Pia elimu dhidi ya kujikinga na wanyamapori hao hatari kwa mali na uhai wa wananchi hutolewa kwa wananchi ili kuwasaidia katika kujikinga na wanyamapori hao na kutoa taarifa katika Idara ya Ardhi na Maliasili.

7.3              Jinsi Maliasili zilizopo Wilayani zinavyochangia Uchumi

Misitu huchangia uchumi kupitia mapato yanayokusanywa na Halmashauri ya Wilaya na Serikali kuu kutokana na tozo mbalimbali za mazao ya misitu na mazao yasiyo ya misitu lakini yanayopatikana ndani ya misitu mfani ukindu. Tozo zinazokusanywa na Halmashauri ni zile zitokanazo na mbao, nguzo za umeme, simu na za kujengea, magome ya miti na mizizi kwa ajili ya dawa mbalimbali. Tozo zinazokusanywa na Serikali kuu ni zile za Usajili wa Biashara ya mazao ya misitu, kibali cha kusafirishia mazao ya misitu (Transit Pass) na mrahaba wa mazao ya misitu yaliyovunwa katika misitu ya asili.

Rasilimali hii inachangia kwenye uchumi kwa kutoa kibali cha ukamaji wa wanyamapori kama vile ndege aina ya kanga kwenye maeneo ya wazi yanayopatikana katika ya wilaya Same. . Kibali hicho kinatolewa na Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Idara ya Wanyamapori na kuidhinishwa na Mkurugenzi wa Wanyamapori na kumtaka Afisa Wanyamapori wa wilaya kumruhusu mdau huyo kukamata wanyama walioidhinishwa. Fungu la fedha lililotokana na ukamataji wa wanyamapori hao hugawiwa kwa Halmashauri husika.

Hata hivyo  maeneo ya wazi yaliyotengwa kwa ajili ya uhifadhi kama vile Pori Tengefu (Ruvu-Same Game Controlled Area) yanakabiliwa na uharibifu mkubwa kutokana na shughuli za kibinadamu  kama vile uvamizi wa mifugo na shughuli za kilimo na ujangili kwenye maeneo yaliyohifadhiwa  hivyo kusababisha kutokuwepo na wanyama wa kutosha kwa ajili ya shughuli za uwindaji ambazo zingeweza kuiletea halmashauri pato.

 

 

7.4                Upandaji wa Miti

Upandaji wa miti hufanyika kwa kuzingatia lengo la mwaka liliowekwa kwa kila Wilaya ambapo kwa Wilaya ya Same lengo la mwaka 2015/2016 lilikuwa ni kupanda miti 1,500,000. 

Aidha pamoja na zoezi la upandaji wa miti, uhamaishaji wa uanzishaji wa vitalu vya miti hufanyika kwa jamii ili kupata vyanzo vya miche kwa ajili ya kupanda. Mpaka sasa jumla ya vitalu vya miti 35 vimeanzishwa na jamii katika Kata za Hedaru, Vunta, Makanya, Maore, Kisiwani, Vumari, Mtii, Bombo na Myamba. Kitalu cha Halmashauri kilichopo Mwembe kina jumla ya miti 9,780. Jumla ya miti 1,351,763 imeshapandwa mpaka sasa ndani ya Wilaya kati ya miti 1,500,000 iliyotarajiwa kupandwa kwa Mwaka 2015/2016 sawa na asilimia 90.01 (90.01%).

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

8.0              IDARA YA UTAWALA NA UTUMISHI/RASILIMALI WATU

8.1              Idadi ya Watumishi waliopo kulingana na Ikama

 

 

 

 

 

8.2              Taarifa ya Watumishi Hewa

 

 

 

 

 

 

8.3              Kiasi cha Fedha zilizopoyea kutokana na Watumishi Hewa

 

 

 

 

 

 

 

8.4              Mikakati/Hatua zilizochukuliwa ili kurejesha Fedha zilizopotea kutokana na Watumishi Hewa

 

 

 

 

 

 

 

 

 

8.5              Matatizo ya Watumishi na Namna Yanavyoshughulikiwa

Tangu January 2016 hadi sasa kuna jumla ya Matatizo ya Watumishi...........yaliyoshughulikiwa na matatizo.......... yanaendelea kushughulikiwa

 

 

8.6              Hali ya Vikao vya Kisheria Ngazi ya Wilaya, Kata na Vijiji na Hatua za kuvisimamia

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

8.7              Hatua zinazochukuliwa kwa kutofanya Vikao

 

 

 

 

 

 

8.8              Motisha zilizopo kwa Watumishi/ Viongozi

 

 

 

 

 

 

 

 

8.9              Utowaji wa Mafunzo ya kuwajengea Uwezo Watumishi /Viongozi

 

 

 

 

 

 

 

8.10          Zana za Ufuatiliaji Watumishi kwa kila Idara

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Ø  KITENGO CHA SHERIA

8.1 Idadi ya Kesi

Halmashauri  ya Wilaya ya Same kama zilivyo Taasisi nyingine za kisheria ina uwezo wa kushitaki na kushitakiwa na katika kipindi cha 2015 hadi 2016 imekuwa na mashauri mbali mbali katika Mahakama ya Wilaya, Mahakama Kuu na Baraza la Ardhi na Nyumba Same.

·        Katika kipindi cha 2015 hadi 2016 Halmashauri imefungua kesi mbili  moja Baraza la Ardhi na Nyumba Same ambayo ni shauri la Madai kati ya Mamlaka ya  Mji Mdogo Same dhidi ya Helios Tower Infanco Tanzania Ltd na Mahakama Kuu Moshi ya Halmashauri ya Wilaya dhidi ya Eliwaha Mbaga na Wenzake. Kesi hizi ziko katika hatua za awali.

Katika kipindi cha 2015 hadi 2016 Halmashauri  imeshitakiwa katika Mahakama ya Wilaya, Mahakama Kuu na Baraza la Ardhi na Nyumba Same na jumla ya mashauri matano(5) yalifunguliwa dhidi yake. Mashauri dhidi ya Halmashauri ni ya Eiza Mkaze dhidi ya Halmashauri na Mwingine, Ramadhani Kanyama Msuya dhidi ya Halmashauri, Christina Elieskia na Miriam Kajiru dhidi ya Mkutugenzi Mtendaji Wilaya, Cheavo Johnson Kihara dhidi ya TANESCO na Halmashauri ya Wilaya na Octavius Leole dhidi ya Halmashauri ya Wilaya. Kesi hizi bado ziko kwenye hatua mbalambali za usikilizwaji na ya Christina na mwenzake imeamuliwa kwa njia ya usulihishi CMA na imerudishwa TSC kwa hatua zaidi

8.2  Mikakati ya kushinda Kesi na kuhakikisha Mikataba inakuwa na Tija kwa Halmashauri na Serikali

Halmashauri ya Wilaya ya Same kupitia Kitengo cha Sheria imejipanga kushinda katika kesi zote kwa kuhudhuria Mahakamani kufuatana na kalenda za Mahakama na kutoa ushahidi thabiti kwa mujibu wa sheria pia kushawishi utatuzi wa migogoro nje ya mahakama pale inapobidi kufanya hivyo ili kuepuka upotevu wa muda na rasilimali fedha.

Kitengo cha Sheria kinashughulika na uandaaji wa mikataba mbalimbali baina ya Halmashauri na wadau wake na vilavile kuandaa mikataba ya watumishi walioruhusiwa kwenda masomoni.

Katika hili Kitengo kinazingatia kanuni,taratibu na sheria za mikataba ili kuhakikisha kwamba mikataba yote inayiongiwa na Halmashauri ina tija kwa Serikali,wananchi na Halmashauri kwa ujumla.

 

8.3  Sheria Ndogondogo

Katika kipindi cha 2015 hadi 2016  Halmashauri kupitia Kitengo cha Sheria imeweza kuanda Sheria Ndogo 7 zitakazo saidia utekelezaji wa majukumu ya Halmashauri katika kuhudumia wananchi wa Wilaya ya Same. Sheria hizo ni Sheria Ndogo za Ushuru wa Mabasi Stendi, Sheria Ndogo ya Kudhibiti Unywaji Holela wa Vileo, Sheria Ndogo za Ushuru wa Pumba za Nafaka, Sheria Ndogo ya Kilimo cha Mazao yanayohimili Ukame, Sheria Ndogo ya Mahudhurio ya Lazima kwa Shule za Msingi na Sekondari, Sheria Ndogo za Ushuru wa Nyumba za Kulala Wageni na Sheria Ndogo ya Kuzuia Ujazaji wa Lumbesa. 

Katika kuhakikisha kwamba tunakuwa na jamii ya watu walio sawa na huru, Halmashauri ya Wilaya ya Same inashirikiana na Taasisi zisizo za kiserikali katika kutoa msaada wa kisheria kwa makundi mbalimbali ya kijamii katika wilaya ya Same.

IDARA YA MAENDELEO YA JAMII

.1      Mambo ya kufanya ili kuhakikisha Jamii inapata Maendeleo

Kinachofanyika na kinachotarajiwa kufanyika ili kuhakikisha jamii inapata maendeleo ni;

  1. Kuhamasisha jamii jamii  kushiriki katika kazi za maendeleo za     kujitegemea kama (misaragambo) ,katika      ujenzi  wa barabara, ofisi za     kata,zahanati, shule za msingi na sekondari,  uchangiaji wa madawati, na kujiunga     katika vikundi. 
  2. Kuhamasisha jamii kutumia teknolojia raisi katika     ujenzi wa nyumba bora na salama      zenye gharama nafuu, kwa kutumia      matofali fungamano. 
  3. Kuijengea jamii elimu ya ufahamu juu dhidi     ya   mila potofu kama vile, Ukeketaji,     ndoa za utotoni, kulazimisha kurithi wajane na zinginezo. 
  4. Kutoa elimu ya      ufahamu  kwa jamii  kuepuka maambukizi  mapya      ya VVU na UKIMWI, Kuacha      ngono zembe  matumizi     sahii  ya kondomu, dawa za ARV.
  5. Kuhamasisha jamii juu kupinga unyasasaji wa kijinsia,     kama vipigo, matusi, dharau na aina yoyote ya unyanyasaji.
  6. Kutoa elimu ya ufahamu kwa wazazi, walezi na     jamii kwa jumla kuwapa fursa sawa watoto wa jinsi katika kuwapa elimu na     kujiendeleza.
  7. Kutoa elimu     ya ufahamu kwa wazazi, walezi,  juu     ya kutumikishwa  kwa watoto,     kuwafanyisha kazi ngumu zilizozidi uwezo wao
  8. Kuhamasisha jamii kuwa na uelewa wa kupinga     matumizi mabaya ya madawa ya kulevya kama vile uvutaji bangi,na ulaji wa     mirungi.
  9. Kutoa elimu kwa jamii juu ya malezi bora kwa     vijana ili kuepusha ongezeko la makundi tete.
  10. Kushirkiana na watoan huduma za kiroho, lil kutoa     huduma kwa makundi ya rika zote katika kuepusha  kusitokee au kupunguza makosa ya jinai
  11. Kuhamasisha jamii ili kujiunga katika vikundi kwa     ajili ya kupatiwa mafunzo ya ujasiriamali.
  12. Kuhasisha jamii ili kujiunga na vikundi vidogo     vidogo vya kuweka na kukopa vijulikanavyo kama VICOBA.
  13. Kuhamasisha jamii ya makundi ya vijana na     wanawake kujiunga katika vikundi vya ujasiriamali kwa ajili ya kupatiwa     mikopo yenye mashariti nafuu.
  14. Kutoa elimu kwa jamii juu ya upimaji wa maeneo     yao kwa ajili ya matumizi bora yan ardhi na mipango miji, ili kuepusha     migogoro.
  15. Kuhamasisha wananchi juu Usafi wa mazingira,     ujenzi wa vyoo bora na matumizi yake ili kupusha magonjwa ya milipuka.

.2      Idadi ya Vikundi vyenye Nguvu

Idadi ya vikundi vilivyopata usajili na vyenye nguvu ya kuweza kupata mikopon katika taasisi za kifedha ni kama ilivyoanishwa hapa chini;

Jedwali 5.1 Idadi ya Vikundi vyenye Nguvu

                       
 

AINA  YA KIKUNDI

 
 

VIKUNDI  VYA VIJANA

 
 

VIKUDI  VYA WANAWAKE

 
 

VIKUNDI  VYA WAJASIRIAMALI

 
 

IDADI

 
 

387

 
 

678

 
 

475

 

 

 

  Chanzo: Idara ya Maendeleo ya Jamii

 

Jedwali 5.2: Idadi ya Vijana wasio na Kazi Maalum

                   
 

WANAWAKE

 
 

WANAUME

 
 

JUMA YA VIJANA  WASIOKUWA NAKAZI

 
 

246

 
 

223

 
 

469

 

Chanzo: Idara ya Maendeleo ya Jamii

 

 

 

.3      Mikakati ya Kuwaendeleza Vijana

v   Kuwahamasisha vijana   ili waweze kujiunga na masomo ya ufundi stadi kv   uashi useremala na ujenzi ili waweze kujiajiri

v   Kwahamasisha vijana kujiunga kwenye vikundi ili wapatiwe mkopo yenye mashariti nafuu

v   Kuwahamasisha vijana ili wajiunge kwenye makundi kwa ajili ya kupatiwa elimu juu ya ujasiriamali

v   Kuwatengea vijana maeneo maalum kwa ajili ya kufanyia biashara ndogo ndogo

v   Kuwahamasisha vijana kutumia elimu mbalimbali katika kuanzisha ufugaji wa kuku na  n g”ombe wa maziwa na nyama

v   Kuhamasiha vijana ili waweze kuanzisha viwanda vidovidogo kv, useremala uashi na ufndi vyuma.

5.       Idadi ya SACCOS/Vikoba

Idadi ya SACCOS na Vikoba ni kama ifuatavyo; 

Jedwali 5.3: Idadi ya SACCOS/Vikoba

                                                                                                           
 

S/N

 
 

JINA LA SACCOS

 
 

KATA/ENEO

 
 

MMILIKI

 
 

1 

 
 

SAME KAYA  SACCOS

 
 

WILAYA

 
 

WANANCHI/WANACHAMA

 
 

2

 
 

SAME TEACHERS  SACCOS

 
 

WILAYA

 
 

WAALIMU  WANACHAMA

 
 

3

 
 

KISIWANI  SACCOS

 
 

KISIWANI

 
 

WANACHAMA

 
 

4

 
 

MKONAPA SACCOS

 
 

VUMARI

 
 

WAFANYAKAZI/WANACHAMA

 
 

5

 
 

NASHENGENA  SACCOS

 
 

MAORE

 
 

WANACHAMA.

 
 

6

 
 

KURUGENZI  SACCOS

 
 

WILAYA

 
 

WAFANYAKAZI

 
 

7

 
 

MARANATHA  SACCOS

 
 

SAME

 
 

WAUMINI  WASABATO

 
 

8

 
 

GAHENDU

 
 

SAWENI

 
 

WANACHAMA WA  GAVAO, HEDARU, GUNDU.

 

Chanzo: Idara ya Maendeleo ya Jamii

 

o  Fedha za Vikundi toka Halmashauri katika bajeti ya 2015/2016 zilizopangwa, Kiasi cha Fedha kilichotolewa na Idadi ya Vikundi vilivyopewa

Fedha zilizopangwa kutolewa na Halimashauri kwa kipindi cha 2015/16 ni jumla ya TShs. 112,000,000/=  na zilizotolewa ni Tshs. 26,000,000/= na idadi ya vikundi vilivyopatiwa mikopo ni 14.

o  Fedha zilizopangwa katika Bajeti ya 2016/2017

Kwa upande wa Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2016/2017, Fedha zilipangwa kutolewa kwa kipindi cha 2016/17 ni Tsh. 146,000,000/=

6.      KITENGO CHA UKAGUZI WA NDANI

o  Idadi ya Hoja za Ukaguzi

Kwa kipindi kinachoishia mwezi Agosti, 2016, Halmashauri ilikuwa na hoja za ukaguzi 54 zinazohitaji majibu yatakayopelekea hoja hizo kufungwa.

o  Mikakati ya kupunguza Hoja za Ukaguzi

Uongozi wa halmashauri umeweka mikakati ili kupunguza hoja za ukaguzi, mikakati hiyo ni:-

                              I.            Kutumia mashine za elektroniki zinazowasiliana na makao makuu ya halmashauri kukusanyia mapato toka katika Kata, itasaidia kuhakikisha mapato yote yaliyokusanywa kufahamika na kuwasilishwa na kuondoa tatizo la upotevu/kutokuwasilishwa  wa vitabu vya kukusanyia mapato

                            II.            Kuendelea kuwasiliana na TAMISEMI , ili kuweza kupata wakuu wa Idara/au kuwathibitisha makaimu wakuu wa idara waliopo, hii itasaidia kupunguza madeni kwa wakuu wa idara wanaokaimu kwa muda mrefu

                        III.            Kuendelea kufuatilia uwepo wa watumishi hewa  kwa kufanya uhakiki wa watumishi kila mwezi

                        IV.            Kuongeza juhudi katika ukusanyaji wa mapato ya ndani na kuibua vyanzo vipya vya mapato ya ndani , na kuendelea kuwasiliana na Hazina /Serikali kuu ili iweze kuleta fedha kwa wakati kulingana na bajeti , hii itasaidia halmashauri kutekeleza kazi kulingana na bajeti na kuwa na uwezo wa kupeleka asilimia 10 ya mapato ya ndani yaliyokusanywa katika mfuko wa wanawake na vijana

                            V.            Kuendelea kufuatilia fedha za miradi  ya maendeleo ambazo hazijawasilishwa toka Hazina na kuomba fedha hizo kuwasilishwa kwa wakati

                        VI.            Kutenganisha thamani ya majengo na ardhi kwa kufanya uthaminishaji

                      VII.            Kuwaelekeza wakuu wa Idara/vitengo/watumishi kutekeleza majukumu kwa kufuata taratibu na sheria

                  VIII.            Kuimarisha mifumo ya udhibiti wa ndani katika usimamizi wa fedha/manunuzi/ubora

                        IX.            Kuhakikisha utekelezaji wa miradi unafanyika mapema mara fedha zinapowasili

                            X.            Kuimarisha Kitengo cha ukaguzi wa ndani kwa kuwajengea uwezo katika mifumo, mfano, mfumo wa ukusanyaji wa mapato kielektronic, LAWSON, EPICOR, PLAN REP.

o  Changamoto zinazosababisha kutokuisha kwa Hoja za Ukaguzi

                              I.            Upungufu wa mkaguzi mmoja kulingana na Ikama

                            II.            Kukosekana/kutokuwasilishwa kwa fedha , kumepelekea kaguzi kutofanyika kulingana na mpango wa ukaguzi wa mwaka 

                        XI.            Wakaguzi kutokujengewa uwezo kuhusiana na mifumo ya ukusanyaji wa mapato kielektronic, LAWSON, EPICOR, PLAN REP

7.      IDARA YA UJENZI

o  Idadi ya Miradi inayoendelea kutekelezwa

Katika mwaka wa fedha 2015/2016 idara ya ujenzi ilitengewa  kiasi cha Tshs 956,160, 000/= kutoka mfuko wa barabara (Road fund) hadi kufikia 30/06/2016 halmashauri imepokea kiasi cha Tsh 215,460, 000/= tu. Miradi inayoendelea kutekelezwa kwa kazi za barabara ni kama ifuatavyo:-

Jedwali 11.1: Idadi ya Miradi inayoendelea kutekelezwa

                                                                                                                             
 

Na.

 
 

Jina la mradi

 
 

Jina la Mkandarasi

 
 

Gharama ya Mkataba

 
 

Maoni

 
 

1

 
 

Matengenezo ya kawaida na  muda maalumu barabara za Makanya – Chankoko na Njia panda – Chankoko -  Mvungwe

 
 

 OLDONYOMAS ENGINEERING

 
 

 

 

105,577,550

 
 

 

 

 

 

Kazi zinaendelea

 
 

2.

 
 

Matengenezo ya kawaida  muda maalumu na miundo mbinu ya maji barabara za Mpirani -Kadando,Maore-  Vuje,Ndungu-Makokane na Mpirani-Bombo 

 
 

 

 

CORNEL (T) LTD

 
 

 

 

88,030,950

 
 

 

 

 

 

Kazi zinaendelea

 
 

3.

 
 

Matengenezo ya kawaida, sehemu  korofi na matengenezo ya muda maalumu barabara za Same -Ruvu-Mferejini na  Ishinde-Vumari.

 
 

CORNEL (T) LTD

 
 

 

 

77,881,180

 
 

 

 

Kazi zinaendelea

 
 

4.

 
 

Matengenezo ya  kawaida,sehemu korofi  na miundombinu  ya maji ya mvua barabara za Kisiwani -Msindo,Mwembe- Mhezi,Mbuyuni-Marindi  na   Ijinyu - Kamadufa 

 
 

 

 

MUGENZO CO. LTD

 
 

 

 

64,431,540

 
 

 

 

 

 

Kazi zinaendelea

 
 

5.

 
 

Matengenezo ya kawaida na  sehemu korofi barabara za  Saweni-Gavao  -Bwambo,Kidenge- Mwala na  Hedaru-  Makasa-Kirangare 

 
 

 

 

HAMORIC INVESTMENT (T) LTD

 
 

 

 

34,499,660

 
 

Kazi zinaendelea

 
 

6

 
 

Matengenezo ya kawaida na  miundombinu ya maji barabara za Majevu-Dido- Njoro, Minyala -Mbono-Mgagao na  dengude- Dido.

 
 

KIV CO.LTD

 
 

70,825,960

 
 

Kazi zinaendelea

 
 

7

 
 

Matengenezo ya kawaida  muda maalumu na miundo mbinu ya maji barabara za Same Mjini.

 
 

SIMJO TECH CO.LTD

 
 

128,118,500

 
 

Kazi zinaendelea

 
 

8

 
 

Matengenezo ya kawaida na  sehemu korofi barabara za  Bangalala  -Chome na Chome - Ikokoa 

 
 

MSHUNGA INVESTMENT LTD

 
 

22,774,000

 
 

Kazi zinaendelea

 

Chanzo: Idara ya Ujenzi

 

11.2 Ubora wa Miradi inayotekelezwa.

Miradi inayotekelezwa ipo katika ubora unaotakiwa kwa kuzingatia taratibu za mikataba.

11.3 Uhakiki kwa Wakandarasi wanaopatiwa Kazi/Tenda

Uhakiki wa wakandarasi wanaopatiwa kazi/tenda hufanyika kipindi cha kufanyiwa uchambuzi wa zabuni (Tender evaluation) wa wazabuni wanapoomba tenda/zabuni.

