Halmashauri ya Wilaya ya Same imeomba kuidhinishiwa Bajeti ya shilingi bilioni 60.3 kwa mwaka wa fedha 2026/2027 ili kufanikisha Utekelezaji wa Miradi ya maendeleo na uendeshaji wa Halmashauri.
Bajeti hiyo ilijadiliwa na kuridhiwa na madiwani kwenye kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika Februari 04, 2026, kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Same.
Akizungumza katika kikao hicho, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Same, Bw. Yusto Mapande, alisema kuwa bajeti hiyo imelenga ustawi wa wananchi wa Same kwa kuzingatia mahitaji yao ya msingi na vipaumbele vya maendeleo.
Nae Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Same, Bw. Abdallah Mnyambo, aliwakumbusha watumishi wa umma pamoja na viongozi wa Serikali kuendelea kusimamia ipasavyo miradi Maendeleo.
Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Same.Haki zote zimehifadhiwa.