• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Same District Council
Same District Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala Za Mikoa na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Same

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idaraya Elimu Sekondari
      • Rasili Mali Watu na Utawala
      • Ardhi Maliasili na Utalii
      • Fedha Na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Kazi na Zimamoto
      • Maji
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi.
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo Cha TEHAMA
      • Kitengo Cha Nyuki
      • Kitengo Cha Uchaguzi
      • Kitengo Cha Manunuzi
      • Kitengo Cha Sheria
    • Kata
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Mipango
      • Elimu,Afya na Maji
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
      • TAMKO LA VIONGOZI WA UMMA KUHUSU RASILIMALI NA MADENI
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Stoo Ya Picha

SAME YAADHIMISHA SIKU YA LISHE

Posted on: November 1st, 2023

Halmashauri ya Wilaya ya Same imeadhimisha siku ya Lishe katika Wilaya hiyo kwa lengo la kuikumbusha Jamii kuzingatia mlo kamili katika kila mlo wanaokula ili kuimarisha afya zao.

Akizungumza katika maadhimisho hayo Mkuu wa Wilaya ya Same Mheshimiwa Kasilda Mgeni aliwataka wananchi kuzingatia maelekezo ya wataalam wa Lishe ili kuhakikisha kuwa wanaokula mlo ulio bora.

Mkuu wa Wilaya ambaye pia alipata fursa ya kutembelea mabanda ya maonyesho ya vyakula mbalimbali vinavyoimarisha afya aliipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Same kwa kuandaa siku ya lishe ambayo imewawezesha wananchi wengi kupata elimu ya Lishe.

"Hii siku ni muhimu sana kwani inaongeza uelewa wa wananchi kuhusu Lishe bora lakini nichukue nafasi hii kuwahimiza wanawake wajawazito kuhudhuria Clinic ili waweze kupata chanjo mbalimbali lakini pia watoto wote Chini ya miaka mitano wapelekwe clinic ili kujua Maendeleo ya ukuaji wao na pia waweze kupata chanjo" alisema Bi.Kasilda

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Bi.Anastazia Tutuba aliwataka wazazi wenye watoto mashuleni kuhakikisha kuwa wanachangia chakula ili watoto wao waweze kupata chakula cha mchana shuleni.

Alisema Wilaya ya Same ni miongoni mwa Wilaya zilizosaini Utekelezaji wa Mkataba wa Afua za Lishe ambapo Wanafunzi kupatiwa chakula cha mchana shuleni ni kigezo cha muhimu.

"Tumeshatunga Sheria ndogo ya Mahudhurio ya lazima shuleni na uchangiaji wa chakula shuleni sasa mzazi yeyote asiyetaka kuchangia chakula kwa hiari shuleni basi atakutana na mkono wa Sheria "alisema Bi.Tutuba.

Akizungumza katika maadhimisho hayo Afisa Lishe wa Wilaya ya Same Bi.Jackline Kilenga amesema kwa sasa Wanafunzi wanaokula shuleni ni asilimia 85 Kati ya Wanafunzi 63,512 wanaopaswa kupata chakula shuleni.

"Kwa upande wa kutembelea Kaya zenye wajawazito na watoto wadogo tumefanikiwa kwa asilimia 100 ambapo Kaya 5,310 zilitembelewa,na Vijiji vyote vina utaratibu wa kuwabana wazazi na walezi juu ya masuala ya Lishe"amesema Bi.Kilenga.





Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 31, 2021
  • Siku ya kufanya usafi mwezi Septemba September 08, 2021
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2020 August 21, 2020
  • MATOKEO DARASA LA SABA 2020 November 23, 2020
  • Tazama Vyote

Habari Za Sasa

  • DC AZINDUA KAMPENI YA KUOTESHA MITI

    November 12, 2023
  • DKT.MAHERA AAHIDI SERIKALI KUTOA FEDHA KUMALIZIA UJENZI WA HOSPITALI YA WILAYA

    November 03, 2023
  • DKT.MAHERA AAHIDI SERIKALI KUTOA FEDHA KUMALIZIA UJENZI WA HOSPITALI YA WILAYA

    November 03, 2023
  • SAME YAOMBA KUJENGEWA DARAJA LA KUWAUNGANISHA NA SIMANJIRO

    November 02, 2023
  • Tazama Vyote

Video

KARIBU MWENGE WA UHURU SAME KILIMANJARO 2022
Video Zaidi

Viunganishi Vya Haraka

  • Forms And Templates
  • Rules and Regulation
  • Videos
  • Galleys
  • News
  • Events
  • Strategic Plan
  • Reports
  • Acts

Viunganishi Vyenye Uhusiano

  • PO-Ralg
  • PO-Psm
  • e-Government Agency
  • Kilimanjaro Region
  • Employment
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Watembeleaji

free HitCounter

Ramani Ya Wilaya

Wasiliana Nasi

    The Way Through Mkomazi Nationa Park or District Hospital(Kibacha Rd)

    Sanduku La Posta: P.O.Box 138

    Simu ya mezani: +255 27 2758034

    Simu Ya Mkononi: +255 717657681

    Email: ded@samedc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Same.Haki zote zimehifadhiwa.