11.4 Ubora na Muda wa Ukamilishaji wa Miradi

Ubora wa kazi unazingatiwa na Mkandarasi kam hajakamilisha kazi kwa wakati anapata adhabu ya kuchelewesha kazi (liquidated damages)

11.5 Idadi ya Miradi ambayo haikukamilika kwa Wakati na sababu zilizopelekea 

Miradi yote haijakamilika kwa wakati kutokana na kuchelewa kupokea fedha kutoka serikali kuu. (Mfuko wa barabara)

11.6 Hali na urefu wa Mtandao wa Barabara

Hadi kufikia mwezi Juni mwaka 2016 Halmashauri ya wilaya ya Same ina mtandao wa Barabara wenye Jumla ya 668.63 Km zinazofanyiwa matengenezo kwa usimamizi wa Halmashauri kupitia kitengo cha barabara. Kati ya barabara hizo 0.8Km ni za lami ambazo zipo Same mjini,128 Km ni za changarawe na 539.83 Km ni za udongo.Asilimia 85 ya barabara ziko milimani na asilimia 15 ni za tambarare.


8.      IDARA YA FEDHA

12.1 Utangulizi

Halmashauri ya Wilaya ya Same kwa mwaka wa fedha 2015/2016 iliidhinishiwa  kupokea fedha  Tshs. 43,351,398,248  hadi kufikia Juni 2016 ilikuwa imepokea Tshs. 41,467,376,632  sawa na asilimia 95.

Jedwali hapo chini linaonyesha vyanzo vya Halmashauri, Makadirio, hali halisi, asilimia, utekelezaji na changamoto zilizojitokeza wakati wa utekelezaji wa bajeti hiyo kama ifuatavyo:-

Jedwali 12.I: Bajeti ya Halmashauri 2015/2016

                                                                                                                             
 

Na.

 
 

Vyanzo vya Halmashauri

 
 

Makadirio

 
 

Hali halisi ya makusanyo  ya Fedha

 
 

Asilimia

 
 

Utekelezaji

 
 

Changamoto

 
 

1.

 
 

Vyanzo vya  ndani

 
 

2,274,732,000

 
 

1,933,320,538

 
 

85

 
 

Fedha za  mapato  ya ndani zimechangia miradi ya  maendeleo;-

 

Mchango wa madawati  Tshs. 212,021,051

 

Kuchangia  ukamilishaji wa ujenzi wa maabara na ununuzi wa vifaa vya maabara Tshs.  37,810,000

 

Kuwezesha  unununzi wa kipaza sauti ukumbi wa Halmashauri Tshs.

 

4,613,400

 

Ukamilishaji  wa kituo cha kilimo Tshs. 5,600,000

 

Kuchangia  ujenzi wa ofisi mpya ya Mkurugenzi Tshs. 30,000,000

 

Kuchangia  ukarabati wa shule za msingi  Tshs.  10,000,000

 

Kufunga mfumo  wa kieletronic Tshs. 75,417,808

 

Kuchangia  mfuko wanawake na Vijana Tshs. 22,150,360 na

 

Uendeshaji wa  shughuli za ofisi vikao na ulipaji wa mishahara kwa watumish wanaolipwa na  mapato ya ndani.

 
 

-Mwamko mdogo  wa wananchi kulipa kodi na ushuru.

 

-Baadhi ya  Vijiji kutokuwa na Maafisa watendaji Vijiji.

 

-Shughuli za  uchaguzi Mkuu

 

-Mabasi  kutoingia stand.

 
 

2.

 
 

Fidia ya  vyanzo vilivyofutwa

 
 

          200,023,000

 
 

     31,977,000

 
 

 

 

16

 
 

Shughuli za  uendeshaji wa ofisi zilifanyika kulingana na fedha iliyotolewa.

 
 

Fedha kuto  kutolewa kulingana na Bajeti.

 
 

3.

 
 

Serikali kuu -  Ruzuku – OC

 
 

  2,327,258,000

 
 

1,769,377,000

 
 

76

 
 

Idara  ilitekeleza shughuli zilizopangwa kutokana na fedha zilizopokelewa 

 
 

Fedha  kutopokelewa kwa wakati.

 

Fedha kuto  kutolewa kulingana na Bajeti.

 
 

4.

 
 

Mishahara

 
 

32,612,236,000

 
 

31,899,123,217

 
 

98

 
 

Mishahara  ililipwa kwa Watumishi kwa wakati

 
 

Madeni ya  Malimbikizo  ya mapunjo ya mishahara.

 
 

5.

 
 

Miradi ya maendeleo.

 
  • Serikali   Kuu
  • Wafadhili
 

-            EGPAF

 

-            EASTERN ARC

 

-            MIVAF

 

-            TANAPA

 

-            Performance For Result (P4R)

 

-            Ujenzi / Uboreshaji Miundombinu- Kibacha

 

-            TASAF

 
 

 

 

 

 

   3,177,944,465

 

   

 

239,474,300

 

  

 

 15,400,000 21,300,000

 

  

 

18,000,000

 

     72,377,209

 

   

 

221,902,836

 

   

 

 

 

 

 

 

 

 

 

2,170,750,438

 

 

 
 

 

 

 

 

     3,147,136,623

 

     

 

166,711,771

 

     

 

15,400,000

 

21,300,000

 

  

 

18,000,000

 

   72,377,209     

 

     

 

     221,902,836

 

  

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 2,170,750,438

 
 

 

 

 

 

99

 

 

 

70

 

 

 

100

 

100

 

 

 

100

 

100

 

 

 

100

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

100

 
 

Utekelezaji wa miradi umefanyika  kulingana na fedha iliyotolewa na lengo lililokusudiwa

 
 

Kuchelewa kupokea fedha kwa wakati.

 
 

 

 
 

Jumla                          

 
 

43,351,398,248      

 
 

41,467,376,632       

 
 

95

 
 

 

 
 

 

 

                       

 

 

 

Jedwali 12.2: Bajeti ya Halmashauri 2016/2017

                                                                     
 

Vyanvo

 
 

Makadirio

 
 

Mikakati ya kufikia malengo

 
 

Vyanzo vya  ndani

 
 

                  

 

    2,335,264,000

 
 

-            Kuhakikisha Takwimu na Bajeti za Mapato zinaandaliwa kutoka kwenye  kila Kijiji pia itawezesha Kijiji kuwa na makadirio ya asilimia 20  itakayorejeshwa Kijijini.

 

-            Kuhakikisha kila Kijiji kinakuwa na malengo ya kukusanya mapato

 

-            Kuhakikisha kila Kata inakuwa na machine ya kukusanyia mapato.

 

-            Kuhakikisha kuna kuwa na ufatiliaji wa mara kwa mara  wa mapato na ufatiliaji wa kushtukiza

 

-            Kubuni vyanzo vipya vya mapato

 

-            Kuendelea kutoa  elimu  kwa walipa kodi na ushuru ili waweze  kuelewa umuhimu wa kulipa kodi na ushuru.

 

-            Kuendelea kufatilia mikakati iliyowekwa na kufanya tathmini..

 
 

Fidia ya  vyanzo vilivyofutwa

 
 

 

 

        192,362,000

 
 

-             

 
 

Serikali kuu -  Ruzuku – OC

 
 

       

 

     3,245,916,850

 
 

-             

 
 

Mishahara

 
 

 

 

   39,475,823,940

 
 

-             

 
 

Miradi ya  maendeleo

 

 

 
 

 

 

   11,251,205,280

 
 

-             

 
 

JUMLA

 
 

   56,500,572,071

 
 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 


12.2 Halmashauri inakusanya mapato Kwa njia ya kieletroniki Na kupitia mfumo WA LGRCIS ambao umeunganishwa na NMB 

Halmashauri ilianza kutumia mashine ya kukusanyia mapato ngazi ya Kata, mwezi Julai 2016.  Tumeshanunua mashine 35 kwa sasa  Kata zinazotumia  mashine  ni Kata 17  nazo ni Mamlaka ya Mji mdogo kata 3, Hedaru, Makanya, Njoro, Bendera, Kihurio, Ndungu, Maore, Kisiwani,   Ruvu ,Vumari, Kalemawe, Bwambo, Myamba na Mpinji  Sambamba na ilo tumeshanunua Mashine zingine 30 za kukusanyia mpato.

12.3 Vyanzo Vipya Vya Mapato

·        Halmashauri imeanza mpango wa kuanzisha soko la mazao katika Kata ya  Ruvu ambalo litawezesha  Halmashauri kukusanya  ushuru wa mazao, tayari timu ya Wilaya imeshakutana na serikali ya Kijiji kwa ajili ya kuwashirikisha  kupata eneo sahihi.

·        Halmashauri imeanza  mpango wa kuanzisha  mnada wa mifugo Kata ya Njoro  siku ya Alhamisi  na Same  siku ya Jumapili.

12.4 Kudhibiti Wizi /Upotevu

Halmashauri imeweka utaratibu wa kuwasilisha mapato mara mbili kwa Mwezi na ukaguzi wa nyaraka za fedha unafanyika kila baada ya miezi mitatu kwa kushirikisha Kitengo cha Ukaguzi wa ndani.

12.5 Ufanisi wa Malipo

Halmashauri inafanya malipo yote  kupitia mfumo wa malipo wa EPICOR, mfumo huu unategemea uwepo wa fedha kwenye  kasma na kifungu  husika, hivyo kasma  na kifungu vinapokuwa na fedha malipo huchukua siku 3 mhusika kulipwa. Iwapo madai yanafika ofisini pasipo kuwa na fedha mhusika hufahamishwa kwa barua kusubiri mpaka hapo itakapopatikana.


9.      IDARA YA MIPANGO, TAKWIMU NA UFUATILIAJI

o  Mipango kiidara

Mipango kiidara ipo, na idara hii ndiyo yenye jukumu la kuunganisha Mipango na shughuli za Idara mbalimbali kupitia mfumo ujulikanao kama Medium Term Expenditure Framework (MTEF). Miradi yote ya kila Idara ngazi ya Kata na Vijiji pamoja na miradi ngazi ya Wilaya huunganishwa na kuratibiwa na Idara hii, ili kuleta ufanisi wa utoaji huduma kwa jamii.

o  Mpango Mkakati/ Strategic Plan

Idara ya Mipango Takwimu na Ufuatiliaji pia ina jukumu la Kuratibu na kusimamia uandaaji wa Mpango Mkakati wa miaka mitano wa     Halmashauri (Strategic Plan). Zoezi hili hufanyika kila baada ya Miaka mitano katika Halmashauri, ambapo Idara inaanda Mpango Mkakati mpya au kuhuisha Mpango Mkakati uliopo. Hadi sasa Idara bado ipo kwenye mchakato wa kuhuisha Mpango Mkakati  wa Halmashauri ambapo mda sio mrefu zoezi hili litakamilika.

o  Hali ya Pato la Mwananchi kwa sasa (GDP)

Pato la Mwananchi (GDP) ni jambo muhimu sana la kuzingatia ili kupima halihalisi ya uchumi kwa kila Mwananchi katika Jamii. Hali ya Pato la Mwananchi katika Halmashauri ya Wilaya ya Same ni Shilingi 720,000/=

o  Uwepo wa Takwimu zinazosaidia Idara kupanga na kufanya Maamuzi

Katika Halmashauri ya Wilaya, Takwimu zote za Kiuchumi na Kijamii zipo na zinatumika ipasavyo katika utekelezaji shughululi mbalimbali za maendeleo. Takwimu kama vile Idadi ya Watu ndizo tunazozitumia sana katika utekelezaji wa shughuli za Miradi ya maendeleo. Takwimu zingine ni za sekta mbalimbali kama vile Takwimu za Elimu, Afya, Kilimo, Mifugo na zingine mbalimbali.

o  Usambazaji wa Takwimu sahihi kwa Matumizi

Hali ya usambazaji wa Takwimu katika Halmashauri ya Wilaya ya Same ni ya kuridhisha, kwani Takwimu hizi zinasambazwa pale zinapohitajika na kwa wakati.

o  Ufuatiliaji wa Utekelezaji wa Kazi za Miradi

Idara hii pia ina jukumu la kufanya ufuatiliaji kwa kina juu ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali za Miradi ya Maendeleo pamoja Kuratibu, kusimamia, kutathmini na kufanya uhakiki wa programu za maendeleo ya Halmashauri. Ufuatliaji wa utekelezaji wa shughuli za Miradi inayotekelezwa Vijijini sio ya kuridhisha sana ukilinganisha na miaka iliyopita. Hali ya ufuatiliaji wa Miradi inaathiriwa na uhaba wa Fedha hasa baada ya Kifungu cha Monitoring and Evaluation katika Bajeti ya Ruzuku ya Miradi ya Maendeleo (LGCDG) kufutwa. Idara imekuwa ikipata changamoto sana juu ya ufuatiliaji wa Miradi ya Maendeleo katika Halmashauri. Idara imejitahidi na inaendelea kujitahidi sana kufuatilia miradi ya maendeleo katika Halmashauri kwa kuomba Fedha kutoka kwenye Mfuko Mkuu (GF). Pia ili kuendelea kusimamia ufanisi wa miradi inayotekelezwa, Idara inawatumia Watendaji wa Kata na Vijiji kwa kufanya mawasiliano ya karibu sana kipindi miradi inatekelezwa jambo ambalo linasaidia pia katika ufanisi wa Miradi ya Maendeleo.

o  Mfumo wa kuhakikisha Utekelezaji wa Shughuli za Miradi na  Idara

Pamoja na majukumu mengine Idara hii inatumia Mfumo wa kuhakikisha Utekelezaji wa Shughuli za Miradi ndani ya Idara na nje ya Idara. Maelekezo na miongozo hutolewa kutoka kwenye Ofisi ya Mkurugenzi na kuletwa ndani ya Idara. Idara hii inasimamia Mipango yote ya shughuli mbalimbali ndani na nje ya Idara. Idara zote huandaa Mipango yao na kazi kubwa ya Idara hii ni Kuratibu na kusimamia mchakato wa Mipango shirikishi na uandaaji wa bajeti ya Halmashauri. Mipango hii ya Halmashauri kiidara huunganishwa katika mfumo mmoja ujulikanao kama Medium Term Expenditure Framework (MTEF). Pia Idara hii inafanya kazi za Kuratibu mchakato wa menejiment ya Takwimu mbalimbali za Halmashauri na kupendekeza sera na mipango inayohitajika. Kazi nyingine ya Idara hii ni Kufanya makisio ya idadi ya watu ya Wilaya (Population Projection) kwa kila mwaka ambapo zoezi hili ni muhimu sana kwani husaidia katika swala zima la uandaaji wa Maoteo [Indicative Planning Figure (IPF)] wakati wa kipindi cha mchakato wa uandaaji wa Mpango na Bajeti. Yote hii ni kuhakikisha kunakuwa na usawa katika ugawaji wa huduma za kiuchumi na kijamii pamoja na Maendeleo kwa ujumla.

o  Dira, Dhima, Desturi na Namna ya Kuzimiliki

Halmashauri ya Wilaya ina Dira, Dhima na Desturi kama ifuatavyo;

Dira: Kuwa na Jamii yenye Maisha bora, iliyohamasika na kuendana na mabadiliko endelevu ya Maendeleo ya Kiuchumi na Kijamii ifikapo mwaka 2016.

Dhima: Kutoa Huduma bora kwa Jamii kupitia matumizi sahihi ya Rasilimali, kuwajengea uwezo, Utawala bora na kuwa na Maisha bora.

Desturi: Kutoa huduma kwa Jamii kwa kutumia mbinu shirikishi (Participatory Approach) ili kuleta ufanisi wa huduma ya utawala bora na Huduma kwa Jamii. Idara ina uhuru wa kumiliki desturi yake ya kutoa huduma katiaka jamii kwa kushirikisha Idara zote na Vitengo katiaka Halmashauri pamoja na ngazi za Kata na Vijiji. Idara inaendelea kufanya shughuli zake kwa kufuata desturi yake ya ushirikishwaji wa jamii.

10.   KITENGO CHA MANUNUZI

o  Ufanisi wa Idara

Kitengo cha manunuzi ni miongoni mwa kitengo (6) vilicho chini ya Mkurugenzi Mtendaji, aidha   Majukumu ya kitengo cha manunuzi ni kama ifuatavyo;-

Ø   Kusimamia shughuli zote za manunuzi

Ø   Kutekeleza maagizo ya Bodi ya zabuni

Ø   Sekretarieti ya bodi ya zabuni

Ø   Kupanga manunuzi na mpango wa kuuza mali za serikali

Ø   Kupendekeza manunuzi njia ya manunuzi na kuuza mali za serikali kwa njia ya zabuni

Ø   Kuandaa mahitaji mahitaji taarifa ya mahitaji

Ø   Kuandaa kabrasha za  Zabuni

Ø   Kuandaa matangazo ya Zabuni

Ø   Kuandaa Mikataba ya Zabuni

Ø   Kutoa Mikataba iliyo idhinishwa

o  Idadi ya Kazi zilizotangazwa, zilizoleta Migogoro na zenye Kesi

Kwa kipindi cha Mwaka 2015/2016 zabuni zilizo tangazwa ni kama ifuatavyo;

1.      Ujenzi wa barabara  zabuni zilizo tangazwa ni 9

2.      Ujenzi wa majengo zabuni zilizotangazwa ni 7

Idadi ya wa tumishi katika kitengo ni 4

Upungufu uliopo ni 1

Kwa upande wa Kazi zilizotangazwa hakuna kazi zozote zenye migogoro na Kesi katika Halmashauri yetu.

 

14.3 Changamoto

Ø   Sheria ya Ununuzi Umma Kurefusha mchakato wa Manunuzi  kwa serikaliza Mitaa

Ø   Upungufu wa Mtumishi (1) katika kitengo cha Manunuzi

Ø   Uelewa Mdogo wa sheria kwa  baadhi ya Idara  tumizi (User departiments)

14.4 Mikakati

Ø   Kushauri wakuu wa Idara na vitengo Kuanzisha michakato ya manunuzi kwa wakati

Ø   Tayari Kitengo kilisha omba kibali cha kupatiwa Mtumishi mmoja. 

Ø   Tayari kitengo cha Manunuzi kimefanya mafunzo kwa wakuuu wa idara na vitengo na kinaendelea

11.   KITENGO CHA TEHAMA

15.1Hali ya Matumizi ya Tehama katika Idara na Vitengo mbalimbali Ndani ya Halmashauri

Kitengo cha TEHAMA ni miongoni mwa vitengo (6) vilivyopo chini ya Mkurugenzi Mtendaji, aidha   matumizi ya TEHAMA kwa kila Idara ni kwa asilimia 100,kwa maana ya kwamba kila Idara na Kitengo ili ufanisi ni Mzuri kwa sababu shughuli zao za kila siku inategemea TEHAMA.

Sambamba na ilo kuna baadhi ya Idara hawawezi kabisa kuendesha shughuli zao za kila siku kama Miundo mbinu ya TEHAMA haipo,mfano Idara ya Utumishi na Utawala,kwaajili ya mfumo wa taarifa za kiutumishi yaani LAWSON,Idara ya Fedha kwaajili ya Mfumo wa Malipo na Matumizi ya Fedha za Serikali yaani EPICOR 9.05, LGRCIS kwaajili ya ukusanyaji wa Mapato.TASAF kwaajili ya uhakiki wa  taarifa sahihi ya kaya maskini yaani PSSN,TOMSHA kwaajili ya taarifa sahihi ya WAVIU na Idara ya Mipango na Takwimu kwamaan ya Mfumo wa uandaaji Bajeti ya Halmashauri yaani PLANREP.

 

15.2Mipango ya Kukuza Tehama

Kama ilivyo kwa Vitengo vingine ifuatayo ni mipango kabambe ya kukuza kitengo cha TEHAMA ndani ya Wilaya:-

v   Kuwa na Tovuti iliyo huishwa (Hosting) ambayo itakuwa inatoa taarifa za Wilaya kwa wakati na ueledi.Touvti iyo ni www.samedc.go.tz kwa sasa tovuti iyo ipo hewani na inatoa taarifa za Wilaya kwa wakati.

v   Kusimamia taasisi zote za Serikali zilizopo ndani ya Wilaya kuwa na matumizi sahihi na bora ya TEHAMA.mfano huduma ya mtandao (internet).

v   Kutumia baadhi ya miundo mbinu ya TEHAMA kwaajili ya kutumika kama vyanzo vya mapato ndani ya Halmashauri mfano Internet Café,

v   Kufuatilia,kusimamia na kujua gharama za uendeshaji na uanzishwaji wa Gazeti au makala ya Wilaya kiujuma.

v   Kufuatilia,kusimamia na kujua gharama za uendeshaji na uanzishwaji wa Redio ya Wilaya

15.3Mipango ya uimarishaji wa Mawasiliano kati ya Halmashauri na Wananchi ndani ya Halmashauri.

Ifuatayo ni Mipango ya uhimarisha wa mawasiliano kati jamii na halmashauri:-

  • Kuwajengea uelewa wa Matumizi ya sahihi ya     mawasiliano mbalimbali mfano simu na      huduma ya internet.
  • Kuhakikisha kila kata katika Wilaya ya Same inakuwa     na Huduma ya Mawasiliano ya Simu, mfano Vodacom,Tigo ,Airtel na Halotel.Kata     ya Vumari ndio pekee ilikuwa imebakia lakini kwa sasa kampuni ya Vietnam     (Halotel) wameshafikisha huduma iyo.
  • Kujaribu kuanisha maeneo mbalimbali ya uwekezaji wa     miundo mbinu mbali mbali ya mawasiliano.

15.4          Mipango ya Kuitangaza Wilaya kwa Wananchi wa Same, Nje ya Same na Nje ya Nchi

i)                    Kuanzisha gazeti/jarida ambalo litaeleza shughuli mbalimbali zinazofanywa na halmashauri ya wilaya ya Same.Gazeti hilo tayari lipo kwenye mchakato nimewasilisha maelezo husika kwa Mkurugenzi Mtendaji.

ii)                  Kuanzisha redio ya halmashauri ya Wilaya ya Same.Kuanzisha redio kunahitaji vitu vifuatavyo;

·        Ofisi/sehemu maalum kwa ajili ya studio

·        Kuandika barua ya maombi kwaTCRA ili tupate kibali maalum cha kuanzisha redio na kurusha matangazo. 

·        Vifaa vya studio ikiwemo mitambo ya kisasa (digital machines) ya kurushia matangazo.  

·        Mzabuni kwa ajili ya kutengeneza studio kwa shughuli za redio

iii)                Kuendelea kujenga mahusiano mazuri na vyombo vya habari ili kuleta urahisi wa kupenyeza taarifa chanya za Halmashauri ya Wilaya. Mfano mpaka sasa tuna mahusiano mazuri na vyombo mbalimbali ambavyo taarifa zetu zinatoka mara kwa mara vyombo kama gazeti la majira na TBC.

iv)                Kuanza kutumia Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya kuweka taarifa mbalimbali pamoja na matangazo mbalimbali ya tender na maonyesho yenye tija kwa Wilaya nzima.

v)                  Kuboresha page ya facebook ya Halmashauri ya Wilaya pamoja na Blog 

vi)                Kuunda group la whatup kwa baadhi ya watumishi watakaoweza kuunganishwa kulingana na uwezo wa simu zao ili wapate taarifa kwa wakati zaidi.

