• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Same District Council
Same District Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala Za Mikoa na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Same

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idaraya Elimu Sekondari
      • Rasili Mali Watu na Utawala
      • Ardhi Maliasili na Utalii
      • Fedha Na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Kazi na Zimamoto
      • Maji
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi.
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo Cha TEHAMA
      • Kitengo Cha Nyuki
      • Kitengo Cha Uchaguzi
      • Kitengo Cha Manunuzi
      • Kitengo Cha Sheria
    • Kata
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Mipango
      • Elimu,Afya na Maji
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
      • TAMKO LA VIONGOZI WA UMMA KUHUSU RASILIMALI NA MADENI
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Stoo Ya Picha

SAME YAOMBA WIZARA YA KILIMO KUIPATAIA MICHE YA PARACHICHI

Posted on: May 1st, 2025

Kufuatia mahitaji makubwa ya miche ya zao la Parachichi Halmashauri ya Wilaya ya Same imeandika maombi Wizara ya Kilimo kuomba kusaidiwa miche 56,289 ya Parachichi  zinazokomaa  muda mfupi ili kuweza kuisambaza kwa wananchi.

Tangu mwaka 2022 Wilaya ya Same imeliweka zao la Parachichi kmiongoni mwa mazao ya kimkakati ya kuinua uchumi wa Wananchi wa ukanda wa milimani kwenye Wilaya ya Same.

Baada ya zao hilo kutangazwa kama zao la kimmkakakti lenye lengo la kuinua uchumi wa Wakulima tayari jumla ya miche 5,822 imeshaoteshwa kenye maeneo mbalimbali ambapo miche hiyo ilitolewa na wafadhili mbalimbali wakiwemo Mfuko wa Uhifadhi wa Milima ya Tao la Mashariki (EAMCEF) pamoja na Shirika la Forest Focus.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya WIlaya ya Same Bw.Jimson Mhagama amesema mwamko wa wananchi kuotesha Parachichi zinazokomaa muda mfupi ni mkubwa sana ndio maana tumeamua kuomba Msaada wa Wizara ili kupata miche zaidi.

“Tuna Kata zaidi ya 12 za ukanda wa milimani ambao una baridi ambapo utafiti umeonyesha kwamba hizi Parachichi zinaweza kustawi na tayari wananchi tumewahamasisha kupanda parachichi hizi na mwamko umekuwa mkubwa” alisema Mhagama.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Same Mheshimiwa Yusto Mapande ameahidi kufuatilia maombi hayo ya Miche Wizara ya Kilimo ili wananchi waweze kupatiwa.

Afisa Kilimo, Mifugo na Uvuvi wa Wilaya ya Same, Dkt.Cainan Kiswaga alisema miche ya Parachichi inayokomaa mapema ni chachu ya kuinua wananchi kiuchumi kwani mti mmoja wenye miaka mine unaweza kuzaa matunda 400 kwa mwaka na uzalishaji huongezeka kwa kadri umri wake unavyoongezeka ambapo mti wa miaka saba huzaa matunda hadi 800 kwa mwaka wakati miti ya asili ina uwezo wa kuzaa matunda 150 tu kwa mwaka.

Alizitaja Kata ambazo zao la Parachichi linastawi kuwa ni pamoja na Mshewa,Mhezi,Msindo,Vuje,Mtii,Bombo,Bwambo,Mpinji,Chome,Vudee, Vunta, Suji na  Myamba.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 31, 2021
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI May 06, 2025
  • Siku ya kufanya usafi mwezi Septemba September 08, 2021
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2020 August 21, 2020
  • Tazama Vyote

Habari Za Sasa

  • WACHIMBA MADINI SAME WATAKIWA KUTUNZA MAZINGIRA

    May 19, 2025
  • SAME YAPANIA KUONGEZA UZALISHAJI WA MKONGE

    May 05, 2025
  • SAME YAPANIA KUONGEZA UZALISHAJI WA MKONGE

    May 05, 2025
  • SAME YAOMBA WIZARA YA KILIMO KUIPATAIA MICHE YA PARACHICHI

    May 01, 2025
  • Tazama Vyote

Video

KARIBU MWENGE WA UHURU SAME KILIMANJARO 2022
Video Zaidi

Viunganishi Vya Haraka

  • Forms And Templates
  • Galleys
  • News
  • Events
  • Strategic Plan
  • Reports
  • Acts
  • Malalamiko

Viunganishi Vyenye Uhusiano

  • PO-Ralg
  • PO-Psm
  • e-Government Agency
  • Kilimanjaro Region
  • Employment
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Watembeleaji

free HitCounter

Ramani Ya Wilaya

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Same.Haki zote zimehifadhiwa.