• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Same District Council
Same District Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala Za Mikoa na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Same

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idaraya Elimu Sekondari
      • Rasili Mali Watu na Utawala
      • Ardhi Maliasili na Utalii
      • Fedha Na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Kazi na Zimamoto
      • Maji
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi.
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo Cha TEHAMA
      • Kitengo Cha Nyuki
      • Kitengo Cha Uchaguzi
      • Kitengo Cha Manunuzi
      • Kitengo Cha Sheria
    • Kata
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Mipango
      • Elimu,Afya na Maji
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
      • TAMKO LA VIONGOZI WA UMMA KUHUSU RASILIMALI NA MADENI
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Stoo Ya Picha

SAME YAZINDUA UANDIKISHAJI WA BIMA YA AFYA KWA WOTE

Posted on: February 17th, 2026

Katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya bila kikwazo cha kifedha, Wilaya ya Same imezindua rasmi zoezi la uandikishaji wa Bima ya Afya kwa Wote. Uzinduzi huo ulifanyika Kata ya Stesheni, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Sera ya Afya  ya kuwafikia wananchi wote kwa huduma za afya.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Katibu Tawala wa Wilaya ya Same, Bi. Mamndolwa Gembe, amewataka watumishi wa afya katika maeneo lengwa kuhakikisha elimu ya Bima ya Afya kwa wote inawafikia wananchi wote ili waweze kuuelewa na kuutumia ipasavyo.

Aidha, amewasisitiza wanufaika kutumia vitambulisho vya bima kwa uaminifu na kuvitunza vizuri, akionya kuwa vitambulisho hivyo vinapaswa kutumiwa na walengwa halali pekee.

“Huduma itatolewa kwa mmiliki wa kitambulisho pekee. Isitokee kumpa ndugu, rafiki au mtu mwingine asiyehusika kutumia. Endapo itabainika, hatua za kisheria zitachukuliwa,” amesema Gembe.

Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Same, Dkt. Alex Alexander, amesema Serikali imewekeza zaidi ya shilingi bilioni 1 kwa ajili ya kugharamia walengwa 7,921 wilayani Same, hatua itakayowawezesha wananchi wasio na uwezo kupata huduma za afya bila kulipia.

Naye Diwani wa Kata ya Stesheni Mhe.Saida Magiri ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kutekeleza mpango huo kwa vitendo, akisema mpango wa Bima ya Afya kwa Wote unalenga kuboresha afya na ustawi wa wananchi wenye mahitaji maalum.

Serikali ilitangaza kuanza rasmi kwa utekelezaji wa mpango wa Bima ya Afya kwa wote kuanzia Januari 26, 2026. Kupitia mpango huo, kaya zitajiunga kwa kulipa shilingi 150,000 kwa mwaka kwa kaya isiyozidi watu sita, huku wananchi wasio na uwezo wakigharamiwa na Serikali.

Matangazo

  • TANGAZO LA USAJILI WA WAANDAAJI WA MAUDHUI MTANDAONI WILAYA YA SAME February 03, 2026
  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA October 28, 2024
  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA October 28, 2024
  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA October 28, 2024
  • Tazama Vyote

Habari Za Sasa

  • WAZIRI MKUU AFANYA ZIARA SAME,ATEMBELEA UJENZI WA CHUO CHA VETA

    February 19, 2026
  • SAME YAZINDUA UANDIKISHAJI WA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    February 17, 2026
  • SAME YAOMBA KUIDHINISHIWA BAJETI YA TSH.BIL60.3

    February 06, 2026
  • WAZIR​I ULEGA AKAGUA UJENZI WA BARABARA YA SAME–MKOMAZI–NDUNGU

    February 16, 2026
  • Tazama Vyote

Video

Video Zaidi

Viunganishi Vya Haraka

  • Forms And Templates
  • Galleys
  • News
  • Events
  • Strategic Plan
  • Reports
  • Acts
  • Malalamiko

Viunganishi Vyenye Uhusiano

  • PO-Ralg
  • PO-Psm
  • e-Government Agency
  • Kilimanjaro Region
  • Employment
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Watembeleaji

free HitCounter

Ramani Ya Wilaya

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Same.Haki zote zimehifadhiwa.