15.5          Kuboresha Mifumo ya ufuatiliaji kwa kutumia Tehama

Kama ilivyo katika Halmashauri nyingine,Halmashauri ya Wilaya ya Same inayo mifumo ambayo inayotumia katika kutekeleza majuku ya kila siku,mifumo ni EPICOR-FEDHA, LAWSON- UTUMISHI, PSSN-TASAF,TOMSHA-TACAIDS, BEMIS-ELIMU MSINGI/SEKONDARI, LGRCIS- UKUSANYAJI WA MAPATO na LMS- ARDHI.

Mifumo yote iyo kimsingi imeboreshwa na ufuatiliaji wake upo vizuri kwani kila wakati imekuwa ikitumika bila ya Tatizo lolote,kwa kushirikiana na TAMISEMI.Pamoja na ayo yote changamoto kubwa iliyopo ndani ya Kitengo cha TEHAMA ni ufinyu wa Bajeti hivyo baadhi ya shughuli zimekuwa ngumu kutekelezeka kabisa.

 

16.   IDARA YA MIFUGO NA UVUVI

16.1Idadi Ya Mifugo

Wilaya ya same ina kanda tatu za ufugaji wa mifugo ambazo ni ukanda wa juu (Milimani), ukanda wa kati na ukanda wa tambarare (Magharibi na Mashariki). Ukanda wa milimani mifugo hufugwa na kulishwa ndani (zero grazing and tethering) kanda zinazobaki yaani ukanda wa kati na tambarare mifugo hufugwa huria (free range) kwa mifugo asili na kufugwa/kulishwa ndani (zero grazing and tethering) kwa mifugo chotara. 

Eneo kubwa la malisho kwa ukanda wa tambarare ya Mashariki limepakana na Mbuga ya Taifa ya Mkomazi na ukanda wa tambarare ya Magharibi malisho haya yamepakana na mto Pangani. Wilaya ya Same ina mifugo mingi kuliko wilaya zote za mkoa wa Kilimanjaro. Eneo la malisho (Range land) lililoainishwa lina ukubwa wa hekta 356,200 ambazo ni asilimia 67.25 ya eneo lote la wilaya. Idadi ya mifugo wilayani ni kama inavyoonekana katika jedwali hapa chini; 

 

 

 

 

 

 

Jedwali 16.1: Aina na Idadi ya Mifugo inayofugwa Wilayani

                                                                                                                 
 

AINA YA MIFUGO

 
 

IDADI YA MIFUGO

 
 

JULMA YA MIFUGO

 
 

ASILI

 
 

CHOTARA

 
 

Ng’ombe  

 
 

176,484

 
             
   

 7,896 

   
 


 
 

184,380

 
 

Mbuzi  

 
 

112,427

 
             
   

 478 

   
 


 
 

112,905

 
 

Kuku  

 
 

210,839

 
             
   

 20,921 

   
 


 
 

231,760

 
 

Kondoo  

 
 

70,903

 
 

70,903

 
 

Punda  

 
 

6,426

 
 

6,426

 
 

Nguruwe  

 
 

2,811

 
 

2,811

 
 

Ngamia 

 
 

18

 
 

18

 
 

Bata 

 
 

9,990

 
 

9,990

 
 

 Mbwa 

 
 

8,796

 
 

8,796

 

Chanzo: Idara ya Mifugo na Uvuvi 

16.2Aina ya Ufugaji na Mikakati ya Kufuga Kisasa

Katika halmashauri ya wilaya ya Same, kuna aina kuu tatu za ufugaji. Aina hizo ni; 

i). Ufugaji huria ambao unatumika kufuga Ng’ombe, Mbuzi, Kondoo, Punda, Mbwa, Bata, Kuku na Ngamia 

ii). Ufugaji nusu huria ambao unatumika kufuga Kuku na Bata 

iii). Ufugaji wa ndani na/ au kufunga ambao unatumika kufuga Ng’ombe na Mbuzi chotara wa maziwa, Kondoo, Kuku, Bata na Mbwa.

Aidha kuna mikakati mbalimbali ambayo imewekwa ili kuhakikisha kuwa ufugaji bora na wakisasa unatekelezwa na wafugaji kama ifuatavyo; 

i). Kushirikiana na idara ya ardhi ili kuhakikisha mipango ya matumizi bora ya ardhi inatekelezwa ili kuepusha migogoro kati ya wafugaji na wadau wengine wanaotumia ardhi. 

ii). Kuwaelimisha wafugaji juu ya kanuni za ufugaji bora na faida zake ikiwemo aina bora na sahihi ya ufugaji pamoja na uvunaji wa mifugo ili kuendana na eneo la nyanda za malisho lililopo. 

iii). Kuboresha koo safu za mifugo kwa lengo la kuongeza uzalishaji wa mazao yatokanayo na mifugo kwa kutumia uhimilishaji na madume yaliyoboreshwa, mitetea pamoja na majogoo bora na kupunguza idadi ya mifugo na kuwa na mifugo michache yenye tija. Hili linafanyika katika ngazi ya mtu mmojammoja, kaya na vikundi. 

16.3Mipango ya kuboresha Bidhaa za Mifugo

i). Kushirikiana na sekta binafsi zinazofanya kazi za kuendeleza sekta ya mifugo na uvuvi ikiweo ujenzi wa machinjio za kisasa, masoko ya bidhaa za mifugo na viwanda vidogo vya kusindika mazao yatokanayo na mifugo. 

ii). Kuboresha koo safu za mifugo kwa lengo la kuongeza uzalishaji wa mazao yatokanayo na mifugo kwa kutumia uhimilishaji na madume yaliyoboreshwa, mitetea pamoja na majogoo bora na kutoa elimu ya ufugaji bora ili kuongeza kipato ngazi ya kaya na Taifa kwa ujumla. 

iii). Kudhibiti magonjwa ya mlipuko kwa kufanya chanjo, tiba za mifugo, uogeshaji wa mifugo pamoja na usimamizi wa minada ili kuongeza ubora na thamani ya mazao yatokanayo na mifugo. 

iv). Kutoa huduma bora ya ukaguzi wa nyama kwa lengo la kulinda afya ya jamii na kuzuia magonjwa ya kuambukiza (Zoonoses). 

v). Kusajili vituo vya huduma za mifugo ili kusogeza huduma za mifugo karibu na wafugaji na kusimamia utoaji wa huduma bora za mifugo zinazotolewa na wadau wa sekta binafsi. 

vi). Kutoa elimu juu ya ufugaji bora wa samaki kwenye mabwawa ya jamii na binafsi na kuzuia uvuvi haramu ili kuongeza kiwango bora cha uzalishaji wa samaki. 

 

 

17.   KITENGO CHA NYUKI

17.1Idadi ya Mizinga

Mizinga ya asili =    30,000

Mizinga ya kisasa =   2200

17.2 Uzalishaji Na Mazao Ya Nyuki Kwa Mwaka Na Kwa Aina Ya (Nyuki Wanaouma Na Wasiouma)

  1. Nyuki     Wanaouma:-

a)      Asali – Wastani wa Kilo 27,576 kwa mwaka.

b)      Nta  -  Wastani wa Kilo   2,519 kwa mwaka

 

  1. Nyuki     Wasiouma – Wastani wa Kilo 300 za Asali kwa mwaka. (Ufugaji wa nyuki hawa     unafanyika maeneo ya milimani).

 

  17.3 Mikakati Ya Kukuza Uzalishaji Wa Mazao Ya Nyuki 

  1. Kuboresha     ufugaji nyuki kwa kutumia mizinga ya kisasa ya masanduku pamoja na zana za     kisasa za ufugaji nyuki.
  2. Kuhamasisha     wananchi (wafugaji nyuki) kuanzisha kilimo cha mazao yanayotoa kwa wingi     chakula cha nyuki.
  3.  Kuwafundisha wafugaji nyuki kuhusu     tekinolojia mwafaka ya ufugaji nyuki, mfano kutumia nyumba/ mabanda ya     nyuki (Bee Houses).
  4. Kuimarisha     vikundi vya ufugaji nyuki vilivyopo pamoja na kusimamia uanzishwaji wa     vikundi vipya.
  5. Kuhamasisha     wafugaji nyuki kutenga maeneo ya Hifadhi za nyuki/ Manzuki ili kupata     umiliki wa ardhi na kurahisisha usimamizi wake.
  6. Kuhamasisha     / Kuelimisha jamii (wakulima) kunyunyizia dawa za kuulia wadudu kwenye     mimea ambayo haijatoa maua ili kuepuka kuua nyuki wanapoenda kuchukua     chakula chao (Maji matamu - Nector).
  7. Kuhimiza /     kuhamasisha jamii kuanzisha mfumo wa Kilimo- mseto unaohusisha Ufugaji     Nyuki.
  8. Kuingiza     shughuli za Ufugaji nyuki katika mpango wa matumizi bora ya ardhi.
  9. Kuhamasisha     wananchi wanaoishi sehemu ambazo zinafaa kwa ufugaji wa nyuki wasiouma     (milimani) hasa wanawake kuanzisha ufugaji wa nyuki wasiouma. 

 

  17.4 Mikakati Ya Kufanya Zao La Asali Kuwa Zao La Kiuchumi Linalotegemewa Na Wilaya

                                I.            Kuanzisha utaratibu wa kukagua mazao ya nyuki ili kudhibiti ubora wake.

                              II.            Kuanzisha na kusimamia vituo vya kukusanyia na kuchakata asali.

                          III.            Kuwa na utaratibu wa kupima asali ili kudhibiti ubora wake.

                          IV.            Kuanzisha utaratibu wa kuweka asali katika madaraja ili kupata bei nzuri. (Viwango vya ubora wa asali vitumike)

                              V.            Kutoa mafunzo na kuelimisha wafugaji nyuki (wazalishaji) na wafanyabiashara wadogo kuhusu njia bora zaidi za kutunza mazao ya nyuki.

                          VI.            Kuhakikisha vifaa vya uvunaji, uchakataji, ufungashaji, uhifadhi na usafirishaji wa asali vinapatika kwa urahisi.

                        VII.            Kuandaa mwongozo wa sheria ndogo kuhusu makusanyo ya mapato (ushuru) utokanao na mazao ya nyuki kwa wafanyabiashara wanaosafirisha nje ya Wilaya.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

18.   KITENGO CHA UWEKEZAJI

Halmashauri ya Wilaya ya Same ni miongoni ya wilaya 6 katika Mkoa wa Kilimanjaro ambayo inafursa za uwekezaji katika maeneo mbalimbali, ikiwemo sekta ya kilimo, madini, usafiri, utalii, ujenzi, uvuvi, ufugaji, mifugo, viwanda, biashara na kijamii (Elimu, Afya na Maji) na Kiutamaduni (Michezo na Utamaduni).n.k. Uwekezaji kwa mujibu wa kitaifa pia unalenga katika kuwezesha maendeleo ya nchi lakini pia kwa wakazi kufaidika na fursa mbalimbali.

 

18.1 Idadi ya wawekezaji waliopo na aina ya uwekezaji

                                                                                                                                                         
 

Na

 
 

Jina la mwekezaji

 
 

aina ya uwekezaji

 
 

Mahali ulipo

 
 

Maelezo

 
 

1.

 
 

Willy Enterprises

 
 

Madini ya boxite

 
 

Mwembe/Chome

 
 

Mwekezaji anachimba madini hayo na kupeleka katika nchi ya Kenya

 
 

2.

 
 

Umoja wa wakulima wa Tangawizi

 
 

Kilimo cha tangawizi

 
 

Myamba

 
 

Umoja wa ushirika unawanachama zaidi 600

 
 

3. 

 
 

 

 
 

Kiwanda cha Tangawizi

 
 

Myamba

 
 

Kiwanda kimesimama

 
 

4.

 
 

Miller International Agrovet

 
 

Kilimo cha vitunguu

 
 

Kijiji cha Jiungeni

 
 

Miller inamiliki eneo la zaidi ya ekari 400.

 
 

5.

 
 

SMK

 
 

Kilimo cha vitunguu

 
 

Kijiji cha Jiungeni

 
 

Anamiliki zaidi ya ekari 200 za vitunguu

 
 

6.

 
 

Tona lodge

 
 

Utalii/Asili

 
 

Kata ya Mshewa

 
 

Uwekezaji unafanya shughuli za utalii wa asili

 
 

7.

 
 

MKUNAPA

 
 

Utalii/wanyama pori

 
 

Mbuga ya Mkomazi

 
 

Eneo la uwekezaji linalolimilikiwa ni ekari 3245.

 
 

8.

 
 

KIDC

 
 

Kiwanda cha vikombe

 
 

Kata ya Same

 
 

Kiwanda hakifanyi kazi kwa ufanisi kutokana na uongozi.

 
 

9.

 
 

Makampuni ya simu

 
 

Mitandao ya simu

 
 

Wilaya ya Same

 
 

Makampuni ya simu ya Airtel, Haloteli Tigo, Vodacom na Zantel

 
 

10.

 
 

Mashirika ya Fedha

 
 

Huduma ya ya fedha

 
 

Wilaya ya Same

 
 

NMB, CRDB, Same Kaya SACCOs, CWT, Amacha, BRAC n.k. 

 

 

19.2 Vivutio vya uwekezaji vilivyopo

                                                                                         
 

Na.

 
 

Aina ya kivutio cha uwekezaji

 
 

Vivutio

 
 

1.

 
 

Mbuga ya Taifa ya Mkomazi yenye ukubwa wa ekari 3245

 
 

Wanyama wa aina mbalimbali, ndege na eneo lenye miti ya asili

 
 

2.

 
 

Uchimbaji wa madini

 
 

Eneo la uchimbaji jasi, green garnet, green tourmaline, rhodilite  na boxite.

 
 

3. 

 
 

Bwawa la Kalimawe  na  Karamba

 
 

Aina ya samaki kama vile: Tilapia, perege, kambale na mkunga.  Bwawa ili lina kilomita za mraba 3.

 
 

4.

 
 

Msitu wa Shengena hekta 27,880

 
 

Aina ya miti, vipepeo, nyuki, ndege, mbega, nyani, tumbili na  maji yanayotiririka kwa mwaka mzima.

 
 

5.

 
 

Mawasiliano na miundo mbinu

 
 

Kuna barabara zinazopitika kwa mwaka mzima, mitandao ya simu na  usafiri wa kampuni za Kilenga, Kimbwe na Phiba.

 
 

6.

 
 

Ujenzi wa viwanda

 
 

Kuna maeneo ya ujenzi wa viwanda kama:- saruji n.k

 
 

7.

 
 

Mto Pangani 

 
 

Mto Pangani unaopita katika Kata ya Ruvu wenye urefu wa km 91,  maji yanafaa kwa kilimo cha umwagiliaji na ufugaji wa samaki. 

 
 

8.

 
 

Huduma za Malazi (Hotel)

 
 

Katika Wilaya tuna wawekezaji katika huduma za malazi km  Elephant Motel, Orlando, Nzoroko n.k.

 

Chanzo: Kitengo cha Uwekezaji

18.3 Maeneo yaliyotengwa kwa uwekezaji

Halmashauri ya wilaya ya Same imetenga jumla ya ekari kama ifuatavyo:-

-Eneo la Kitamri Halmashauri imetenga ekari 150 kwa ajili ya ujenzi wa viwanda

-Eneo la Kata ya Makanya Kijiji kimetenga jumla ya ekari 100 kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda cha saruji.

Mkakati wa halmashauri ya uendelezaji wa fursa za uwekezaji;-

Ø   Halmashauri imeandaa mpango wa kujenga mazingira kwa makundi haya ya wakulima wadogo na wafugaji kuchangamkia fursa hizi badala ya kuelekeza jitihada kubwa katika uwekezaji kutoka nje.

Ø   Halmashauri inautaratibu wa kuwashirikisha wawekezaji kutoka nje wawekeze katika msingi wa ubia na wazalishaji wadogo, kwa maana kuwa wazalishaji wadogo - wakulima na wafugaji - katika vikundi vyao, msingi wao mkubwa ukiwa ni rasilimali ardhi, wanaweza kuingia katika ubia na wawekezaji toka nje kwa namna ambayo wanakuwa na sauti katika maamuzi na hivyo kuwezesha kile tukiitacho win win situation, yaani 'hali ya mafanikio kwa pande zote zinazohusika'.

Ø   Halmashauri inawezesha vikundi vya wajasiriamali wadogo kwa kuwapa mikopo ya riba nafuu ili kuwa na fursa za wazalishaji wadogo vijijini. 

Ø   Halmashauri kwa kushirikiana na wawekezaji kuimarisha miundombinu ya barabara na mawasiliano ya simu katika maeneo ya Wilaya ya Same.

 

18.4 Mikakati ya kuwa na viwanda Wilayani

·        Kampuni ya DOTT Services (T) imeanza mazungumzo na Halmashauri kwa ajili ujenzi wa kiwanda cha kuparck maji na uvunjaji wa kokoto katika eneo la Saweni.

·        Uwekezaji wa kiwanda cha saruji katika Kata ya Makanya, ambapo mkakati wa kumpatia mwekezaji wa kampuni ya A to Z toka Arusha. Taratibu za kupata eneo katika Kata ya Makanya (Vikao vya awali vya kijiji cha Makanya vimekwisha fanyika)

·        Kilimo cha miwa; Uwekezaji wa kilimo cha miwa kampuni ya Kilimanjaro Biochem Limited inayomiliki kiwanda cha utengenezaji wa spiriti katika wilaya ya Mwanga kimeanza maandalizi ya kuwa na mikataba na wakulima ili waweze kulima miwa katika kata ya Ruvu. KBL inahitaji kulimiwa miwa kiasi cha ekari 2000 wameanza mazungumzo na wakulima wa maeneo ya kata ya Ruvu. Endapo wakulima wataridhia mikataba hiyo, kampuni hiyo imepanga kujenga kiwanda katika eneo la Ruvu Muungano cha kukamua miwa na kusafirisha ikiwa maji ya miwa (syrup). Kiwanda hicho kitakuwa na uwezo wa kuajiri wafanyakazi zaidi ya 200. (Ombi la KBL liliwasilishwa kwenye kamati ya Fedha, Utawala na Mipango).

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

19.   CHANGAMOTO ZA KIWILAYA

19.1Njaa 

 

 

 

 

 

 

19.2Migogoro ya Wakulima na Wafugaji

 

 

 

 

 

 

 

 

 

19.3Changamoto zingine

 

 

 

 

 

 

 

 

 

20.   MIKAKATI YA KIWILAYA

20.1Kumaliza Tatizo la Njaa

·      Kuhakikisha elimu ya uvunaji maji ya mvua, matumizi bora ya maji  na hifadhi ya ardhi na udongo imetolewa kwa wakulima.

·      Kutoa elimu kwa wakulima juu ya kuzuia/kupunguza upotevu wa

     mazao ya nafaka na mikunde wakati wa kuvuna na kuhifadhi    

     (Post harvest loss handling).

·      Kuhakikisha elimu ya ukadiriaji wa mahitaji ya mazao ya chakula kwa wakulima ngazi ya kaya imetolewa.

·      Kutoa elimu kwa wakulima juu ya hifadhi na matumizi bora ya mazao ya chakula kwa maeneo ambayo yamepata mavuno mazuri msimu wa vuli hasa maeneo ya kilimo cha umwagiliaji.

·      Kutoa ushauri kwa wakulima kutekeleza kilimo cha mazaoyanayostahimili ukame na yanayotumia kiasi kidogo cha unyevu hadi kukomaa kama  mazao jamii ya mizizi na mikunde na Mtama.

·      Kuhakikisha uimarishaji wa matumizi bora ya maji katika  miundombinu ya umwagiliaji iliyopo na kuhakikisha kunakuwepo na ongezeko la uzalishaji wa mazao ya chakula kwa misimu miwili na wakulima wanazingatia ushauri wa wataalam waliopo vijijini.

·      Kwa kuwatumia Maafisa Ugani waliopo kuhakikisha wakulima wanatumia teknolojia bora na sahihi za uzalishaji mazao ya chakula na biashara kwa ajili ya uhakika na usalama wa chakula ngazi ya kaya.

·      Kuhimiza wafugaji walio na mifugo kuuza wakati bado ikiwa na hali nzuri ya kiafya na kununua chakula na kuhifadhi kwa ajili ya matumizi ya familia.

·      Kuhimiza wakulima waliopo maeneo ya umwagiliaji kulima mazao yenye thamani na ubora kwa uhakika wa kuongeza kipato hatimaye kumudu kujinunulia chakula cha kutosha.

·      Kuhamasisha wafanyabiashara wenye uwezo  kununua chakula Katika maeneo yenye chakula cha ziada na kuleta kuuza katika maeneo yenye upungufu kwa bei nafuu/elekezi.

 

 

 

20.2Kumaliza Tatizo la Migogoro ya Wakulima na Wafugaji

 

 

 

 

 

 

20.3Kuongeza Pato la Mwananchi

 

 

 

 

 

 

20.4Kuongeza Mapato ya Halmashauri

 

 

 

 

 

 

 

20.5Kuongeza Fedha tunayochangia kwenye Mfuko wa Taifa (TRA)

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

20.6Kuongeza na Kuboresha Viwanda

·        Kampuni ya DOTT Services (T) imeanza mazungumzo na Halmashauri kwa ajili ujenzi wa kiwanda cha kuparck maji na uvunjaji wa kokoto katika eneo la Saweni.

·        Uwekezaji wa kiwanda cha saruji katika Kata ya Makanya, ambapo mkakati wa kumpatia mwekezaji wa kampuni ya A to Z toka Arusha. Taratibu za kupata eneo katika Kata ya Makanya (Vikao vya awali vya kijiji cha Makanya vimekwisha fanyika)

·        Kilimo cha miwa; Uwekezaji wa kilimo cha miwa kampuni ya Kilimanjaro Biochem Limited inayomiliki kiwanda cha utengenezaji wa spiriti katika wilaya ya Mwanga kimeanza maandalizi ya kuwa na mikataba na wakulima ili waweze kulima miwa katika kata ya Ruvu. KBL inahitaji kulimiwa miwa kiasi cha ekari 2000 wameanza mazungumzo na wakulima wa maeneo ya kata ya Ruvu. Endapo wakulima wataridhia mikataba hiyo, kampuni hiyo imepanga kujenga kiwanda katika eneo la Ruvu Muungano cha kukamua miwa na kusafirisha ikiwa maji ya miwa (syrup). Kiwanda hicho kitakuwa na uwezo wa kuajiri wafanyakazi zaidi ya 200. (Ombi la KBL liliwasilishwa kwenye kamati ya Fedha, Utawala na Mipango).

