• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Same District Council
Same District Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala Za Mikoa na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Same

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idaraya Elimu Sekondari
      • Rasili Mali Watu na Utawala
      • Ardhi Maliasili na Utalii
      • Fedha Na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Kazi na Zimamoto
      • Maji
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi.
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo Cha TEHAMA
      • Kitengo Cha Nyuki
      • Kitengo Cha Uchaguzi
      • Kitengo Cha Manunuzi
      • Kitengo Cha Sheria
    • Kata
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Mipango
      • Elimu,Afya na Maji
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
      • TAMKO LA VIONGOZI WA UMMA KUHUSU RASILIMALI NA MADENI
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Stoo Ya Picha

WAFUGAJI WATAKIWA KUTOA USHIRIKIANO ZOEZI LA CHANJO

Posted on: August 11th, 2025

Wafugaji Wilayani Same wametakiwa kutoa ushirikiano kwa maafisa mifugo wakati huu ambao kunafanyika zoezi la utoaji wa chanjo za mifugo zenye ruzuku ya Serikali ili kukinga mifugo na kuku dhidi ya magonjwa mbalimbali.

Afisa Mifugo na kilimo Wilayani Same Bw.Ninzari Idd amesema zoezi hilo la chanjo ya Ruzuku linakwenda sambamba na zoezi la utambuzi wa mifugo kwa kuvishwa hereni maalumu za kielektroniki ili iweze kutambuliwa popote itakapokuwepo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan katika juhudi za kuboresha uzalishaji wa mifugo hapa nchini alizindua kampeni ya Kkitaifa ya utoaji chanjo za mifugo zenye ruzuku ya Serikali tarehe 16 Juni 2025 Wilayani Bariadi (Simiyu).

Chanjo hizi ni dhidi ya Homa ya Mapafu ya Ng’ombe (CBPP) ambayo inatolewa kwa Tsh 500 kwa ng’ombe mmoja badala ya Tsh 1000 na kwa upande wa mbuzi, chanjo ya Sotoka ya mbuzi itatolewa kwa Tsh 300 kwa mbuzi mmoja badala ya Tsh 500 ya bei ya soko. Aidha chanjo ya kuku aina ya Tatu moja ambayo ni dhidi ya magojwa ya Ndui, Mafua na kideri yanayoathiri kuku inatolewa bure (bila malipo).

Bw.Ninzari amesema faida za kampeni hii ya kitaifa ya utoaji chanjo na utambuzi wa mifugo ni pamoja na kuboresha afya za mifugo na uzalishaji, kuwa na uhakika wa masoko ya mifugo ndani nan je ya nchi  na kuzuia wizi wa mifugo.

Zoezi la utoaji wa chanjo za mifugo Wilayani Same lilianza Julai 4, 2025 kwa utoaji wa chanjo aina ya Tatu moja kwa kuku dhidi ya magonjwa ya Ndui, Mafua makali na kideri/mdondo ambapo hadi mwanzoni mwa mwezi Oktoba 2025, jumla ya kuku 202,401 wamechanjwa na lengo ni kufikia kuku 220,000.

Ambapo kwa upande wa Ng,ombe jumla ya Ng’ombe 24,364 wameshachanjwa na kuwekwa hereni za kielekroniki kati ya ng’ombe 130,000 wanaotarajiwa kuchanjwa katika Wilaya ya Same.

Mfugaji John Samweli Mamasita wa Kata ya Ruvu amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwaletea chanjo wa mifugo yenye ruzuku kwani imewapunguzia gharama hivyo itawezesha mifugo yote kuchanjwa.

Naye Mfugaji Yohana Kiroya ambaye anasema tayari mifugo yake imeshapatiwa chanjo na anaendelea na zoezi la uwekaji hereni za kielektronik ameishukuru Serikali kwa kuwapatia ruzuku ya Chanjo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 31, 2021
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI May 06, 2025
  • Siku ya kufanya usafi mwezi Septemba September 08, 2021
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2020 August 21, 2020
  • Tazama Vyote

Habari Za Sasa

  • WAGOMBEA TISA KUCHUANA UBUNGE SAME

    October 01, 2025
  • WAFUGAJI WATAKIWA KUTOA USHIRIKIANO ZOEZI LA CHANJO

    August 11, 2025
  • BODI YA PAMBA YATOA ZAWADI SAME

    September 16, 2025
  • RAS KILIMANJARO APONGEZA USIMAMIZI WA MIRADI

    October 03, 2025
  • Tazama Vyote

Video

Video Zaidi

Viunganishi Vya Haraka

  • Forms And Templates
  • Galleys
  • News
  • Events
  • Strategic Plan
  • Reports
  • Acts
  • Malalamiko

Viunganishi Vyenye Uhusiano

  • PO-Ralg
  • PO-Psm
  • e-Government Agency
  • Kilimanjaro Region
  • Employment
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Watembeleaji

free HitCounter

Ramani Ya Wilaya

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Same.Haki zote zimehifadhiwa.