• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Same District Council
Same District Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala Za Mikoa na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Same

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idaraya Elimu Sekondari
      • Rasili Mali Watu na Utawala
      • Ardhi Maliasili na Utalii
      • Fedha Na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Kazi na Zimamoto
      • Maji
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi.
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo Cha TEHAMA
      • Kitengo Cha Nyuki
      • Kitengo Cha Uchaguzi
      • Kitengo Cha Manunuzi
      • Kitengo Cha Sheria
    • Kata
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Mipango
      • Elimu,Afya na Maji
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
      • TAMKO LA VIONGOZI WA UMMA KUHUSU RASILIMALI NA MADENI
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Stoo Ya Picha

BODI YA PAMBA YATOA ZAWADI SAME

Posted on: September 16th, 2025

Bodi ya Pamba nchini (TCB)) imetoa zawadi ya majiko ya gesi kwa wakulima hodari wa Pamba Wilayani Same ambao wameweza kuzingatia kanuni za kilimo bora cha Pamba kilichowezesha uzalishaji wa zaidi ya kilo 1,500 kwenye ekari moja.

Bodi hiyo pia imetoa zawadi ya vitenge na kanga kwa maafisa Ugani Wilayani Same kama sehemu ya kutambua mchango wao katika kuongeza uzalishaji wa zao la Pamba.

Wakulima walionufaika na zawadi hizo ni Gabriel Mbwambo na Praise Mbwambo ambao wote wanatoka Kata ya Kisiwani na maafisa ugani waliopatiea zawadi ni Debora Mtati na Fatuma Sadala.

Akikabidhi zawadi hizo Afisa Kilimo kutoka Bodi ya Pamba Bw. Alphonce Ngawagala

alisema utoaji wa zawadi ni motisha kwa Wakulima na maafisa ugani ili kuchochea ongezeko la uzalishaji wa Pamba hapa nchini.

"Bodi ya Pamba itaendelea kutoa zawadi kama motisha kwa wakulima wa pamba ili zao hili liweze kuzalishwa kwa wingi katika maeneo mengi wilayani Same na nchini kwa jumla"alisema Bw.Ngawagala na kuongeza kuwa mwaka jana Bodi hiyo ilikabidhi zawadi ya Trekta yenye thamani ya mil 55 kwa mkulima Gabriel Mbwambo baada ya kuibuka mkulima bora wa Pamba kwenye Kanda hii.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Same Bw.Wambura Yamo aliwapongeza Wakulima waliofanya vizuri msimu huu na kuwataka kuongeza jitihada ili zao la Pamba lienee maeneo mengi Wilayani Same."Uzalishaji wa Pamba unapoongezeka hata mapato ya serikali yanaongezeka kupitia ushuru wa mazao na Serikali inapoongeza mapato inaboresha utoaji wa huduma za kijamii.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 31, 2021
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI May 06, 2025
  • Siku ya kufanya usafi mwezi Septemba September 08, 2021
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2020 August 21, 2020
  • Tazama Vyote

Habari Za Sasa

  • WAGOMBEA TISA KUCHUANA UBUNGE SAME

    October 01, 2025
  • WAFUGAJI WATAKIWA KUTOA USHIRIKIANO ZOEZI LA CHANJO

    August 11, 2025
  • BODI YA PAMBA YATOA ZAWADI SAME

    September 16, 2025
  • RAS KILIMANJARO APONGEZA USIMAMIZI WA MIRADI

    October 03, 2025
  • Tazama Vyote

Video

Video Zaidi

Viunganishi Vya Haraka

  • Forms And Templates
  • Galleys
  • News
  • Events
  • Strategic Plan
  • Reports
  • Acts
  • Malalamiko

Viunganishi Vyenye Uhusiano

  • PO-Ralg
  • PO-Psm
  • e-Government Agency
  • Kilimanjaro Region
  • Employment
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Watembeleaji

free HitCounter

Ramani Ya Wilaya

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Same.Haki zote zimehifadhiwa.