 

 

 

 

 

 

 

 

20.7Kuongeza Ajira kwa Vijana 

HALMASHAURI YA WILAYA YA SAME

TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI MBALIMBALI ZA KISEKTA KWA MKUU WA WILAYA YA SAME BI. ROSEMARY SITAKI

UTANGULIZI

Halmashauri ya Wilaya ya Same ilianzishwa rasmi kwa Sheria ya Bunge Sura ya 287 (Mamlaka za Wilaya) ya Sheria za Tanzania na ilianza kutekeleza majukumu yake tarehe 01 Januari 1984. Aidha Halmashauri ina Idara 13 na vitengo 6 ambavyo vinatekeleza majukumu mbalimbali kama ambavyo imeanishwa hapo chini:-

 

IDARA YA AFYA  

1.1 Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF)

Asilimia 30.6 ya kaya za Wilaya ya Same zimejiunga na CHF. Kwa Mkoa wa Kilimanjaro Wilaya ya Same ni ya 3 Kati ya Wilaya saba za Mkoa.

1.1.1 Mipango/Mikakati Iliyopo kufikisha 80%

  1. Kuhakikisha walengwa wanaopata Fedha kupitia mpango wa Kaya maskini-TASAF wanajiunga na mfuko wa CHF
  2. Kutumia wanafunzi wa shule wakiwa kwenye makundi ya watu sita kujiunga na CHF kwa mfano Same Sekondari.
  3. Bodi ya Afya ya Wilaya kufanya ziara ya uhamasishaji kwa kamati za vituo vya Afya kujiunga na CHF.
  4. Kamati za Afya za vituo kufanya uhamasishaji kwa jamii kupia mikutano ya vijiji na CHF kuwa Agenda ya kudumu kwenye vikao vya vijiji.

 

Jedwali 1.1: Vituo Vya Kutolea Huduma Za Afya Wilayani

S/No

AINA YA KITUO

IDADI

 

 

SERIKALI

MASHIRIKA YA DINI

BINAFSI

JUMLA

1

Hospitali

1

1

-

2

2

Vituo vya Afya

6

1

1

8

3

Zahanati

39

15

9

62


Jumla

46

17

10

72

Chanzo: Idara ya Afya

1.3 Hali ya upatikanaji wa dawa na vifaa tiba

  • Upatikanaji wa dawa na vifaa tiba katika vituo vya kutolea huduma ni wa wastani, hii imesababishwa na upungufu wa dawa na vifaa tiba kutoka bohari ya dawa (msd), pia msd kutotoa ruhusa ya kununua dawa na vifaa tiba mapema kutoka kwa wazabuni wengine. Vifaa vilivyopo kwenye Hospitali ya Wilaya ni X-ray, Ultrasound, Anaesthetic machine, Autoclave, Washing mashine, Generator, Microscope, Votex, Diathermy na Pima Machine.

1.4 Mkakati makini wa zoezi la usafi na Mipango ya kuwafanya watu wajenge tabia ya usafi

Kila kitongoji kuwa na siku moja ya usafi itakayoshirikisha kila mwananchi tofauti na siku ya jumamosi ya mwisho wa mwezi ya usafi kitaifa

Kuunnda/kuwa na vikundi kazi kwa kila kata vitakavyotokana na jamii , vitakavyohusika kusimamia usafi kwa kila kata na watakao kaidi watatozwa faini. Aidha asilimia kadhaa ya faini itakuwa ya vikundi/kikundi kutegemeana na makubaliano

Kila kata kuwa na Afisa afya atakayeshirikiana na wataalamu wengine waliopo kwenye kata. Kata ambayo haina Afisa afya ateuliwe afisa maendeleo ya jamii kukaimu nafasi ya Afisa afya

Kuchukua hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kuwafikisha mahakamani wote watakaokiuka sheria na kanuni za afya ya mazingira

Kuwa na dampo la taka ngumu na taka maji katika Halmashauri

Kuwa na vitendea kazi, gari rasmi la kusomba taka na ada za uzoaji taka zitumike kwa makusudi ya uzoaji taka

Kuwezesha walezi wa kata siku 5 kila robo mwaka kwa ajili ya kutembelea kata na kuhamasisha jamii juu ya usafi wa mazingira

Kila biashara/ kaya kuwa na chombo/vyombo vya kuhifadhia taka

Kushinadanisha kitongoji au mtaa, kata na kata ili kuleta ushindani na kuboresha usafi

Kujenga vizimba vya taka katika maeneo yatakayo ainishwa Elimu ya usafi na mazingira ikaziwe shuleni (shule za msingi, sekondari na vyuo) mahali pa kazi yao.

 

 

 

1.5 Idadi ya Watumishi waliopo, Ikama na Pungufu ndani ya Idara 

Idara ya afya inahitaji jumla ya watumishi 1114 waliopo ni 462, idara ina upungufu wa watumishi 689. Sawa na 61.8%. Hospitali ya Wilaya inahitaji Watumishi kwa kada kama ifuatavyo:-

Jedwali 1.1: Idadi ya Watumishi waliopo, Ikama na Pungufu ndani ya Idara

   

FANI YA MTUMISHI

HITAJIKA

WALIYOPO

PUNGUFU

Medical Doctor

23

4

19

Assistant Medical officer

39

3

36

Assistant Dental officer

1

-

1

Dental therapist

2

1

1

Pharmacist

2

1

1

Pharmaceutical Technologist


5


AssistantPharmaceutical Technologist

8

-

8

Social welfare

3

-

3

Environmental  officer Health officer

2

1

1

Wauguzi

99

71

28

Laboratory scientist

1

1

-

Health laboratory technologist

4

4

-

AssistantHealth  laboratory technologist

4

1

3

Occupational therapist

2

1

1

Physiotherapist

2

2

-

Medicall attendants

59

44

15

Health secretary

1

1

-

Medical recoder

5

1

4

Radiology scientist

1

-

1

Radiographer technologist

3

-

3

Nutritionist

1

1

-

Ophthalmologist

1

1

-

Optometrist

3

-

3

Economist

1

-

1

Biomedical technologist

4

-

4

Motury attendants

5

-

5

Computer system analysit

1

-

1

Computer operator

1

-

1

Accountant

1

-

1

Assistant Accountants

2

-

2

Supplier officer

1

-

1

Assistant supplier officer

1

1

-

Electrical Technician

4

-

4

Personal secretary

1

1

-

Plumber

1

-

1

Security guard

4

2

2

Cooker

4

-

4

Dhobi

4

-

4

Driver

5

2

3






Chanzo: Idara ya Afya

Kwa upande wa Hospitali ya Wilaya, kutokana na staffing level 2014-2018 Hospitali ya wilaya ina upungufu wa watumishi 97.

1.6 Magonjwa Kumi yanayoongoza kwa Idara ya Wagonjwa wa Nje ni:

Magonjwa ya njia ya hewa, Nimonia, Malaria, Magonjwa ya kuhara, Minyoo ya tumbo, Magonjwa ya ngozi, Magonjwa mengine, Upasuaji wa dharura, Upungufu wa damu na Magonjwa ya macho.

1.7 Magonjwa Kumi yanayoongoza kwa Idara ya Wagonjwa wa Ndani ni: Nimonia, Magonjwa ya njia ya hewa, Magonjwa mengine, Malaria kali, Upungufu wa damu, Magonjwa ya kuhara, Watoto waliozaliwa na uzito mdogo, Upasuaji wa dharura, Ukimwi na Majeraha mbalimbali.

1.8 Vifo Vya Watoto Umri Chini Ya Siku 28

Mwaka 2015 vilitokea vifo 5 katika vizazi hai 1000

1.9 Vifo Vya Watoto Chini Ya Miaka 5

Mwaka 2015 vilitokea vifo 8 katika vizazi hai 1000

 

 

 

1.10 Hali Ya Maambukizi Ya Virusi Vya UKIMWI

Kiwango cha maambukizi ni 1.4%, Watu wanaoishi na VVU ni 6,181, wanaotumia dawa ni WAVIU 4, 688, vituo vinavyotoa huduma kwa WAVIU ni 8, na huduma kwa njia ya kliniki ya mkoba ziko 9.

 

1.11 Changamoto

Idara ya afya inapambana na Changamoto zifuatazo: -

Upungufu wa watumishi wenye taaluma mbalimbali kwa asilimia 61.4%

 Kuchelewa kupokea fedha za mfuko wa pamoja na kutokupokea kabisa fedha za kutokana na kutokupata fedha za matumizi mengineyo (OC) ruzuku kutoka serikali kuu tangu mwezi Januari 2016

Wodi zilizopo ni ndogo hazikidhi mahitaji.

Upungufu na uchakavu wa nyumba za watumishi katika ngazi zote za vituo vya huduma.

Maabara ya Hospitali ya wilaya ni ndogo, Halmashauri imeanza funya mawasiliano na marafiki wake wa Tillburg Partnership Uholanzi ili kupata fedha za ujenzi wa Maabara mpya.

Kutokupokea fedha ya kulipa watumishi walioitwa kazini (on call allowance) tangu mwezi Janauri 2016.

1.12 Mikakati ya kupambana na Changamoto 

Ili kupambana na changamoto hizo, idara imeweka mikakati ifuatayo:

Kuomba vibali vya ajira na kuweka vivutio kwa waajiriwa wapya na watumishi kwa ujumla (Staff attraction and Retention strategies)

Kushirikiana na Bohari ya dawa (MSD) kuboresha upatikanaji wa dawa na vifaa tiba, kwa kuhakikisha kwamba kila kituo kinaandaa na kutuma taarifa na maombi ya dawa na vifaa – tiba kwa wakati kwenda MSD, na Idara kufuatilia maombi hayo ili yafanyiwe kazi na makasha kusambazwa vituoni kwa wakati muafaka.

Halmashauri tayari imeomba mkopo wa dawa kutoka Mfuko wa Taifya wa Bima ya Afya na inakarabati chumba kwa ajili ya duka la dawa ndani ya hospitali ya Wilaya ili kukabiliana na changamoto ya wagonjwa kununua dawa na vifaa tiba nje ya hospitali.

Kushirikisha wadau wengine wa sekta ya Afya katika upatikanaji wa           Vifaa tiba na vitendea kazi Muhimu vya kutolea huduma bora za afya. Hadi sasa Idara imewashirikisha Tillburg Partnership (Uholanzi), PSPF, CRDB na NMB. Bado Idara inatafuta wadau wengine.

Kuwashirikisha wadau mbalimbali ili kupata fedha za kujengea jengo la kusubiria wajawazito na wodi za wagonjwa katika Hospitali ya wilaya.

Kuendelea kuomba fedha serikali kuu kwa ajili ya ruzuku, posho za kuitwa kazini na posho ya kujikimu kwa waajiriwa wapya.

2.0 IDARA YA ELIMU MSINGI

2.1 Utangulizi

Halmashauri ina jumla ya shule za Msingi 192 kati ya hizo shule 185 ni za Serikali na 7 ni za binafsi. Shule hizi ziko katika Kata za Kiutawala 34 na Kata 1 ya Kielimu.. Shule hizi zina jumla ya wanafunzi 59833 kati yao wasichana ni 30613 na wavulana ni 2920.

2.2 Ufaulu wa Wanafunzi

Kiwango cha kufaulu kwa Mtihani wa Taifa darasa la Saba Kimkoa na Kitaifa ni kama ifuatavyo:-

Jedwali 2.1: Ufaulu wa Mtihani wa Taifa darasa la Saba Kimkoa na Kitaifa

MWAKA

KIWANGO CHA UFAULU (%)

NAFASI KIMKOA

NAFASI TAIFA

2014

63.48

7

52

2015

75.94

6

51

Chanzo: Idara ya Elimu Msingi

2.3 Malengo Ya Kuongeza Ufaulu

Ili kufikia malengo ya asilimia themanini na tano ya ufaulu (85%), Halmashauri kupitia idara ya Elimu Msingi imeweka mikakati ya kukabiliana na tatizo la ufaulu duni katika mitihani ya ndani na ya kitaifa kama ifuatavyo:

Kufuatiliaji utendaji kazi wa walimu katika Uongozi na Utawala na Utekelzaji wa Mtaala. Zoezi lilianza kwa kufuatilia shule 35 zilizofanya vibaya zaidi

Kuomba walimu toka TAMISEMI ili tuweze kupunguza upungufu mkubwa wa walimu.

Kuhamashisha wazazi na walezi kuchangia chakula cha mchana ili wanafunzi wapate chakula cha mchana shuleni.

Shule zote zimepewa maagizo ya kutekeleza Ratiba ya ufundishaji wa muda wa ziada ili kurekebisha mapungufu yaliyojitokeza kipindi kilichopita.

Halmashauri kwa kushirikiana na wadau mbali mbali wa elimu itaendelea kutoa mafunzo ya mbinu za ufundishaji kwa walimu mfano semina ya somo la Lugha na Hisabati.

Idara inaendelea na mpango wa kusoma na kutafisiri mpango wa kuinua taaluma ya Mkoa wa  Katavi ujulikanao kama “ Katavi model” ili uweze kuhawilishwa na kutumika katika wilaya ya Same kwa lengo la kuinua na kuboresha taaluma.

Kuhimiza na kusimamia mazoezi ya mwisho wa wiki, mwezi, mitihani ya utamirifu na ile ya Mwisho wa mihula ili kuchochea ushindani katika ngazi ya darasa, shule, Kata, Tarafa, Wilaya na Mkoa.

Kupitia na kutekeleza Ushauri na Mapendekezo Mthibiti Ubora wa Elimu shuleni.

Kutoa motisha chanya kwa walimu, wanafunzi na shule zilizofanya vizuri katika mitihani ya utamirifu Wilaya, Mkoa na Mitihani ya Kitaifa.

Jedwali 2.2: Miundo Mbinu Ya Shule: Samani Na Majengo

SAMANI

MAHITAJI

VILIVYOPO

UPUNGUFU

MADAWATI

26389

32775

6387

MEZA

2914

1719

1195

VITI

3211

1692

1519

KABATI

1714

523

1191

MAJENGO

 

 

 

NYUMBA ZA WALIMU

1463

368

1095

MADARASA

1551

1298

253

VYOO

2602

1599

1003

STOO

370

93

277

OFISI

372

295

77

Chanzo: Idara ya Elimu Msingi

2.4 Hali Ya Walimu Katika Shule Za Msingi:

Hali ya walimu ni kama ifuatavyo:-

 Jedwali 2.3: Walimu wa Shule Za Msingi Kwa Madaraja

SIFA

MAHITAJI

WALIOPO

PUNGUFU

ME

KE

JML

DARAJA IIIA

1999

558

846

1404

 

 

581

STASHAHADA

7

7

14

SHAHADA

0

0

0

JUMLA

565

853

1418

Chanzo: Idara ya Elimu Msingi

  Jedwali 2.4: Idadi Ya Walimu Katika Shule Za Msingi (Angalia Kiambatisho)

MAHITAJI

WALIOPO

ASILIMIA

UPUNGUFU

ASILIMIA

1999

1418

70.9

581

29.1

Chanzo: Idara ya Elimu Msingi

2.5 Utoaji wa Chakula Shuleni

 Idadi ya shule zinazotoa chakula katika wilaya Same ni 17 kati ya 185 shule hizo Nasuro, Daghaseta, Mughungani, Mkanyeni, Mwembe, Mshewa, Kafingiro, Goma, Kwizu Mrindi, Manka, Kweresha ,Kiomande, Parane, Ivuga, Mpinji na Tae.

 

2.6 Hali Ya Mimba

Hakuna taarifa ya mwanafunzi aliyepata mimba toka mwezi Januari hadi sasa

 

2.7 Changamoto Mbalimbambali Zilizopo 

Shule za Msingi Wilaya ya Same zinakumbana na changamoto mbali mbali, ambazo zinasababisha ufaulu wa wanafunzi kuwa wa kiwango cha chini. Baadhi ya changamoto hizo ni :

Uhaba wa nyumba za walimu katika maeneo ya shule.

Kukosekana kwa chakula cha mchana kwa wanafunzi shuleni.

Upungufu mkubwa wa Walimu.

Upungufu wa rasilimali fedha na vifaa kwa ajili ya ufuatiliji utendaji kazi wa walimu

3.0 IDARA YA ELIMU SEKONDARI 

3.1 Utangulizi

Halmashauri ya Wilaya ya Same ina jumla shule 51 za sekondari, kati ya shule hizo 36 ni za serikali na 15 ni za binafsi. Mwaka 2015 shule 47 za sekondari ndizo zilikuwa na watahiniwa wa shule wa Mtihani Taifa kidato cha nne. Shule moja ya Hedaru Sekondari haikufanikiwa kupata matokeo mpaka tathmini hii inafanyika kutokana na kutokuwasilisha nyaraka muhimu Baraza kwa wakati.

  • 3.2 Idadi ya Wanafunzi, kabla na baada ya Uhakiki

Idadi ya Wanafunzi, kabla na baada ya Uhakiki ni kama ilivyoainishwa katika Majedwali hapa chini;


  • Jedwali 3.1: Idadi ya Wanafunzi kabla ya Uhakiki

Chanzo: Idara ya Elimu Secondari

  • Jedwali 3.2: Idadi ya Wanafunzi baada ya Uhakiki
         

IDADI YA WANAFUNZI ILIVYO MWEZI AGOSTI, 2016 BAADA YA UHAKIKI


KID I

KID II

KID III

KID IV

KID V

KID VI

JUMLA KUU


ME

KE

JML

ME

KE

JML

ME

KE

JML

ME

KE

JML

ME

KE

JML

ME

KE

JML

ME

KE

JML


2133

2553

4686

1748

2142

3890

1162

1293

2455

1568

1865

3433

438

0

438

459

0

459

7508

7853

15361



Chanzo: Idara ya Elimu Secondari


  • 3.3 Hali ya Ufaulu Katika Mitihani ya Kitaifa

Watahiniwa waliosajiliwa kufanya mtihani huo walikuwa 5044, kati yao wasichana ni 2816 na wavulana ni 2228.watahiniwa waliofanya mtihani walikuwa ni 4958 na waliopata daraja la ufaulu kuanzia daraja I-IV ni 2809 sawa na asilimia 56.6 ya waliofanya mtihani huo, ambapo watahiniwa 2149 walifeli, sawa na asilimia 43.4. Aidha, ufaulu huu umeshuka kwa asilimia 1.6 ukilinganisha na ufaulu wa mwaka 2014 ambapo ulikuwa ni asilimia 58.2.

Aidha, matokeo ya kidato cha pili, 2015, Watahiniwa waliosajiliwa kufanya mtihani wa upimaji walikuwa 4977, kati yao watahiniwa waliofanya mtihani walikuwa 4720 sawa na aslimia 94.8 ya waliosajiliwa. Kati ya Watahiniwa 4720 waliofanya Mtihani wa upimaji wa Taifa kidato cha pili, Watahiniwa waliopata madaraja ya ufaulu walikuwa 3856 sawa na asilimia 82 ya waliofanya mtihani. Watahiniwa waliofeli walikuwa 864 sawa na asilimia 18 ya waliofanya mtihani.

3.2.1 Mchanganuo wa Ufaulu Kidato cha Nne 

Kufuatia utaratibu ambao  Baraza la Mitihani la Tanzania limetumia kutunuku matokeo ya mtihani wa taifa wa kidato cha nne 2015 kwa kutumia madaraja ya ufaulu kama ilivyokuwa mwaka 2013 na kurudi nyuma, matokeo ya kila shule yameainishwa katika madaraja matano ambayo ni “daraja la kwanza, pili, tatu, nne na waliofeli. Ufaulu huo kimadaraja ni kama ifuatavyo;

  • Jedwali 3.3: Hali ya ufaulu kimadaraja

 Chanzo: Idara ya Elimu Secondari

  •  

 

 

 

3. 2.2 Nafasi Ya Wilaya Kimkoa Na Kitaifa

Katika mtihani wa taifa wa kidato cha nne (CSEE) mwaka 2014 wilaya ilishika nafasi ya 96. Kwa mwaka 2015 wilaya imeshika nafasi 7 kati ya wilaya 7 kimkoa na nafasi ya 102 kitaifa. Aidha, katika mtihani wa upimaji wa kidato cha pili (FTNA) kwa mwaka 2014, wilaya ilishika nafasi ya 47, na mwaka 2015 wilaya imeshika nafasi ya 57.

  • Mikakati ya Kuinua Taaluma Kiwilaya
  1. Kuendelea kufanya ufuatiliaji wa ufundishaji na ujifunzaji mashuleni katika   kuhamasisha   walimu na wanafunzi kutimiza wajibu na majukumu yao  ipasavyo
  2. Fomu ya mahdhurio ya walimu darasani na mahudhurio ya walimu kwa mwezi zimeandaliwa na zinatumika. Ambapo kila mwisho wa mwezi inawasilishwa ofisi ya Afisa  Elimu ili kujiridhisha namna ufundishaji na ujifunzaji unavyoendelea shuleni
  3. Mawasiliano yamefanyika  kuiomba serikali kupanga walimu wa sayansi kwa shule za serikali ambazo zinaupungufu mkubwa
  4. Walimu kuendelea kuandaa na kutumia nyaraka muhimu za ufundishaji kama inavyoelekezwa na mamlaka husika
  5. Walimu kufanya tathmini ya mitihani mbalimbali inayofanyika shuleni      

vi.   Wakuu wa shule wameagizwa kushirikiana na waratibu Elimu Kata kudhibiti utoro wa           wanafunzi ambao hawahudhurii masomo badala yake wanakuja siku za mitihani tu.

  1. kutoa motisha kwa walimu na wanafunzi wanaofanya vizuri katika mitihani ya taifa.
  2. Kupitia vikao vya wazazi, WDC bodi za shule msisitizo ni  kwamba wazazi kushirikiana na walimu pamoja na jamii nzima kutoa malezi mfungamano yatakayosaidia kuboresha taaluma na kuwafanya wanafunzi kuwa na nidhamu nzuri.
  3. Idara inaendelea na mpango wa kusoma na kutafisiri mpango wa kuinua taaluma ya Mkoa wa  Katavi ujulikanao kama “ Katavi model” ili uweze kuhawilishwa na kutumika katika wilaya ya Same kwa lengo la kuinua na kuboresha taaluma. Aidha, baada ya kusoma na kutafsiri, idara itaandaa mpango wake na kuwasilishwa kama ilivyoelekezwa.
  • Hali ya Madarasa/ Vyoo/ Nyumba za Walimu/Maabara na Mikakati ya ukamilishaji

Kwa upande wa hali ya Madarasa, Vyoo na Nyumba za Walimu ni kama ilivyoainishwa katika jedwali lifuatalo;

  • Jedwali 3.4: Madarasa, Vyoo, Nyumba za Walimu

 Chanzo: Idara ya Elimu Secondari

  • Idadi ya Walimu ukilinganisha na Ikama

Kwa upande wa Idati ya Walimu, tuna uhaba mkubwa kwa upande wa Walimu wa Masomo ya Sayansi ukilinganisha na Walimu wa Masomo ya sanaa ambao wapo wakutosha na baadhi ya masomo wamezidi. Mfano katika somo la Kiswahili kuna zidio la Walimu 32 na somo la Kingereza kuna zidio la Walimu 13 kama inavyoonekana katika jedwali hapa chini;

Jedwali 3.5: Idadi ya Walimu Wanaohitajika, Waliopo na Pungufu kwa kila somo

 Chanzo: Idara ya Elimu Secondari

3.6 Ukamilishaji wa Maabara

Idara imejitahidi kusimamia ujenzi wa maabara katika shule zote 36, kama ambavyo iliagizwa na Mh. Rais wa awamu iliyopita. Ambapo jumla ya vyumba vya maabara vilivyotakiwa ni 108. Kwa sasa vyumba ambavyo havijakamilika ni vinne (04), vyumba vilivyokamilika ni 104. Ambayo havijakamilika ni katika shule za sekondari Lugulu na Masheko ambazo zote ni shule mpya. Aidha katika baadhi ya shule samani za maabara hazijakamili pia bado kuna upungufu wa vifaa vya ufundishiaji na ujifunzaji kwa masomo ya sayansi.

3.7 Mikakati ya Ukamilishaji

Mikakati iliyopo katika kukamilisha ujenzi wa maabara hizo ni;

  1. WDC kupitia vikao vyao wameagizwa kuwa ukamilishaji wa ujenzi wa vyumba vya maabara iwe agenda ya vikao vyao kila wanapokutana.
  2. Wananchi kuendelea kuchangia michango ya fedha/vifaa vya ujenzi ili kukamilisha ujenzi na kuweka samani katika vyumba ambavyo bado havina samani.
  3. Wakuu wa shule kuendelea kununua vifaa vya kufundishia masomo ya sayansi kupita fedha ya ruzuku ya uendeshaji ambayo hutolewa na serikali kila mwezi.
  • Utoaji Wa Chakula Cha Mchana Kwa Wanafunzi wa Kutwa

Hali ya utoaji chakula katika shule za kutwa za serikali kwa sasa siyo nzuri, baada ya tangazo la Elimu bila malipo ambapo shule zote za sekondari zilikuwa zinatoa chakula cha mchana. Aidha, kwasasa idadi ya wanafunzi wanaopata chakula cha mchana ni kama ifuatavyo;  wanafunzi 8445 wanapata chakula na ambao hawapati chakula ni 6916.

Aidha, ofisi imepokea waraka wa Elimu Na. 3 wa mwaka 2016, ambao unawataka wajumbe wa bodi na wazazi kuhakikisha wanafunzi wote wa shule za sekondari za kutwa wanapata chakula cha mchana. Waraka huu umeshapelekwa shuleni kwa ajili ya utekelezaji.  Kama ilivyoelezwa katika kifungu cha 3.7 kamati / bodi za shule za serikali (iii) kushirikiana na wazazi/jamii kuweka utaratibu wa chakula cha mchana au chakula na huduma za hosteli katika shule za kutwa kulingana na mazingira yao, na kutuma mapendekezo kwa MkurugenziMtendaji wa Halmashauri.

 

3.9 Mikakati Ya Kudhibiti Utoro Na Mimba Shuleni

Hali ya utoro limekuwa tatizo sugu kwa baadhi ya wanafunzi, hii ni kutokana na baadhi ya wanafunzi kushiriki katika biashara za kuendesha boda boda na shughuli nyingine zinazofanywa na wazazi / walezi.

  1. Watendaji kata na Waratibu Elimu Kata na Wakuu wa shule wameandikiwa barua kuwachukulia hatua za kisheria wzazi/walezi ambao aidha kwa kujua au kuto jua watoto wao hawahudhurii masomo bila sababu zozote.  Barua zilizo andikwa ni za tarehe 02/06/2016 yenye Kumb. Na. WS/EL/UT.I7/VOL.VI/133. Barua ya waratibu Elimu Kata yenye Kumb. Na. WS/EL/UT.17/VOL.180 ya tarehe 22/08/ 2016
  2. Watendaji kata kuwa wachukulia hatua na kuwafungulia kesi Mahakamani wale wote wanaobainika kuwapa mimba wanafunzi.
  3. Jamii imehamasishwa kujenga hosteli kwa ajili ya wanafunzi wanaotembea umbali mrefu, ili wanafunzi wake wakae katika mabweni rafiki yanayoendeshwa na wazazi.
  4. Walimu kuendelea kutoa ushauri nasaha na unasihi kwa wanafunzi ili wasome kwa bidii bila kuathiriwa na mazingira ya nje ya shule.

Kupitia vikao vya bodi, wazazi /walezi, jamii kutoa malezi mfungamano, basipo kuangalia na kubagua watoto ili kuboresha nidhamu na kuwajengea uwezo wa kujitambua kama sehemu ya jamii wanayoishi.

Jedwali 3.6: Taarifa za Wanafunzi Watoro, Waliopata Mimba, Waliohama Na Kuhamia pamoja na Wanaopata na Wasiopata Chakula

                                                                               

S/N

SHULE

MIMBA

WATORO

WALIOHAMA

WALIOHAMIA

WANAOPATA CHAKULA

WASIOPATA CHAKULA



ME

KE

JML

ME

KE

JML

ME

KE

JML


1

BANGALALA

4

6

7

13

0

0

0

0

0

0

106

81


2

BEMKO

0

0

0

0

0

0

0

0

0

0

408

0


3

BOMBO

2

3

4

7

0

0

0

0

0

0

46

310


4

CHALAO

3

3

2

5

2

3


3

0

3

539

0


5

CHANJAGAA

1

3

5

8

0

0

0

0

0

0

100

112


6

GONJA

3

27

9

36

0

0

0

0

0

0

0

835


7

KASEMPOMBE

2

10

8

18

4

2

0

0

0

0

180

171


8

KAZITA

3

3

2

5

0

0

0

0

0

0

183

0


9

KIBACHA

2

13

15

28

0

0

0

0

0

0

765

0


10

KIGANGO

0

0

0

0

0

0

0

0

0

0

160

0


11

KIHURIO

2

2

4

6

0

0

0

0

0

0

193

349


12

KIMALA

1

7

9

16

0

0

0

0

0

0

491

0


13

KIRANGARE

1

4

2

6

4

1

0

0

6

0

50

363


14

KISIWANI

4

2

0

2

2

0

0

3

3

6

730

0


15

KWAKOKO

4

7

10

17

0

0

0

0

0

0

405

0


16

KWIZU

0

0

0

0

1

0

1

1

0

1

375

0


17

LUGULU

3

2

2

4

13

26

39

11

18

29

78

124


18

MABILIONI

1

2

1

3

2

7

9

2

16

18

140

306


19

MADIVENI

1

11

18

29

0

0

0

0

0

0

300

0


20

MAKANYA

1

13

6

19

0

0

0

0

0

0

497

0


21

MALINDI

0

2

0

2

1

1

2

2

0

2

153

117


22

MASHEKO

0

0

0

0

0

0

0

0

0

0

130

75


23

MKOMBOZI

3

22

0

22

0

0

0

0

0

0

48

1091


24

MOIPO

1

23

12

35

0

0

0

0

0

0

219

143


25

MTII

3

3

2

5

0

0

0

0

0

0

100

213


26

MVUREKONGEI

4

2

3

5

0

0

0

0

0

0

0

184


27

MYAMBA

0

1

0

1

0

0

0

0

0

0

245

321


28

NDUNGU

3

4

0

4

0

0

0

0

0

0

0

687


29

NTENGA

2

2

4

6

0

0

0

0

0

0

0

618


30

PARENI

2

1

2

3

3

4

7

0

0


274

0


31

SAME

0

2

0

2

0

0

0

0

0

0

756

0


32

SAWENI

0

6

12

18

0

0

0

0

0

0

252

0


33

TAE

0

6

8

14

0

0

0

0

0

0

145

72


34

VUDEE

1

6

4

10

0

0

0

0

0

0

198

58


35

VUMARI

0

7

8

15

6

4

10

4

5

9

96

459


36

VUNTA

0

9

5

14

0

2

2

0

0

0

83

227



JUMLA

57

214

164

378

38

50

88

26

48

68

8445

6916


IDARA YA MAJI

Upatikanaji wa Huduma ya maji 

Upatikanaji wa maji vijijini ni 70% na Vijiji vyenye maji ni 75

4.2 Mpango uliopo kwa mji wa Same

Mradi wa Maji wa Same – Mwanga – Korogwe unalenga kuhudumia watu 456,931 ifikapo mwaka 2038 katika Wilaya za Same (watu 264,793), Mwanga (watu 177,085) na watu 15,053 katika Wilaya ya Korogwe, kwenye vijiji 38 na miji ya Same na Mwanga. Mifugo na viwanda vidogo pia vitanufaika na mradi huu.

Katika Vijiji 38 vitakavyonufaika Vijiji vya Same ni Hedaru, Mabilioni, Gavao, Makanya, Mgwasi, Bangalala, Chajo, Mwembe, Njoro, Ishinde, Ruvu Mferejini, Ruvu Jiungeni, Majengo, Bendera, Mkonga Ijinyu, Mgandu (vijiji 16 katika Wilaya ya Same)

4.3 Utekelezaji wa Mradi

  1. Kwasasa awamu ya kwanza imeshaanza ambayo ni ujenzi wa wa chanzo na mitambo ya kutibu maji eneo la nyumba ya mungu ( Kisangara) na itakamilika ifikapo may 2017
  • Awamu ya nne ambayo ni kulete maji katika Mji wa Same, Mkandarasi ameshapatikana, anaitwa Badri East Africa Limited na alishafika eneo la kazi kujitambulisha. Ataanza kazi mara baada ya kusaini Mkataba na kulipwa malipo ya awali. Pia ataweka kambi (Camp Site) maeneo ya Same Mjini na Kijiji cha Njoro. Gharama za awamu hii ni  USD 52 milion sawa na shilingi 104 bilioni


KITENGO CHA ARDHI

Sekta ya ardhi ni mojawapo ya sekta iliyopo chini ya idara ya ardhi na maliasili inayosimamia masuala yote ya ardhi. Sekta ina sehemu 4 ambazo ni ardhi utawala, mipango miji, upimaji na ramani na uthamini. Idadi ya Vijiji vilivyopimiwa Ardhi, Idadi ya Vijiji vilivyofanyiwa Matumizi bora ya Ardhi, Idadi ya Migogoro Sugu ya Ardhi Mjini na Vijiji, Sababu za kutokea kwa Migogoro ya Ardhi na kusababisha migogoro hiyo kuwepo kwa muda mrefu, Mipango/Mikakati ya kumaliza Migogoro ya Ardhi, Mipango/Mikakati ya kuboresha Mji/Master plan, Hali ya Ukusanyaji wa Kodi za Viwanja na Nyumba pamoja na Idadi ya Miji yenye Sifa ya kuwa Miji Midogo ni kama ilivyoainishwa katika jedwali hapa chini;


Jedwali 5.1: Hali ya Utekelezaji wa Shughuli za Kitengo cha Ardhi

S/N

VIJIJI VILIVYOPIMWA

VIJIJI VILIVYOGAWANYIKA

VIJIJI VYENYE MATUMIZI BORA YA ARDHI

MIGOGORO SUGU

MIGOGORO YA KAWAIDA

SABABU ZA MIGOGORO

MIKAKATI YA KUMALIZA MIGOGORO

MIPANGO YA KUBORESHA MJI

UKUSANYAJI WA KODI ZA ARDHI/MAJENGO

MIJI YENYE SIFA YA KUWA MIJI MIDOGO

1

Halmashauri ya Wilaya ya Same ina jumla ya vijiji 100 kati ya Vijiji hivyo vilivyopimwa vilikuwa ni vijiji  84, kati ya vilivyokuwa vimepimwa vijiji saba (7) vimegawanyika kati ya Vijiji hivyo sasa vilivyogawanyika vimezaliwa Vijiji 16

-Chajo kimegawanyika na kuwa Kijiji cha Chajo na Nasuro.

-Tae kimegawanyika na kuwa Kijiji cha Tae, Heikonti  na Rikweni.

-Njoro kimegawanyika na kuwa Kijiji cha Njoro na Emuguri.

-Gavao Saweni kimegawanyika na kuwa Kijiji cha Gavao Ngarito na Saweni.

-Mabilioni kimegawanyika na kuwa Kijiji cha Mabilioni, Ruvu mbuyuni na Chekereli.-Hedaru kimegawanyika na kuwa Kijiji cha Hedaru, Kijomu na Gundusine. Bangalala kimegawanyika na kuwa Kijiji cha Bangalala na Mkanyeni.

Duma, Lugulu, Kanza na Mtii, Makanya, Hedaru na Gavao Saweni.

Kutokana na ufinyu wa bajeti Halmashauri imefanikiwa kuandaa mpango wa matumizi bora ya ardhi ya vijiji saba (7) kupitia ufadhili wa wadau wa maendeleo kama TFCG na Ongawa.

-Kijiji cha Makanya na Ruvu

- Kijiji cha Mgwasi na Makanya,

Kitongoji cha Kavambughu Ishinde.

-Maore na Mheza.

-Migogoro ya wakulima na wafugaji kata ya Ruvu.

Migogoro ya kawaida haiwezi kuhesabika kwani huibuka na kupatiwa ufumbuzi.

Baadhi ya wananchi wanadai kuchukuliwa maeneo yao bila kulipwa fidia.

Kukosewa mipaka ya vijiji katika ramani zilizopimwa na Wizara ya Ardhi

Wananchi kujenga bila vibali vya ujenzi kutoka mamlaka husika.

Kukagua vijiji vyenye migogoro ya mipaka na kuiandikia Wizara barua ili waje warekebishe mipaka hiyo.

Kuandaa mipango ya matumizi bora ya ardhi ili kumaliza migogoro ya wakulima na wafugaji.

Kubaini na kuhakiki uhalali wa madai ya wananchi ambao wanadai maeneo yao kuchukuliwa bila kulipwa fidia.

Halmashauri  kutafuta eneo kwa ajili ya kulipima ili kuwafidia wananchi hao.

Maandalizi yanafanyika ili kutenga fedha katika bajeti ijayo ili kuandaa master plan (Mpango kamambe) wa mji wa Same.

Ukusanyaji wa kodi za ardhi unaendelea vizuri.

Kodi ya majengo ndani ya Mamlaka ya Mji mdogo hukusanywa na mamlaka ya  Mji mdogo wa Same kama mapato ya ndani.

Katika Halmashauri ya Wilaya ya Same ipo miji ya kibiashara ambayo inakuwa kwa kasi na ina sifa ya kuwa miji midogo ambayo ni Hedaru,

Makanya,

Kisiwani,

Maore na

Ndungu.

Chanzo: Kitengo cha Ardhi


IDARA YA KILIMO

  • Eneo la  Kilimo na Mazao yanayolimwa
  • Eneo linalofaa kwa shughuli za kilimo katika Wilaya ya Same linakadiriwa kuwa na jumla ya hekta 45,000. Eneo linalofaa kwa kilimo cha umwagiliaji ni takriban hekta 20,000 ambazo kati ya hizo ni hekta 12,200 zinazotumika kwa umwagiliaji wa kisasa na wa asili.

Fursa zilizopo Wilayani kwa ajili ya shughuli za kilimo ni pamoja na kuwa na bonde zuri lenye maji ya mito upande wa Same Mashariki ukanda wa tambarare. Eneo hili lina Skimu za umwagiliaji ambapo mazao mbalimbali ya chakula na biashara huzalishwa kama vile Mpunga, mahindi, maharage na mbogamboga. Upande wa Magharibi hutegemea zaidi Mto Pangani ambapo kuna kilimo cha umwagiliaji wa mazao ya mahindi, mpunga na mbogamboga. Upande huu ndio wenye eneo kubwa la malisho kwa upande wa ufugaji.

Mazao ya biashara yanayolimwa katika Wilaya yetu ni Tangawizi, Pamba, Fiwi na Kahawa, na Iliki. Mazao ya chakula ni pamoja na mahindi, mpunga na mtama. Mazao aina ya mikunde ni pamoja na maharage na fiwi, mazao mengine ni viazi vikuu, viazi mviringo na mihogo. Aidha Wilaya inazalisha pia aina kadhaa za mbogamboga na matunda ikiwemo ndizi, matango, tikitimaji, na nyanya.

 

Malengo ya Kilimo na Matarajio ya mavuno

Wilaya hii ni mojawapo ya Wilaya zinazokabiliwa na upungufu wa chakula mara kwa mara. Hali hii inasababishwa na mvua chache zinazosababishwa na mabadiliko ya tabia nchi ambayo huathiri ustawi wa mazao ya kilimo hasa maeneo ya tambarare.

Katika msimu wa kilimo wa mwaka 2016/2017 halmashauri ya wilaya ya same imeweka malengo ya kulima hekta 39,700 ambapo kiasi cha tani 208,297 cha mazao mbalimbali kinatarajiwa kuzalishwa, ambapo tani 155,668 ni mazao ya chakula, tani 3,289 ni mazao ya biashara, tani 26,403 ni mbogamboga, tani 7,440 ni matunda na tani 15,506 ni Viungo.

               Jedwali 6.1: Malengo ya kilimo na utekelezaji wa mazao muhimu  


2015/2016

2016/2017

LENGO

UTEKELEZAJI

LENGO

Ha

Tani

Ha

Tani

Ha

Tani

MAZAO YA CHAKULA

Mahindi

20,500

48,000

19,781

63,299

15,200

50,000

Mpunga

3,200

19,200

3,300

16,500

3,200

24,000

Mtama

500

500

100

80

500

800

Maharage

1,500

1,320

1,250

1,100

1,500

1,400

Muhogo

3,140

31,400

3,140

29,400

3,140

32,000

Ndizi

3,200

32,000

3,200

31,100

3,200

32,000

Viazi Vitamu

600

3,000

550

2,750

600

3,000

Viazi Mviringo

350

3,500

300

3,000

350

3,500

JUMLA

32,990

138,920

31,621

147,229

27,690

146,700

MAZAO YA BIASHARA

Pamba

80

120

50

60

80

120

Tangawizi

1,200

13,500

1,250

14,500

1,350

15,500

Kahawa

1,650

660

1,500

320

1,650

660

Fiwi

4,000

8,000

3,500

5,250

4,200

8000

JUMLA

6,930

22,280

6,300

20,130

7,280

24,280

                Chanzo: Idara ya Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika

6.3 Hali ya Chakula na mikakati ya kumaliza njaa

Kwa mwaka 2015/16 hali ya chakula Wilayani Same ilikuwa ya kuridhisha kutokana na mvua kunyesha kiasi cha kutosha. Kimsingi mahitaji ya chakula (nafaka) kwa mwaka ni tani 81,101 ambapo kila mtu mzima anastahili kiasi kisichopungua gunia 3 za mahindi kwa mwaka, makadirio haya ni kutokana na idadi ya watu iliyopo ndani ya Wilaya (Watu 269,807), na hii ni kwa mujibu wa Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012.  Uzalishaji wa chakula katika maeneo ya skimu za umwagiliaji za Ndungu, Maore, Kisiwani na sehemu za Kata ya Bendera nao umeongezeka kutokana na jitihada kubwa zilizofanyika za kuongeza uzalishaji katika maeneo ya umwagiliaji.

  • Mipango ya Wilaya  wa kuongeza uzalishaji na kabiliana na upungufu wa chakula
  • Kuhakikisha elimu ya uvunaji maji ya mvua, matumizi bora ya maji  na hifadhi ya ardhi na udongo imetolewa kwa wakulima.

Kutoa elimu kwa wakulima juu ya kuzuia/kupunguza upotevu wa

     mazao ya nafaka na mikunde wakati wa kuvuna na kuhifadhi   

     (Post harvest loss handling).

Kuhakikisha elimu ya ukadiriaji wa mahitaji ya mazao ya chakula kwa wakulima ngazi ya kaya imetolewa.

Kutoa elimu kwa wakulima juu ya hifadhi na matumizi bora ya mazao ya chakula kwa maeneo ambayo yamepata mavuno mazuri msimu wa vuli hasa maeneo ya kilimo cha umwagiliaji.

Kutoa ushauri kwa wakulima kutekeleza kilimo cha mazaoyanayostahimili ukame na yanayotumia kiasi kidogo cha unyevu hadi kukomaa kama  mazao jamii ya mizizi na mikunde na Mtama.

Kuhakikisha uimarishaji wa matumizi bora ya maji katika  miundombinu ya umwagiliaji iliyopo na kuhakikisha kunakuwepo na ongezeko la uzalishaji wa mazao ya chakula kwa misimu miwili na wakulima wanazingatia ushauri wa wataalam waliopo vijijini.

Kwa kuwatumia Maafisa Ugani waliopo kuhakikisha wakulima wanatumia teknolojia bora na sahihi za uzalishaji mazao ya chakula na biashara kwa ajili ya uhakika na usalama wa chakula ngazi ya kaya.

Kuhimiza wafugaji walio na mifugo kuuza wakati bado ikiwa na hali nzuri ya kiafya na kununua chakula na kuhifadhi kwa ajili ya matumizi ya familia.

Kuhimiza wakulima waliopo maeneo ya umwagiliaji kulima mazao yenye thamani na ubora kwa uhakika wa kuongeza kipato hatimaye kumudu kujinunulia chakula cha kutosha.

Kuhamasisha wafanyabiashara wenye uwezo  kununua chakula Katika maeneo yenye chakula cha ziada na kuleta kuuza katika maeneo yenye upungufu kwa bei nafuu/elekezi.

  • Mikakati ya mnyororo wa thamani wa mazao

Halmashauri ya Wilaya iliteua kuendeleza mnyororo wa thamani kwa mazao mawili ya biashara ambayo ni Tangawizi na Mpunga.

Kwa zao la tangawizi Halamashauri ikishirikia na wadau wengine imekuwa na mikakati ya kuboresha miundo mbinu ya umwagiliaji katika maeneo yanayozalisha tangawizi ili kuimarisha kilimo cha umwagiliaji kwa zao hilo. Vilevile kwa kupitia mradi wa MIVARF Halmashauri imekuwa na mikakati ya kuboresha miundo mbinu ya mawasiliano katika maeneo yanayolimwa zao hilo, pia kujengea uwezo wakulima wa tangawizi kwa kuwapa mafunzo ya kilimo bora cha tangawizi na kuwaunganisha na masoko.

Kwa zao la mpunga Halmashauri imekua na mikakati ya kuboresha miundo mbinu ya umwagiliaji katika maeneo yanayolimwa mpunga na kutoa mafunzo kwa wakulima wa mpunga kwa kuanzisha mashamba ya mfano na mashamba darasa. Aidha Halmashauri imekua na mikakati ya kufufua na kuhakikisha kinu cha kukoboa mpunga katika skimu ya Ndungu kinafanya kazi ili kuongeza thamani ya zao la mpunga.

  • Uendelezaji viwanda

6.6.1 Kiwanda cha Tangawizi

Wilaya ya Same ni miongoni mwa Wilaya zinazozalisha Tangawizi kwa wingi hapa nchini, ambapo inakadiriwa kuwa zaidi ya tani 14,500 zinazalishwa kila mwaka. Wakulima wengi hasa wa maeneo ya milimani hutegemea na kutumia zao hili kama zao la biashara. Kutokana na hali hiyo Ushirika wa wakulima wa Tangawizi Mamba Myamba uliamua kujenga kiwanda ili kuongeza thamani ya zao la Tangawizi. Kiwanda kilizinduliwa na Mhe. Rais Mstaafu mnamo mwaka 2012. Baada ya kuzinduliwa kiwanda kiliweza kusindika zaidi ya tani 100 za Tangawizi na kuziuza.

Katika uendeshaji baadhi ya mitambo ilieonekana kutofanya kazi vizuri na hivyo kuhitaji kuboreshwa. Hali hii ilipelekea kiwanda kusimama kwa muda na hivyo Shirika la SIDO wametakiwa kutengeneza na kuirekebisha mitambo hiyo.  SIDO ndio waliosanifu na kutengeneza mitambo yote ya kiwanda hicho na wanaendelea kushirikiana na ushirika pale mitambo inapoleta hitilafu.

Soko la Tangawizi mbichi na iliyosindikwa lipo la kutosha nje na ndani ya nchi. Serikali kupitia Mradi wa uboreshaji miundo mbinu ya masoko na uongezaji thamani (MIVARF) kwa kushirikiana na Shirika la Faida Mali inaendelea kusaidia ushirika huo kutafuta na kuwaunganisha na masoko ya uhakika. Tayari masoko yafuatayo yameshapatikana Kampuni ya Afri Tea, kampuni ya Tausi, TAQWA, Kampuni ya India market na Kampuni ya lion wattle.  Wanunuzi waliopatikana wapo tayari kununua tangawizi iliyosindikwa mara tu kiwanda kitakapoanza tena kufanya kazi.Kwa sasa bei ya Tangawizi ni Tshs. 1300 – 1500 kwa kilo ya tangawizi mbichi.

Zipo Changamoto za msingi zinazokabili ushirika kwa sasa, ambazo zinasababisha kiwanda kisifanye kazi vizuri. Changamoto hizo ni pamoja Uelewa mdogowa viongozi wa ushirika waliopo kwa sasa juu ya usimamizi na uendeshaji wa kiwanda, na Ukosefu wa mtaji wa kutosha kununua malighafi (Tangawizimbichi) kuajiri na kulipa watumishi na kulipia gharama za uendeshaji.

Hatua zinaendelea kuchukuliwa ili kuhakikisha kiwanda kinafanya kazi vizuri. Hatua hizo ni pamoja na Kuimarisha na kujengea uwezo viongozi wa ushirika na wanachama ili kuweza kujipanga na kuepuka bei zisizokuwa na maslahi zinazopangwa na wafanyabiashara. Aidha mafunzo yametolewa juu ya usimamizi na utunzaji wa fedha ili baada ya kuwa na uelewa wa kutosha waweze kuomba na kupata mkopo kutoka kwenye taasisi za fedha na hatimaye kuendesha kiwanda.

  •  
  •  
  •  
  •  
  •  
  •  
  •  
  •  
  •  
  •  
  •  
  •  
  •  
  •  
  •  
  •  

KITENGO CHA MALIASILI NA MAZINGIRA

  • Maliasili zilizopo Wilayani

7.1.1 Misitu Iliyopo

Wilaya ya Same ina jumla ya hakari 256,503 za misitu ambayo ni sawa na asilimia 20.3 (20.3%) ya eneo lote la Wilaya ya Same ambalo ni Kilomita za mraba 5,186 (5,186Km2). Misitu hii ni ya aina mbalimbali kama kama misitu ya Kupandwa, Mataji wazi (Miombo Woodland), Hifadhi za Serikali (Cathment Forests), Hifadhi za Vijiji na Hifadhi za kimila (Itasio).

7.1.2 Wanyamapori

Kitengo cha wanyamapori kina dhamana ya kuhifadhi rasilimali wanyamapori iliyoko kwenye maeneo ya wazi yenye wanyamapori kama vile Ruvu, kuwarudisha wanyamapori watoka nje ya na hifadhi ya taifa ya Mkomazi. Maeneo yaliyohifadhiwa yanachangia uhifadhi wa bioanuai mbalimbali ili zisitoweke kama vile tembo, nyani, kiboko, nyati, simba, mbwa mwitu pamoja na aina mbalimbali za ndege.

  • Utunzaji wa Maliasili zilizopo Wilayani

Wilaya ya Same ina jumla ya Misitu ya Hifadhi 17 ambayo kati ya misitu hiyo, Misitu minne (4) ipo chini ya Serikali kuu, Misitu tisa (9) chini ya Halmashauri na Misitu (4) ipo chini ya Vijiji.

Usimamzi wake unategemea na mmiliki ambapo Misitu ya Serikali kuu husimamiwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Misitu ya halmashauri husimiwa na Halmashauri ya Wilaya kupitia Kitengo cha Maliasili na Misitu ya Vijiji inasimamiwa na Vijiji kupitia Kamati za Maliasili za Vijiji. Misitu hii husimamiwa kupitia mipango ya usimamizi ya misitu husika ambapo shughuli za Doria, Upandaji wa Misitu, kulinda mipaka ya hifadhi na kuzuia matukio ya moto hufanyika.

Kitengo hiki kinatunza rasilimali wanyamapori kwa kuwalinda dhidi ya majangili kwa kufanya doria mara kwa mara kwenye maeneo yenye wanyamapori  ili kuwalinda dhidi na ujangili.  Rasilimali hii pia inatunzwa kwa kuhakikisha kuna udhibiti na usimamizi wa umilikaji wa nyara kama vile kutoa kibali kwenye ukamataji wa ndege kama vile kanga.

Endapo wanyamapori watatoka nje ya hifadhi ya taifa ya Mkomazi au maeneo ya wazi na kwenda kwenye makazi na mashamba ya wananchi, ni jukumu la watumishi wa kitengo cha wanyamapori kuwarudisha kwenye hifadhi.

Pia hufanyika udhibiti wa wanyamapori waharibifu hususani viboko ambao huvamia maeneo ya wananchi na wakati mwingine kusababisha vifo au madhara kwa watu na mazao mashambani kwa kuwarudisha katika makazi yao. Aidha kumekuwa pia na udhibiti wa wanyamapori kama tembo na simba wanaotoka katika hifadhi ya taifa Mkomazi. Zoezi la kuwarudisha hifadhini hufanyika haraka iwezekanavyo ili wasilete madhara kwa wananchi na mali zao. Viongozi wa kata au vijiji husika huimizwa kutoa taarifa pindi wanyamapori hao watakapoonekana katika maeneo yao. Pia elimu dhidi ya kujikinga na wanyamapori hao hatari kwa mali na uhai wa wananchi hutolewa kwa wananchi ili kuwasaidia katika kujikinga na wanyamapori hao na kutoa taarifa katika Idara ya Ardhi na Maliasili.

  • Jinsi Maliasili zilizopo Wilayani zinavyochangia Uchumi

Misitu huchangia uchumi kupitia mapato yanayokusanywa na Halmashauri ya Wilaya na Serikali kuu kutokana na tozo mbalimbali za mazao ya misitu na mazao yasiyo ya misitu lakini yanayopatikana ndani ya misitu mfani ukindu. Tozo zinazokusanywa na Halmashauri ni zile zitokanazo na mbao, nguzo za umeme, simu na za kujengea, magome ya miti na mizizi kwa ajili ya dawa mbalimbali. Tozo zinazokusanywa na Serikali kuu ni zile za Usajili wa Biashara ya mazao ya misitu, kibali cha kusafirishia mazao ya misitu (Transit Pass) na mrahaba wa mazao ya misitu yaliyovunwa katika misitu ya asili.

Rasilimali hii inachangia kwenye uchumi kwa kutoa kibali cha ukamaji wa wanyamapori kama vile ndege aina ya kanga kwenye maeneo ya wazi yanayopatikana katika ya wilaya Same. . Kibali hicho kinatolewa na Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Idara ya Wanyamapori na kuidhinishwa na Mkurugenzi wa Wanyamapori na kumtaka Afisa Wanyamapori wa wilaya kumruhusu mdau huyo kukamata wanyama walioidhinishwa. Fungu la fedha lililotokana na ukamataji wa wanyamapori hao hugawiwa kwa Halmashauri husika.

Hata hivyo  maeneo ya wazi yaliyotengwa kwa ajili ya uhifadhi kama vile Pori Tengefu (Ruvu-Same Game Controlled Area) yanakabiliwa na uharibifu mkubwa kutokana na shughuli za kibinadamu  kama vile uvamizi wa mifugo na shughuli za kilimo na ujangili kwenye maeneo yaliyohifadhiwa  hivyo kusababisha kutokuwepo na wanyama wa kutosha kwa ajili ya shughuli za uwindaji ambazo zingeweza kuiletea halmashauri pato.

  •   Upandaji wa Miti

Upandaji wa miti hufanyika kwa kuzingatia lengo la mwaka liliowekwa kwa kila Wilaya ambapo kwa Wilaya ya Same lengo la mwaka 2015/2016 lilikuwa ni kupanda miti 1,500,000.

Aidha pamoja na zoezi la upandaji wa miti, uhamaishaji wa uanzishaji wa vitalu vya miti hufanyika kwa jamii ili kupata vyanzo vya miche kwa ajili ya kupanda. Mpaka sasa jumla ya vitalu vya miti 35 vimeanzishwa na jamii katika Kata za Hedaru, Vunta, Makanya, Maore, Kisiwani, Vumari, Mtii, Bombo na Myamba. Kitalu cha Halmashauri kilichopo Mwembe kina jumla ya miti 9,780. Jumla ya miti 1,351,763 imeshapandwa mpaka sasa ndani ya Wilaya kati ya miti 1,500,000 iliyotarajiwa kupandwa kwa Mwaka 2015/2016 sawa na asilimia 90.01 (90.01%).

  •  
  •  
  •  
  •  
  •  
  •  
  •  
  •  
  •  
  •  
  •  
  •  
  •  
  •  

 

  •  
  •  

 

IDARA YA UTAWALA NA UTUMISHI/RASILIMALI WATU

  • Idadi ya Watumishi waliopo kulingana na Ikama 

 

 

 

 

 

  • Taarifa ya Watumishi Hewa

 

 

 

 

 

 

  • Kiasi cha Fedha zilizopoyea kutokana na Watumishi Hewa

 

 

 

 

 

 

 

  • Mikakati/Hatua zilizochukuliwa ili kurejesha Fedha zilizopotea kutokana na Watumishi Hewa
  •  

 

 

 

 

 

 

 

 

  • Matatizo ya Watumishi na Namna Yanavyoshughulikiwa

Tangu January 2016 hadi sasa kuna jumla ya Matatizo ya Watumishi...........yaliyoshughulikiwa na matatizo.......... yanaendelea kushughulikiwa

 

 

  • Hali ya Vikao vya Kisheria Ngazi ya Wilaya, Kata na Vijiji na Hatua za kuvisimamia

 

 

  •  
  •  
  •  
  •  
  •  
  •  
  •  
  •  
  •  
  • Hatua zinazochukuliwa kwa kutofanya Vikao

 

 

 

 

 

 

  • Motisha zilizopo kwa Watumishi/ Viongozi

 

 

 

 

 

 

 

 

  • Utowaji wa Mafunzo ya kuwajengea Uwezo Watumishi /Viongozi

 

 

 

 

 

 

 

  • Zana za Ufuatiliaji Watumishi kwa kila Idara

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

KITENGO CHA SHERIA

8.1 Idadi ya Kesi

Halmashauri  ya Wilaya ya Same kama zilivyo Taasisi nyingine za kisheria ina uwezo wa kushitaki na kushitakiwa na katika kipindi cha 2015 hadi 2016 imekuwa na mashauri mbali mbali katika Mahakama ya Wilaya, Mahakama Kuu na Baraza la Ardhi na Nyumba Same.

Katika kipindi cha 2015 hadi 2016 Halmashauri imefungua kesi mbili  moja Baraza la Ardhi na Nyumba Same ambayo ni shauri la Madai kati ya Mamlaka ya  Mji Mdogo Same dhidi ya Helios Tower Infanco Tanzania Ltd na Mahakama Kuu Moshi ya Halmashauri ya Wilaya dhidi ya Eliwaha Mbaga na Wenzake. Kesi hizi ziko katika hatua za awali.

Katika kipindi cha 2015 hadi 2016 Halmashauri  imeshitakiwa katika Mahakama ya Wilaya, Mahakama Kuu na Baraza la Ardhi na Nyumba Same na jumla ya mashauri matano(5) yalifunguliwa dhidi yake. Mashauri dhidi ya Halmashauri ni ya Eiza Mkaze dhidi ya Halmashauri na Mwingine, Ramadhani Kanyama Msuya dhidi ya Halmashauri, Christina Elieskia na Miriam Kajiru dhidi ya Mkutugenzi Mtendaji Wilaya, Cheavo Johnson Kihara dhidi ya TANESCO na Halmashauri ya Wilaya na Octavius Leole dhidi ya Halmashauri ya Wilaya. Kesi hizi bado ziko kwenye hatua mbalambali za usikilizwaji na ya Christina na mwenzake imeamuliwa kwa njia ya usulihishi CMA na imerudishwa TSC kwa hatua zaidi

  • Mikakati ya kushinda Kesi na kuhakikisha Mikataba inakuwa na Tija kwa Halmashauri na Serikali

Halmashauri ya Wilaya ya Same kupitia Kitengo cha Sheria imejipanga kushinda katika kesi zote kwa kuhudhuria Mahakamani kufuatana na kalenda za Mahakama na kutoa ushahidi thabiti kwa mujibu wa sheria pia kushawishi utatuzi wa migogoro nje ya mahakama pale inapobidi kufanya hivyo ili kuepuka upotevu wa muda na rasilimali fedha.

Kitengo cha Sheria kinashughulika na uandaaji wa mikataba mbalimbali baina ya Halmashauri na wadau wake na vilavile kuandaa mikataba ya watumishi walioruhusiwa kwenda masomoni.

Katika hili Kitengo kinazingatia kanuni,taratibu na sheria za mikataba ili kuhakikisha kwamba mikataba yote inayiongiwa na Halmashauri ina tija kwa Serikali,wananchi na Halmashauri kwa ujumla.

  • Sheria Ndogondogo

Katika kipindi cha 2015 hadi 2016  Halmashauri kupitia Kitengo cha Sheria imeweza kuanda Sheria Ndogo 7 zitakazo saidia utekelezaji wa majukumu ya Halmashauri katika kuhudumia wananchi wa Wilaya ya Same. Sheria hizo ni Sheria Ndogo za Ushuru wa Mabasi Stendi, Sheria Ndogo ya Kudhibiti Unywaji Holela wa Vileo, Sheria Ndogo za Ushuru wa Pumba za Nafaka, Sheria Ndogo ya Kilimo cha Mazao yanayohimili Ukame, Sheria Ndogo ya Mahudhurio ya Lazima kwa Shule za Msingi na Sekondari, Sheria Ndogo za Ushuru wa Nyumba za Kulala Wageni na Sheria Ndogo ya Kuzuia Ujazaji wa Lumbesa. 

Katika kuhakikisha kwamba tunakuwa na jamii ya watu walio sawa na huru, Halmashauri ya Wilaya ya Same inashirikiana na Taasisi zisizo za kiserikali katika kutoa msaada wa kisheria kwa makundi mbalimbali ya kijamii katika wilaya ya Same.

IDARA YA MAENDELEO YA JAMII

  • Mambo ya kufanya ili kuhakikisha Jamii inapata Maendeleo

Kinachofanyika na kinachotarajiwa kufanyika ili kuhakikisha jamii inapata maendeleo ni;

  1. Kuhamasisha jamii jamii  kushiriki katika kazi za maendeleo za kujitegemea kama (misaragambo) ,katika  ujenzi  wa barabara, ofisi za kata,zahanati, shule za msingi na sekondari,  uchangiaji wa madawati, na kujiunga katika vikundi.
  2. Kuhamasisha jamii kutumia teknolojia raisi katika ujenzi wa nyumba bora na salama  zenye gharama nafuu, kwa kutumia   matofali fungamano.
  3. Kuijengea jamii elimu ya ufahamu juu dhidi ya   mila potofu kama vile, Ukeketaji, ndoa za utotoni, kulazimisha kurithi wajane na zinginezo.
  4. Kutoa elimu ya  ufahamu  kwa jamii  kuepuka maambukizi  mapya  ya VVU na UKIMWI, Kuacha  ngono zembe  matumizi sahii  ya kondomu, dawa za ARV.
  5. Kuhamasisha jamii juu kupinga unyasasaji wa kijinsia, kama vipigo, matusi, dharau na aina yoyote ya unyanyasaji.
  6. Kutoa elimu ya ufahamu kwa wazazi, walezi na jamii kwa jumla kuwapa fursa sawa watoto wa jinsi katika kuwapa elimu na kujiendeleza.
  7. Kutoa elimu ya ufahamu kwa wazazi, walezi,  juu ya kutumikishwa  kwa watoto, kuwafanyisha kazi ngumu zilizozidi uwezo wao
  8. Kuhamasisha jamii kuwa na uelewa wa kupinga matumizi mabaya ya madawa ya kulevya kama vile uvutaji bangi,na ulaji wa mirungi.
  9. Kutoa elimu kwa jamii juu ya malezi bora kwa vijana ili kuepusha ongezeko la makundi tete.
  10. Kushirkiana na watoan huduma za kiroho, lil kutoa huduma kwa makundi ya rika zote katika kuepusha  kusitokee au kupunguza makosa ya jinai
  11. Kuhamasisha jamii ili kujiunga katika vikundi kwa ajili ya kupatiwa mafunzo ya ujasiriamali.
  12. Kuhasisha jamii ili kujiunga na vikundi vidogo vidogo vya kuweka na kukopa vijulikanavyo kama VICOBA.
  13. Kuhamasisha jamii ya makundi ya vijana na wanawake kujiunga katika vikundi vya ujasiriamali kwa ajili ya kupatiwa mikopo yenye mashariti nafuu.
  14. Kutoa elimu kwa jamii juu ya upimaji wa maeneo yao kwa ajili ya matumizi bora yan ardhi na mipango miji, ili kuepusha migogoro.
  15. Kuhamasisha wananchi juu Usafi wa mazingira, ujenzi wa vyoo bora na matumizi yake ili kupusha magonjwa ya milipuka.
  • Idadi ya Vikundi vyenye Nguvu

Idadi ya vikundi vilivyopata usajili na vyenye nguvu ya kuweza kupata mikopon katika taasisi za kifedha ni kama ilivyoanishwa hapa chini;

Jedwali 5.1 Idadi ya Vikundi vyenye Nguvu

AINA YA KIKUNDI

VIKUNDI VYA VIJANA

VIKUDI VYA WANAWAKE

VIKUNDI VYA WAJASIRIAMALI

IDADI

387

678

475

 

  Chanzo: Idara ya Maendeleo ya Jamii

 

Jedwali 5.2: Idadi ya Vijana wasio na Kazi Maalum

WANAWAKE

WANAUME

JUMA YA VIJANA WASIOKUWA NAKAZI

246

223

469

Chanzo: Idara ya Maendeleo ya Jamii

 

 

 

  • Mikakati ya Kuwaendeleza Vijana

Kuwahamasisha vijana   ili waweze kujiunga na masomo ya ufundi stadi kv   uashi useremala na ujenzi ili waweze kujiajiri

Kwahamasisha vijana kujiunga kwenye vikundi ili wapatiwe mkopo yenye mashariti nafuu

Kuwahamasisha vijana ili wajiunge kwenye makundi kwa ajili ya kupatiwa elimu juu ya ujasiriamali

Kuwatengea vijana maeneo maalum kwa ajili ya kufanyia biashara ndogo ndogo

Kuwahamasisha vijana kutumia elimu mbalimbali katika kuanzisha ufugaji wa kuku na  n g”ombe wa maziwa na nyama

Kuhamasiha vijana ili waweze kuanzisha viwanda vidovidogo kv, useremala uashi na ufndi vyuma.

  • Idadi ya SACCOS/Vikoba

Idadi ya SACCOS na Vikoba ni kama ifuatavyo;

Jedwali 5.3: Idadi ya SACCOS/Vikoba

S/N

JINA LA SACCOS

KATA/ENEO

MMILIKI

1

SAME KAYA SACCOS

WILAYA

WANANCHI/WANACHAMA

2

SAME TEACHERS SACCOS

WILAYA

WAALIMU WANACHAMA

3

KISIWANI SACCOS

KISIWANI

WANACHAMA

4

MKONAPA SACCOS

VUMARI

WAFANYAKAZI/WANACHAMA

5

NASHENGENA SACCOS

MAORE

WANACHAMA.

6

KURUGENZI SACCOS

WILAYA

WAFANYAKAZI

7

MARANATHA SACCOS

SAME

WAUMINI WASABATO

8

GAHENDU

SAWENI

WANACHAMA WA GAVAO, HEDARU, GUNDU.

Chanzo: Idara ya Maendeleo ya Jamii

 

  • Fedha za Vikundi toka Halmashauri katika bajeti ya 2015/2016 zilizopangwa, Kiasi cha Fedha kilichotolewa na Idadi ya Vikundi vilivyopewa

Fedha zilizopangwa kutolewa na Halimashauri kwa kipindi cha 2015/16 ni jumla ya TShs. 112,000,000/=  na zilizotolewa ni Tshs. 26,000,000/= na idadi ya vikundi vilivyopatiwa mikopo ni 14.

  • Fedha zilizopangwa katika Bajeti ya 2016/2017

Kwa upande wa Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2016/2017, Fedha zilipangwa kutolewa kwa kipindi cha 2016/17 ni Tsh. 146,000,000/=

KITENGO CHA UKAGUZI WA NDANI

  • Idadi ya Hoja za Ukaguzi

Kwa kipindi kinachoishia mwezi Agosti, 2016, Halmashauri ilikuwa na hoja za ukaguzi 54 zinazohitaji majibu yatakayopelekea hoja hizo kufungwa.

  • Mikakati ya kupunguza Hoja za Ukaguzi

Uongozi wa halmashauri umeweka mikakati ili kupunguza hoja za ukaguzi, mikakati hiyo ni:-

Kutumia mashine za elektroniki zinazowasiliana na makao makuu ya halmashauri kukusanyia mapato toka katika Kata, itasaidia kuhakikisha mapato yote yaliyokusanywa kufahamika na kuwasilishwa na kuondoa tatizo la upotevu/kutokuwasilishwa  wa vitabu vya kukusanyia mapato

Kuendelea kuwasiliana na TAMISEMI , ili kuweza kupata wakuu wa Idara/au kuwathibitisha makaimu wakuu wa idara waliopo, hii itasaidia kupunguza madeni kwa wakuu wa idara wanaokaimu kwa muda mrefu

Kuendelea kufuatilia uwepo wa watumishi hewa  kwa kufanya uhakiki wa watumishi kila mwezi

Kuongeza juhudi katika ukusanyaji wa mapato ya ndani na kuibua vyanzo vipya vya mapato ya ndani , na kuendelea kuwasiliana na Hazina /Serikali kuu ili iweze kuleta fedha kwa wakati kulingana na bajeti , hii itasaidia halmashauri kutekeleza kazi kulingana na bajeti na kuwa na uwezo wa kupeleka asilimia 10 ya mapato ya ndani yaliyokusanywa katika mfuko wa wanawake na vijana

Kuendelea kufuatilia fedha za miradi  ya maendeleo ambazo hazijawasilishwa toka Hazina na kuomba fedha hizo kuwasilishwa kwa wakati

Kutenganisha thamani ya majengo na ardhi kwa kufanya uthaminishaji

Kuwaelekeza wakuu wa Idara/vitengo/watumishi kutekeleza majukumu kwa kufuata taratibu na sheria

Kuimarisha mifumo ya udhibiti wa ndani katika usimamizi wa fedha/manunuzi/ubora

Kuhakikisha utekelezaji wa miradi unafanyika mapema mara fedha zinapowasili

Kuimarisha Kitengo cha ukaguzi wa ndani kwa kuwajengea uwezo katika mifumo, mfano, mfumo wa ukusanyaji wa mapato kielektronic, LAWSON, EPICOR, PLAN REP.

  • Changamoto zinazosababisha kutokuisha kwa Hoja za Ukaguzi

Upungufu wa mkaguzi mmoja kulingana na Ikama

Kukosekana/kutokuwasilishwa kwa fedha , kumepelekea kaguzi kutofanyika kulingana na mpango wa ukaguzi wa mwaka

Wakaguzi kutokujengewa uwezo kuhusiana na mifumo ya ukusanyaji wa mapato kielektronic, LAWSON, EPICOR, PLAN REP

IDARA YA UJENZI

  • Idadi ya Miradi inayoendelea kutekelezwa

Katika mwaka wa fedha 2015/2016 idara ya ujenzi ilitengewa  kiasi cha Tshs 956,160, 000/= kutoka mfuko wa barabara (Road fund) hadi kufikia 30/06/2016 halmashauri imepokea kiasi cha Tsh 215,460, 000/= tu. Miradi inayoendelea kutekelezwa kwa kazi za barabara ni kama ifuatavyo:-

Jedwali 11.1: Idadi ya Miradi inayoendelea kutekelezwa

Na.

Jina la mradi

Jina la Mkandarasi

Gharama ya Mkataba

Maoni

1

Matengenezo ya kawaida na muda maalumu barabara za Makanya – Chankoko na Njia panda – Chankoko - Mvungwe

 OLDONYOMAS ENGINEERING

105,577,550

Kazi zinaendelea

2.

Matengenezo ya kawaida muda maalumu na miundo mbinu ya maji barabara za Mpirani -Kadando,Maore- Vuje,Ndungu-Makokane na Mpirani-Bombo

CORNEL (T) LTD

88,030,950

Kazi zinaendelea

3.

Matengenezo ya kawaida, sehemu korofi na matengenezo ya muda maalumu barabara za Same -Ruvu-Mferejini na Ishinde-Vumari.

CORNEL (T) LTD

77,881,180

Kazi zinaendelea

4.

Matengenezo ya kawaida,sehemu korofi  na miundombinu ya maji ya mvua barabara za Kisiwani -Msindo,Mwembe- Mhezi,Mbuyuni-Marindi na  Ijinyu - Kamadufa

MUGENZO CO. LTD

 

64,431,540

Kazi zinaendelea

5.

Matengenezo ya kawaida na sehemu korofi barabara za  Saweni-Gavao -Bwambo,Kidenge- Mwala na  Hedaru- Makasa-Kirangare

 

HAMORIC INVESTMENT (T) LTD

34,499,660

Kazi zinaendelea

6

Matengenezo ya kawaida na miundombinu ya maji barabara za Majevu-Dido- Njoro, Minyala -Mbono-Mgagao na dengude- Dido.

KIV CO.LTD

70,825,960

Kazi zinaendelea

7

Matengenezo ya kawaida muda maalumu na miundo mbinu ya maji barabara za Same Mjini.

SIMJO TECH CO.LTD

128,118,500

Kazi zinaendelea

8

Matengenezo ya kawaida na sehemu korofi barabara za  Bangalala -Chome na Chome - Ikokoa

MSHUNGA INVESTMENT LTD

22,774,000

Kazi zinaendelea

Chanzo: Idara ya Ujenzi

 

11.2 Ubora wa Miradi inayotekelezwa.

Miradi inayotekelezwa ipo katika ubora unaotakiwa kwa kuzingatia taratibu za mikataba.

  •  Uhakiki kwa Wakandarasi wanaopatiwa Kazi/Tenda

Uhakiki wa wakandarasi wanaopatiwa kazi/tenda hufanyika kipindi cha kufanyiwa uchambuzi wa zabuni (Tender evaluation) wa wazabuni wanapoomba tenda/zabuni.

IDARA YA FEDHA

12.1 Utangulizi

Halmashauri ya Wilaya ya Same kwa mwaka wa fedha 2015/2016 iliidhinishiwa  kupokea fedha  Tshs. 43,351,398,248  hadi kufikia Juni 2016 ilikuwa imepokea Tshs. 41,467,376,632  sawa na asilimia 95.

Jedwali hapo chini linaonyesha vyanzo vya Halmashauri, Makadirio, hali halisi, asilimia, utekelezaji na changamoto zilizojitokeza wakati wa utekelezaji wa bajeti hiyo kama ifuatavyo:-

Jedwali 12.I: Bajeti ya Halmashauri 2015/2016

Na.

Vyanzo vya Halmashauri

Makadirio

Hali halisi ya makusanyo  ya Fedha

Asilimia

Utekelezaji

Changamoto

1.

Vyanzo vya ndani

2,274,732,000

1,933,320,538

85

Fedha za mapato  ya ndani zimechangia miradi ya maendeleo;-

Mchango wa madawati Tshs. 212,021,051

Kuchangia ukamilishaji wa ujenzi wa maabara na ununuzi wa vifaa vya maabara Tshs. 37,810,000

Kuwezesha unununzi wa kipaza sauti ukumbi wa Halmashauri Tshs.

4,613,400

Ukamilishaji wa kituo cha kilimo Tshs. 5,600,000

Kuchangia ujenzi wa ofisi mpya ya Mkurugenzi Tshs. 30,000,000

Kuchangia ukarabati wa shule za msingi  Tshs. 10,000,000

Kufunga mfumo wa kieletronic Tshs. 75,417,808

Kuchangia mfuko wanawake na Vijana Tshs. 22,150,360 na

Uendeshaji wa shughuli za ofisi vikao na ulipaji wa mishahara kwa watumish wanaolipwa na mapato ya ndani.

-Mwamko mdogo wa wananchi kulipa kodi na ushuru.

-Baadhi ya Vijiji kutokuwa na Maafisa watendaji Vijiji.

-Shughuli za uchaguzi Mkuu

-Mabasi kutoingia stand.

2.

Fidia ya vyanzo vilivyofutwa

          200,023,000

     31,977,000

16

Shughuli za uendeshaji wa ofisi zilifanyika kulingana na fedha iliyotolewa.

Fedha kuto kutolewa kulingana na Bajeti.

3.

Serikali kuu - Ruzuku – OC

  2,327,258,000

1,769,377,000

76

Idara ilitekeleza shughuli zilizopangwa kutokana na fedha zilizopokelewa

Fedha kutopokelewa kwa wakati.

Fedha kuto kutolewa kulingana na Bajeti.

4.

Mishahara

32,612,236,000

31,899,123,217

98

Mishahara ililipwa kwa Watumishi kwa wakati

Madeni ya Malimbikizo  ya mapunjo ya mishahara.

5.

Miradi ya maendeleo.

  • Serikali   Kuu
  • Wafadhili

EGPAF

EASTERN ARC

MIVAF

TANAPA

Performance For Result (P4R)

Ujenzi / Uboreshaji Miundombinu- Kibacha

TASAF

   3,177,944,465

  

239,474,300

 

 15,400,000 21,300,000

 

18,000,000

     72,377,209

  

221,902,836

  

2,170,750,438

    3,147,136,623

    

166,711,771

   

15,400,000

21,300,000

 

18,000,000

   72,377,209   

   

     221,902,836

 

 2,170,750,438

99

70

100

100

100

100

100

100

Utekelezaji wa miradi umefanyika kulingana na fedha iliyotolewa na lengo lililokusudiwa

Kuchelewa kupokea fedha kwa wakati.

 

Jumla                          

43,351,398,248      

41,467,376,632       

95

 

 

                        

 

 

 

Jedwali 12.2: Bajeti ya Halmashauri 2016/2017

Vyanvo

Makadirio

Mikakati ya kufikia malengo

Vyanzo vya ndani

                 

    2,335,264,000

Kuhakikisha Takwimu na Bajeti za Mapato zinaandaliwa kutoka kwenye kila Kijiji pia itawezesha Kijiji kuwa na makadirio ya asilimia 20 itakayorejeshwa Kijijini.

Kuhakikisha kila Kijiji kinakuwa na malengo ya kukusanya mapato

Kuhakikisha kila Kata inakuwa na machine ya kukusanyia mapato.

Kuhakikisha kuna kuwa na ufatiliaji wa mara kwa mara  wa mapato na ufatiliaji wa kushtukiza

Kubuni vyanzo vipya vya mapato

Kuendelea kutoa  elimu  kwa walipa kodi na ushuru ili waweze kuelewa umuhimu wa kulipa kodi na ushuru.

Kuendelea kufatilia mikakati iliyowekwa na kufanya tathmini..

Fidia ya vyanzo vilivyofutwa

        192,362,000


Serikali kuu - Ruzuku – OC

      

     3,245,916,850


Mishahara

   39,475,823,940


Miradi ya maendeleo

   11,251,205,280


JUMLA

   56,500,572,071

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 


12.2 Halmashauri inakusanya mapato Kwa njia ya kieletroniki Na kupitia mfumo WA LGRCIS ambao umeunganishwa na NMB 

Halmashauri ilianza kutumia mashine ya kukusanyia mapato ngazi ya Kata, mwezi Julai 2016.  Tumeshanunua mashine 35 kwa sasa  Kata zinazotumia  mashine  ni Kata 17  nazo ni Mamlaka ya Mji mdogo kata 3, Hedaru, Makanya, Njoro, Bendera, Kihurio, Ndungu, Maore, Kisiwani,  Ruvu ,Vumari, Kalemawe, Bwambo, Myamba na Mpinji  Sambamba na ilo tumeshanunua Mashine zingine 30 za kukusanyia mpato.

12.3 Vyanzo Vipya Vya Mapato

Halmashauri imeanza mpango wa kuanzisha soko la mazao katika Kata ya  Ruvu ambalo litawezesha  Halmashauri kukusanya  ushuru wa mazao, tayari timu ya Wilaya imeshakutana na serikali ya Kijiji kwa ajili ya kuwashirikisha  kupata eneo sahihi.

Halmashauri imeanza  mpango wa kuanzisha  mnada wa mifugo Kata ya Njoro  siku ya Alhamisi  na Same  siku ya Jumapili.

12.4 Kudhibiti Wizi /Upotevu

Halmashauri imeweka utaratibu wa kuwasilisha mapato mara mbili kwa Mwezi na ukaguzi wa nyaraka za fedha unafanyika kila baada ya miezi mitatu kwa kushirikisha Kitengo cha Ukaguzi wa ndani.

12.5 Ufanisi wa Malipo

Halmashauri inafanya malipo yote  kupitia mfumo wa malipo wa EPICOR, mfumo huu unategemea uwepo wa fedha kwenye  kasma na kifungu  husika, hivyo kasma  na kifungu vinapokuwa na fedha malipo huchukua siku 3 mhusika kulipwa. Iwapo madai yanafika ofisini pasipo kuwa na fedha mhusika hufahamishwa kwa barua kusubiri mpaka hapo itakapopatikana.


IDARA YA MIPANGO, TAKWIMU NA UFUATILIAJI

  • Mipango kiidara

Mipango kiidara ipo, na idara hii ndiyo yenye jukumu la kuunganisha Mipango na shughuli za Idara mbalimbali kupitia mfumo ujulikanao kama Medium Term Expenditure Framework (MTEF). Miradi yote ya kila Idara ngazi ya Kata na Vijiji pamoja na miradi ngazi ya Wilaya huunganishwa na kuratibiwa na Idara hii, ili kuleta ufanisi wa utoaji huduma kwa jamii.

  • Mpango Mkakati/ Strategic Plan

Idara ya Mipango Takwimu na Ufuatiliaji pia ina jukumu la Kuratibu na kusimamia uandaaji wa Mpango Mkakati wa miaka mitano wa     Halmashauri (Strategic Plan). Zoezi hili hufanyika kila baada ya Miaka mitano katika Halmashauri, ambapo Idara inaanda Mpango Mkakati mpya au kuhuisha Mpango Mkakati uliopo. Hadi sasa Idara bado ipo kwenye mchakato wa kuhuisha Mpango Mkakati  wa Halmashauri ambapo mda sio mrefu zoezi hili litakamilika.

  • Hali ya Pato la Mwananchi kwa sasa (GDP)

Pato la Mwananchi (GDP) ni jambo muhimu sana la kuzingatia ili kupima halihalisi ya uchumi kwa kila Mwananchi katika Jamii. Hali ya Pato la Mwananchi katika Halmashauri ya Wilaya ya Same ni Shilingi 720,000/=

  • Uwepo wa Takwimu zinazosaidia Idara kupanga na kufanya Maamuzi

Katika Halmashauri ya Wilaya, Takwimu zote za Kiuchumi na Kijamii zipo na zinatumika ipasavyo katika utekelezaji shughululi mbalimbali za maendeleo. Takwimu kama vile Idadi ya Watu ndizo tunazozitumia sana katika utekelezaji wa shughuli za Miradi ya maendeleo. Takwimu zingine ni za sekta mbalimbali kama vile Takwimu za Elimu, Afya, Kilimo, Mifugo na zingine mbalimbali.

  • Usambazaji wa Takwimu sahihi kwa Matumizi

Hali ya usambazaji wa Takwimu katika Halmashauri ya Wilaya ya Same ni ya kuridhisha, kwani Takwimu hizi zinasambazwa pale zinapohitajika na kwa wakati.

  • Ufuatiliaji wa Utekelezaji wa Kazi za Miradi

Idara hii pia ina jukumu la kufanya ufuatiliaji kwa kina juu ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali za Miradi ya Maendeleo pamoja Kuratibu, kusimamia, kutathmini na kufanya uhakiki wa programu za maendeleo ya Halmashauri. Ufuatliaji wa utekelezaji wa shughuli za Miradi inayotekelezwa Vijijini sio ya kuridhisha sana ukilinganisha na miaka iliyopita. Hali ya ufuatiliaji wa Miradi inaathiriwa na uhaba wa Fedha hasa baada ya Kifungu cha Monitoring and Evaluation katika Bajeti ya Ruzuku ya Miradi ya Maendeleo (LGCDG) kufutwa. Idara imekuwa ikipata changamoto sana juu ya ufuatiliaji wa Miradi ya Maendeleo katika Halmashauri. Idara imejitahidi na inaendelea kujitahidi sana kufuatilia miradi ya maendeleo katika Halmashauri kwa kuomba Fedha kutoka kwenye Mfuko Mkuu (GF). Pia ili kuendelea kusimamia ufanisi wa miradi inayotekelezwa, Idara inawatumia Watendaji wa Kata na Vijiji kwa kufanya mawasiliano ya karibu sana kipindi miradi inatekelezwa jambo ambalo linasaidia pia katika ufanisi wa Miradi ya Maendeleo.

  • Mfumo wa kuhakikisha Utekelezaji wa Shughuli za Miradi na  Idara

Pamoja na majukumu mengine Idara hii inatumia Mfumo wa kuhakikisha Utekelezaji wa Shughuli za Miradi ndani ya Idara na nje ya Idara. Maelekezo na miongozo hutolewa kutoka kwenye Ofisi ya Mkurugenzi na kuletwa ndani ya Idara. Idara hii inasimamia Mipango yote ya shughuli mbalimbali ndani na nje ya Idara. Idara zote huandaa Mipango yao na kazi kubwa ya Idara hii ni Kuratibu na kusimamia mchakato wa Mipango shirikishi na uandaaji wa bajeti ya Halmashauri. Mipango hii ya Halmashauri kiidara huunganishwa katika mfumo mmoja ujulikanao kama Medium Term Expenditure Framework (MTEF). Pia Idara hii inafanya kazi za Kuratibu mchakato wa menejiment ya Takwimu mbalimbali za Halmashauri na kupendekeza sera na mipango inayohitajika. Kazi nyingine ya Idara hii ni Kufanya makisio ya idadi ya watu ya Wilaya (Population Projection) kwa kila mwaka ambapo zoezi hili ni muhimu sana kwani husaidia katika swala zima la uandaaji wa Maoteo [Indicative Planning Figure (IPF)] wakati wa kipindi cha mchakato wa uandaaji wa Mpango na Bajeti. Yote hii ni kuhakikisha kunakuwa na usawa katika ugawaji wa huduma za kiuchumi na kijamii pamoja na Maendeleo kwa ujumla.

  • Dira, Dhima, Desturi na Namna ya Kuzimiliki

Halmashauri ya Wilaya ina Dira, Dhima na Desturi kama ifuatavyo;

Dira: Kuwa na Jamii yenye Maisha bora, iliyohamasika na kuendana na mabadiliko endelevu ya Maendeleo ya Kiuchumi na Kijamii ifikapo mwaka 2016.

Dhima: Kutoa Huduma bora kwa Jamii kupitia matumizi sahihi ya Rasilimali, kuwajengea uwezo, Utawala bora na kuwa na Maisha bora.

Desturi: Kutoa huduma kwa Jamii kwa kutumia mbinu shirikishi (Participatory Approach) ili kuleta ufanisi wa huduma ya utawala bora na Huduma kwa Jamii. Idara ina uhuru wa kumiliki desturi yake ya kutoa huduma katiaka jamii kwa kushirikisha Idara zote na Vitengo katiaka Halmashauri pamoja na ngazi za Kata na Vijiji. Idara inaendelea kufanya shughuli zake kwa kufuata desturi yake ya ushirikishwaji wa jamii.

KITENGO CHA MANUNUZI

  • Ufanisi wa Idara

Kitengo cha manunuzi ni miongoni mwa kitengo (6) vilicho chini ya Mkurugenzi Mtendaji, aidha   Majukumu ya kitengo cha manunuzi ni kama ifuatavyo;-

Kusimamia shughuli zote za manunuzi

Kutekeleza maagizo ya Bodi ya zabuni

Sekretarieti ya bodi ya zabuni

Kupanga manunuzi na mpango wa kuuza mali za serikali

Kupendekeza manunuzi njia ya manunuzi na kuuza mali za serikali kwa njia ya zabuni

Kuandaa mahitaji mahitaji taarifa ya mahitaji

Kuandaa kabrasha za  Zabuni

Kuandaa matangazo ya Zabuni

Kuandaa Mikataba ya Zabuni

Kutoa Mikataba iliyo idhinishwa

  • Idadi ya Kazi zilizotangazwa, zilizoleta Migogoro na zenye Kesi

Kwa kipindi cha Mwaka 2015/2016 zabuni zilizo tangazwa ni kama ifuatavyo;

Ujenzi wa barabara  zabuni zilizo tangazwa ni 9

Ujenzi wa majengo zabuni zilizotangazwa ni 7

Idadi ya wa tumishi katika kitengo ni 4

Upungufu uliopo ni 1

Kwa upande wa Kazi zilizotangazwa hakuna kazi zozote zenye migogoro na Kesi katika Halmashauri yetu.

 

14.3 Changamoto

Sheria ya Ununuzi Umma Kurefusha mchakato wa Manunuzi  kwa serikaliza Mitaa

Upungufu wa Mtumishi (1) katika kitengo cha Manunuzi

Uelewa Mdogo wa sheria kwa  baadhi ya Idara  tumizi (User departiments)

14.4 Mikakati

Kushauri wakuu wa Idara na vitengo Kuanzisha michakato ya manunuzi kwa wakati

Tayari Kitengo kilisha omba kibali cha kupatiwa Mtumishi mmoja.

Tayari kitengo cha Manunuzi kimefanya mafunzo kwa wakuuu wa idara na vitengo na kinaendelea

KITENGO CHA TEHAMA

  • Kuwa na Tovuti iliyo huishwa (Hosting) ambayo itakuwa inatoa taarifa za Wilaya kwa wakati na ueledi.Touvti iyo ni www.samedc.go.tz kwa sasa tovuti iyo ipo hewani na inatoa taarifa za Wilaya kwa wakati.

    Kusimamia taasisi zote za Serikali zilizopo ndani ya Wilaya kuwa na matumizi sahihi na bora ya TEHAMA.mfano huduma ya mtandao (internet).

    Kutumia baadhi ya miundo mbinu ya TEHAMA kwaajili ya kutumika kama vyanzo vya mapato ndani ya Halmashauri mfano Internet Café,

    Kufuatilia,kusimamia na kujua gharama za uendeshaji na uanzishwaji wa Gazeti au makala ya Wilaya kiujuma.

    Kufuatilia,kusimamia na kujua gharama za uendeshaji na uanzishwaji wa Redio ya Wilaya

    • Mipango ya uimarishaji wa Mawasiliano kati ya Halmashauri na Wananchi ndani ya Halmashauri.
  • Ifuatayo ni Mipango ya uhimarisha wa mawasiliano kati jamii na halmashauri:-

    • Kuwajengea uelewa wa Matumizi ya sahihi ya mawasiliano mbalimbali mfano simu na  huduma ya internet.
    • Kuhakikisha kila kata katika Wilaya ya Same inakuwa na Huduma ya Mawasiliano ya Simu, mfano Vodacom,Tigo ,Airtel na Halotel.Kata ya Vumari ndio pekee ilikuwa imebakia lakini kwa sasa kampuni ya Vietnam (Halotel) wameshafikisha huduma iyo.
    • Kujaribu kuanisha maeneo mbalimbali ya uwekezaji wa miundo mbinu mbali mbali ya mawasiliano.

    • Mipango ya Kuitangaza Wilaya kwa Wananchi wa Same, Nje ya Same na Nje ya Nchi
    • Kuanzisha gazeti/jarida ambalo litaeleza shughuli mbalimbali zinazofanywa na halmashauri ya wilaya ya Same.Gazeti hilo tayari lipo kwenye mchakato nimewasilisha maelezo husika kwa Mkurugenzi Mtendaji.
    • Kuanzisha redio ya halmashauri ya Wilaya ya Same.Kuanzisha redio kunahitaji vitu vifuatavyo;
    • Ofisi/sehemu maalum kwa ajili ya studio
    • Kuandika barua ya maombi kwaTCRA ili tupate kibali maalum cha kuanzisha redio na kurusha matangazo.
    • Vifaa vya studio ikiwemo mitambo ya kisasa (digital machines) ya kurushia matangazo. 
    • Mzabuni kwa ajili ya kutengeneza studio kwa shughuli za redio
    • Kuendelea kujenga mahusiano mazuri na vyombo vya habari ili kuleta urahisi wa kupenyeza taarifa chanya za Halmashauri ya Wilaya. Mfano mpaka sasa tuna mahusiano mazuri na vyombo mbalimbali ambavyo taarifa zetu zinatoka mara kwa mara vyombo kama gazeti la majira na TBC.
    • Kuanza kutumia Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya kuweka taarifa mbalimbali pamoja na matangazo mbalimbali ya tender na maonyesho yenye tija kwa Wilaya nzima.
    • Kuboresha page ya facebook ya Halmashauri ya Wilaya pamoja na Blog
    • Kuunda group la whatup kwa baadhi ya watumishi watakaoweza kuunganishwa kulingana na uwezo wa simu zao ili wapate taarifa kwa wakati zaidi.
    • Kuboresha Mifumo ya ufuatiliaji kwa kutumia Tehama
  • Kama ilivyo katika Halmashauri nyingine,Halmashauri ya Wilaya ya Same inayo mifumo ambayo inayotumia katika kutekeleza majuku ya kila siku,mifumo ni EPICOR-FEDHA, LAWSON- UTUMISHI, PSSN-TASAF,TOMSHA-TACAIDS, BEMIS-ELIMU MSINGI/SEKONDARI, LGRCIS- UKUSANYAJI WA MAPATO na LMS- ARDHI.

    Mifumo yote iyo kimsingi imeboreshwa na ufuatiliaji wake upo vizuri kwani kila wakati imekuwa ikitumika bila ya Tatizo lolote,kwa kushirikiana na TAMISEMI.Pamoja na ayo yote changamoto kubwa iliyopo ndani ya Kitengo cha TEHAMA ni ufinyu wa Bajeti hivyo baadhi ya shughuli zimekuwa ngumu kutekelezeka kabisa.

    • IDARA YA MIFUGO NA UVUVI
    • Idadi Ya Mifugo
  • Wilaya ya same ina kanda tatu za ufugaji wa mifugo ambazo ni ukanda wa juu (Milimani), ukanda wa kati na ukanda wa tambarare (Magharibi na Mashariki). Ukanda wa milimani mifugo hufugwa na kulishwa ndani (zero grazing and tethering) kanda zinazobaki yaani ukanda wa kati na tambarare mifugo hufugwa huria (free range) kwa mifugo asili na kufugwa/kulishwa ndani (zero grazing and tethering) kwa mifugo chotara.

    Eneo kubwa la malisho kwa ukanda wa tambarare ya Mashariki limepakana na Mbuga ya Taifa ya Mkomazi na ukanda wa tambarare ya Magharibi malisho haya yamepakana na mto Pangani. Wilaya ya Same ina mifugo mingi kuliko wilaya zote za mkoa wa Kilimanjaro. Eneo la malisho (Range land) lililoainishwa lina ukubwa wa hekta 356,200 ambazo ni asilimia 67.25 ya eneo lote la wilaya. Idadi ya mifugo wilayani ni kama inavyoonekana katika jedwali hapa chini;

     

     

    Jedwali 16.1: Aina na Idadi ya Mifugo inayofugwa Wilayani

    AINA YA MIFUGO

    IDADI YA MIFUGO

    JULMA YA MIFUGO

    ASILI

    CHOTARA

    Ng’ombe

    176,484

     7,896

    184,380

    Mbuzi

    112,427

     478

    112,905

    Kuku

    210,839

     20,921

    231,760

    Kondoo

    70,903

    70,903

    Punda

    6,426

    6,426

    Nguruwe

    2,811

    2,811

    Ngamia

    18

    18

    Bata

    9,990

    9,990

     Mbwa

    8,796

    8,796

    Chanzo: Idara ya Mifugo na Uvuvi 

    • Aina ya Ufugaji na Mikakati ya Kufuga Kisasa
  • Katika halmashauri ya wilaya ya Same, kuna aina kuu tatu za ufugaji. Aina hizo ni;

    i). Ufugaji huria ambao unatumika kufuga Ng’ombe, Mbuzi, Kondoo, Punda, Mbwa, Bata, Kuku na Ngamia

    ii). Ufugaji nusu huria ambao unatumika kufuga Kuku na Bata

    iii). Ufugaji wa ndani na/ au kufunga ambao unatumika kufuga Ng’ombe na Mbuzi chotara wa maziwa, Kondoo, Kuku, Bata na Mbwa.

    Aidha kuna mikakati mbalimbali ambayo imewekwa ili kuhakikisha kuwa ufugaji bora na wakisasa unatekelezwa na wafugaji kama ifuatavyo;

    i). Kushirikiana na idara ya ardhi ili kuhakikisha mipango ya matumizi bora ya ardhi inatekelezwa ili kuepusha migogoro kati ya wafugaji na wadau wengine wanaotumia ardhi.

    ii). Kuwaelimisha wafugaji juu ya kanuni za ufugaji bora na faida zake ikiwemo aina bora na sahihi ya ufugaji pamoja na uvunaji wa mifugo ili kuendana na eneo la nyanda za malisho lililopo.

    iii). Kuboresha koo safu za mifugo kwa lengo la kuongeza uzalishaji wa mazao yatokanayo na mifugo kwa kutumia uhimilishaji na madume yaliyoboreshwa, mitetea pamoja na majogoo bora na kupunguza idadi ya mifugo na kuwa na mifugo michache yenye tija. Hili linafanyika katika ngazi ya mtu mmojammoja, kaya na vikundi.

    • Mipango ya kuboresha Bidhaa za Mifugo
  • i). Kushirikiana na sekta binafsi zinazofanya kazi za kuendeleza sekta ya mifugo na uvuvi ikiweo ujenzi wa machinjio za kisasa, masoko ya bidhaa za mifugo na viwanda vidogo vya kusindika mazao yatokanayo na mifugo.

    ii). Kuboresha koo safu za mifugo kwa lengo la kuongeza uzalishaji wa mazao yatokanayo na mifugo kwa kutumia uhimilishaji na madume yaliyoboreshwa, mitetea pamoja na majogoo bora na kutoa elimu ya ufugaji bora ili kuongeza kipato ngazi ya kaya na Taifa kwa ujumla.

    iii). Kudhibiti magonjwa ya mlipuko kwa kufanya chanjo, tiba za mifugo, uogeshaji wa mifugo pamoja na usimamizi wa minada ili kuongeza ubora na thamani ya mazao yatokanayo na mifugo.

    iv). Kutoa huduma bora ya ukaguzi wa nyama kwa lengo la kulinda afya ya jamii na kuzuia magonjwa ya kuambukiza (Zoonoses).

    v). Kusajili vituo vya huduma za mifugo ili kusogeza huduma za mifugo karibu na wafugaji na kusimamia utoaji wa huduma bora za mifugo zinazotolewa na wadau wa sekta binafsi.

    vi). Kutoa elimu juu ya ufugaji bora wa samaki kwenye mabwawa ya jamii na binafsi na kuzuia uvuvi haramu ili kuongeza kiwango bora cha uzalishaji wa samaki.

    KITENGO CHA NYUKI

    • Asali – Wastani wa Kilo 27,576 kwa mwaka.

      Nta  -   Wastani wa Kilo   2,519 kwa mwaka

      1. Nyuki Wasiouma – Wastani wa Kilo 300 za Asali kwa mwaka. (Ufugaji wa nyuki hawa unafanyika maeneo ya milimani).
    •  

        17.3 Mikakati Ya Kukuza Uzalishaji Wa Mazao Ya Nyuki 

      1. Kuboresha ufugaji nyuki kwa kutumia mizinga ya kisasa ya masanduku pamoja na zana za kisasa za ufugaji nyuki.
      2. Kuhamasisha wananchi (wafugaji nyuki) kuanzisha kilimo cha mazao yanayotoa kwa wingi chakula cha nyuki.
      3.  Kuwafundisha wafugaji nyuki kuhusu tekinolojia mwafaka ya ufugaji nyuki, mfano kutumia nyumba/ mabanda ya nyuki (Bee Houses).
      4. Kuimarisha vikundi vya ufugaji nyuki vilivyopo pamoja na kusimamia uanzishwaji wa vikundi vipya.
      5. Kuhamasisha wafugaji nyuki kutenga maeneo ya Hifadhi za nyuki/ Manzuki ili kupata umiliki wa ardhi na kurahisisha usimamizi wake.
      6. Kuhamasisha / Kuelimisha jamii (wakulima) kunyunyizia dawa za kuulia wadudu kwenye mimea ambayo haijatoa maua ili kuepuka kuua nyuki wanapoenda kuchukua chakula chao (Maji matamu - Nector).
      7. Kuhimiza / kuhamasisha jamii kuanzisha mfumo wa Kilimo- mseto unaohusisha Ufugaji Nyuki.
      8. Kuingiza shughuli za Ufugaji nyuki katika mpango wa matumizi bora ya ardhi.
      9. Kuhamasisha wananchi wanaoishi sehemu ambazo zinafaa kwa ufugaji wa nyuki wasiouma (milimani) hasa wanawake kuanzisha ufugaji wa nyuki wasiouma.
    •   17.4 Mikakati Ya Kufanya Zao La Asali Kuwa Zao La Kiuchumi Linalotegemewa Na Wilaya

      Kuanzisha utaratibu wa kukagua mazao ya nyuki ili kudhibiti ubora wake.

      Kuanzisha na kusimamia vituo vya kukusanyia na kuchakata asali.

      Kuwa na utaratibu wa kupima asali ili kudhibiti ubora wake.

      Kuanzisha utaratibu wa kuweka asali katika madaraja ili kupata bei nzuri. (Viwango vya ubora wa asali vitumike)

      Kutoa mafunzo na kuelimisha wafugaji nyuki (wazalishaji) na wafanyabiashara wadogo kuhusu njia bora zaidi za kutunza mazao ya nyuki.

      Kuhakikisha vifaa vya uvunaji, uchakataji, ufungashaji, uhifadhi na usafirishaji wa asali vinapatika kwa urahisi.

      Kuandaa mwongozo wa sheria ndogo kuhusu makusanyo ya mapato (ushuru) utokanao na mazao ya nyuki kwa wafanyabiashara wanaosafirisha nje ya Wilaya.

       

       

       

       

       

       

       

       

       

       

       

       

       

      KITENGO CHA UWEKEZAJI

      Halmashauri ya Wilaya ya Same ni miongoni ya wilaya 6 katika Mkoa wa Kilimanjaro ambayo inafursa za uwekezaji katika maeneo mbalimbali, ikiwemo sekta ya kilimo, madini, usafiri, utalii, ujenzi, uvuvi, ufugaji, mifugo, viwanda, biashara na kijamii (Elimu, Afya na Maji) na Kiutamaduni (Michezo na Utamaduni).n.k. Uwekezaji kwa mujibu wa kitaifa pia unalenga katika kuwezesha maendeleo ya nchi lakini pia kwa wakazi kufaidika na fursa mbalimbali.

       

      18.1 Idadi ya wawekezaji waliopo na aina ya uwekezaji

      Na

      Jina la mwekezaji

      aina ya uwekezaji

      Mahali ulipo

      Maelezo

      1.

      Willy Enterprises

      Madini ya boxite

      Mwembe/Chome

      Mwekezaji anachimba madini hayo na kupeleka katika nchi ya Kenya

      2.

      Umoja wa wakulima wa Tangawizi

      Kilimo cha tangawizi

      Myamba

      Umoja wa ushirika unawanachama zaidi 600

      3.


      Kiwanda cha Tangawizi

      Myamba

      Kiwanda kimesimama

      4.

      Miller International Agrovet

      Kilimo cha vitunguu

      Kijiji cha Jiungeni

      Miller inamiliki eneo la zaidi ya ekari 400.

      5.

      SMK

      Kilimo cha vitunguu

      Kijiji cha Jiungeni

      Anamiliki zaidi ya ekari 200 za vitunguu

      6.

      Tona lodge

      Utalii/Asili

      Kata ya Mshewa

      Uwekezaji unafanya shughuli za utalii wa asili

      7.

      MKUNAPA

      Utalii/wanyama pori

      Mbuga ya Mkomazi

      Eneo la uwekezaji linalolimilikiwa ni ekari 3245.

      8.

      KIDC

      Kiwanda cha vikombe

      Kata ya Same

      Kiwanda hakifanyi kazi kwa ufanisi kutokana na uongozi.

      9.

      Makampuni ya simu

      Mitandao ya simu

      Wilaya ya Same

      Makampuni ya simu ya Airtel, Haloteli Tigo, Vodacom na Zantel

      10.

      Mashirika ya Fedha

      Huduma ya ya fedha

      Wilaya ya Same

      NMB, CRDB, Same Kaya SACCOs, CWT, Amacha, BRAC n.k.

       

      19.2 Vivutio vya uwekezaji vilivyopo

      Na.

      Aina ya kivutio cha uwekezaji

      Vivutio

      1.

      Mbuga ya Taifa ya Mkomazi yenye ukubwa wa ekari 3245

      Wanyama wa aina mbalimbali, ndege na eneo lenye miti ya asili

      2.

      Uchimbaji wa madini

      Eneo la uchimbaji jasi, green garnet, green tourmaline, rhodilite na boxite.

      3.

      Bwawa la Kalimawe  na Karamba

      Aina ya samaki kama vile: Tilapia, perege, kambale na mkunga. Bwawa ili lina kilomita za mraba 3.

      4.

      Msitu wa Shengena hekta 27,880

      Aina ya miti, vipepeo, nyuki, ndege, mbega, nyani, tumbili na maji yanayotiririka kwa mwaka mzima.

      5.

      Mawasiliano na miundo mbinu

      Kuna barabara zinazopitika kwa mwaka mzima, mitandao ya simu na usafiri wa kampuni za Kilenga, Kimbwe na Phiba.

      6.

      Ujenzi wa viwanda

      Kuna maeneo ya ujenzi wa viwanda kama:- saruji n.k

      7.

      Mto Pangani

      Mto Pangani unaopita katika Kata ya Ruvu wenye urefu wa km 91, maji yanafaa kwa kilimo cha umwagiliaji na ufugaji wa samaki.

      8.

      Huduma za Malazi (Hotel)

      Katika Wilaya tuna wawekezaji katika huduma za malazi km Elephant Motel, Orlando, Nzoroko n.k.

      Chanzo: Kitengo cha Uwekezaji

      18.3 Maeneo yaliyotengwa kwa uwekezaji

      Halmashauri ya wilaya ya Same imetenga jumla ya ekari kama ifuatavyo:-

      -Eneo la Kitamri Halmashauri imetenga ekari 150 kwa ajili ya ujenzi wa viwanda

      -Eneo la Kata ya Makanya Kijiji kimetenga jumla ya ekari 100 kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda cha saruji.

      Mkakati wa halmashauri ya uendelezaji wa fursa za uwekezaji;-

      Halmashauri imeandaa mpango wa kujenga mazingira kwa makundi haya ya wakulima wadogo na wafugaji kuchangamkia fursa hizi badala ya kuelekeza jitihada kubwa katika uwekezaji kutoka nje.

      Halmashauri inautaratibu wa kuwashirikisha wawekezaji kutoka nje wawekeze katika msingi wa ubia na wazalishaji wadogo, kwa maana kuwa wazalishaji wadogo - wakulima na wafugaji - katika vikundi vyao, msingi wao mkubwa ukiwa ni rasilimali ardhi, wanaweza kuingia katika ubia na wawekezaji toka nje kwa namna ambayo wanakuwa na sauti katika maamuzi na hivyo kuwezesha kile tukiitacho win win situation, yaani 'hali ya mafanikio kwa pande zote zinazohusika'.

      Halmashauri inawezesha vikundi vya wajasiriamali wadogo kwa kuwapa mikopo ya riba nafuu ili kuwa na fursa za wazalishaji wadogo vijijini.

      Halmashauri kwa kushirikiana na wawekezaji kuimarisha miundombinu ya barabara na mawasiliano ya simu katika maeneo ya Wilaya ya Same.

      18.4 Mikakati ya kuwa na viwanda Wilayani

      Kampuni ya DOTT Services (T) imeanza mazungumzo na Halmashauri kwa ajili ujenzi wa kiwanda cha kuparck maji na uvunjaji wa kokoto katika eneo la Saweni.

      Uwekezaji wa kiwanda cha saruji katika Kata ya Makanya, ambapo mkakati wa kumpatia mwekezaji wa kampuni ya A to Z toka Arusha. Taratibu za kupata eneo katika Kata ya Makanya (Vikao vya awali vya kijiji cha Makanya vimekwisha fanyika)

      Kilimo cha miwa; Uwekezaji wa kilimo cha miwa kampuni ya Kilimanjaro Biochem Limited inayomiliki kiwanda cha utengenezaji wa spiriti katika wilaya ya Mwanga kimeanza maandalizi ya kuwa na mikataba na wakulima ili waweze kulima miwa katika kata ya Ruvu. KBL inahitaji kulimiwa miwa kiasi cha ekari 2000 wameanza mazungumzo na wakulima wa maeneo ya kata ya Ruvu. Endapo wakulima wataridhia mikataba hiyo, kampuni hiyo imepanga kujenga kiwanda katika eneo la Ruvu Muungano cha kukamua miwa na kusafirisha ikiwa maji ya miwa (syrup). Kiwanda hicho kitakuwa na uwezo wa kuajiri wafanyakazi zaidi ya 200. (Ombi la KBL liliwasilishwa kwenye kamati ya Fedha, Utawala na Mipango).

       

       

       

       

       

       

      CHANGAMOTO ZA KIWILAYA

      MIKAKATI YA KIWILAYA

      Kuhakikisha elimu ya uvunaji maji ya mvua, matumizi bora ya maji  na hifadhi ya ardhi na udongo imetolewa kwa wakulima.

  • Kutoa elimu kwa wakulima juu ya kuzuia/kupunguza upotevu wa

         mazao ya nafaka na mikunde wakati wa kuvuna na kuhifadhi   

         (Post harvest loss handling).

    Kuhakikisha elimu ya ukadiriaji wa mahitaji ya mazao ya chakula kwa wakulima ngazi ya kaya imetolewa.

    Kutoa elimu kwa wakulima juu ya hifadhi na matumizi bora ya mazao ya chakula kwa maeneo ambayo yamepata mavuno mazuri msimu wa vuli hasa maeneo ya kilimo cha umwagiliaji.

    Kutoa ushauri kwa wakulima kutekeleza kilimo cha mazaoyanayostahimili ukame na yanayotumia kiasi kidogo cha unyevu hadi kukomaa kama  mazao jamii ya mizizi na mikunde na Mtama.

    Kuhakikisha uimarishaji wa matumizi bora ya maji katika  miundombinu ya umwagiliaji iliyopo na kuhakikisha kunakuwepo na ongezeko la uzalishaji wa mazao ya chakula kwa misimu miwili na wakulima wanazingatia ushauri wa wataalam waliopo vijijini.

    Kwa kuwatumia Maafisa Ugani waliopo kuhakikisha wakulima wanatumia teknolojia bora na sahihi za uzalishaji mazao ya chakula na biashara kwa ajili ya uhakika na usalama wa chakula ngazi ya kaya.

    Kuhimiza wafugaji walio na mifugo kuuza wakati bado ikiwa na hali nzuri ya kiafya na kununua chakula na kuhifadhi kwa ajili ya matumizi ya familia.

    Kuhimiza wakulima waliopo maeneo ya umwagiliaji kulima mazao yenye thamani na ubora kwa uhakika wa kuongeza kipato hatimaye kumudu kujinunulia chakula cha kutosha.

    Kuhamasisha wafanyabiashara wenye uwezo  kununua chakula Katika maeneo yenye chakula cha ziada na kuleta kuuza katika maeneo yenye upungufu kwa bei nafuu/elekezi.

    Kampuni ya DOTT Services (T) imeanza mazungumzo na Halmashauri kwa ajili ujenzi wa kiwanda cha kuparck maji na uvunjaji wa kokoto katika eneo la Saweni.

    Uwekezaji wa kiwanda cha saruji katika Kata ya Makanya, ambapo mkakati wa kumpatia mwekezaji wa kampuni ya A to Z toka Arusha. Taratibu za kupata eneo katika Kata ya Makanya (Vikao vya awali vya kijiji cha Makanya vimekwisha fanyika)

    Kilimo cha miwa; Uwekezaji wa kilimo cha miwa kampuni ya Kilimanjaro Biochem Limited inayomiliki kiwanda cha utengenezaji wa spiriti katika wilaya ya Mwanga kimeanza maandalizi ya kuwa na mikataba na wakulima ili waweze kulima miwa katika kata ya Ruvu. KBL inahitaji kulimiwa miwa kiasi cha ekari 2000 wameanza mazungumzo na wakulima wa maeneo ya kata ya Ruvu. Endapo wakulima wataridhia mikataba hiyo, kampuni hiyo imepanga kujenga kiwanda katika eneo la Ruvu Muungano cha kukamua miwa na kusafirisha ikiwa maji ya miwa (syrup). Kiwanda hicho kitakuwa na uwezo wa kuajiri wafanyakazi zaidi ya 200. (Ombi la KBL liliwasilishwa kwenye kamati ya Fedha, Utawala na Mipango).

     

     

     

     

     

     

     

    Kuongeza Ajira kwa Vijana 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 31, 2021
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI May 06, 2025
  • Siku ya kufanya usafi mwezi Septemba September 08, 2021
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2020 August 21, 2020
  • Tazama Vyote

Habari Za Sasa

  • WACHIMBA MADINI SAME WATAKIWA KUTUNZA MAZINGIRA

    May 19, 2025
  • SAME YAPANIA KUONGEZA UZALISHAJI WA MKONGE

    May 05, 2025
  • SAME YAPANIA KUONGEZA UZALISHAJI WA MKONGE

    May 05, 2025
  • SAME YAOMBA WIZARA YA KILIMO KUIPATAIA MICHE YA PARACHICHI

    May 01, 2025
  • Tazama Vyote

Video

KARIBU MWENGE WA UHURU SAME KILIMANJARO 2022
Video Zaidi

Viunganishi Vya Haraka

  • Forms And Templates
  • Galleys
  • News
  • Events
  • Strategic Plan
  • Reports
  • Acts
  • Malalamiko

Viunganishi Vyenye Uhusiano

  • PO-Ralg
  • PO-Psm
  • e-Government Agency
  • Kilimanjaro Region
  • Employment
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Watembeleaji

free HitCounter

Ramani Ya Wilaya

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Same.Haki zote zimehifadhiwa.