• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Same District Council
Same District Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala Za Mikoa na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Same

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idaraya Elimu Sekondari
      • Rasili Mali Watu na Utawala
      • Ardhi Maliasili na Utalii
      • Fedha Na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Kazi na Zimamoto
      • Maji
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi.
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo Cha TEHAMA
      • Kitengo Cha Nyuki
      • Kitengo Cha Uchaguzi
      • Kitengo Cha Manunuzi
      • Kitengo Cha Sheria
    • Kata
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Mipango
      • Elimu,Afya na Maji
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
      • TAMKO LA VIONGOZI WA UMMA KUHUSU RASILIMALI NA MADENI
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Stoo Ya Picha

SAME KUWEKEZA ZAIDI KATIKA KILIMO BIASHARA

Posted on: August 8th, 2023

Katika jitihada za kuboresha kilimo na kuinua uchumi wa wakulima Halmashauri ya Wilaya ya Same imegawa Kanda tatu za Uchumi wa Kilimo ambazo wakulima wanapewa elimu juu ya aina ya mazao ya biashara yanayoweza kustawi katika Kanda hizo.

Akizungumza katika maonesho ya Nanenane Kanda ya Kaskazini yaliyofanyika katika viwanja vya Themi,Njiro mkoani Arusha Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Same Mhe. Yusto Mapande alisema kwa muda mrefu wakulima wilayani humo wamekuwa wakilima kilimo cha mazoea ambacho hakijaweza kuwainua kiuchumi.

“Tumeamua kugawa Kanda tatu za kilimo ambazo ni Ukanda wa Tambarare ambao unalimwa Mkonge na mbogamboga katika eneo la umwagiliaji la Ruvu,Ukanda wa Kati ambao unalima Mpunga na Ukanda wa juu milimani ambao unalima Tangawizi na kwa sasa tunahimiza sana kilimo cha parachichi na tayari tumeshaanzisha vitalu vya miche ya parachichi” alisema Mapande

Amesema ili kufanikisha malengo ya kuinua uchumi wa wakulima Halmashauri inatengeneza miundombinu ya umwagiliaji ili kuwasaidia wakulima kuondokana na kilimo cha mazoea cha kutegemea mvua za msimu.

“Sambamba na kuboresha miundombinu pia tunahakikisha wakulima wanapata pembejeo za kilimo kwa wakati ambapo tunatumia mawakala wa pembejeo waliopo katika maeneo yetu yote” amesema Mhe.Mapande.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Same Bi.Anastazia Tutuba amesema maafisa Ugani wa Halmashauri waliopo katika Kata wamekuwa wakiendelea kutoa elimu kwa wakulima juu ya njia mbalimbali za kuboresha kilimo.

“Njia nyingine ya kutoa elimu kwa wakulima wetu ni kupitia maonesho haya ya Nanenane,hapa tumekuja na wakulima wetu ambapo pamoja na kutangaza bidhaa zao lakini wanajifunza mbinu mbalimbali za kilimo kutoka kwa wenzao wa maeneo mengine” amesema Bi.Tutuba.

Mkurugenzi huyo amesema kwa mwaka wa fedha ulioishia June 2023, Divisheni ya Kilimo,Mifugo na Uvuvi ilitumia shilingi milioni 116 katika kuboresha kilimo na ufugaji wilayani humo.

Akizungumza katika Maonesho hayo, Mwenyekiti wa wakulima wa Tangawizi Kata ya Myamba Bw.Mbaraka Ally amesema "Faida kubwa ya kushiriki maonyesho ya nanenane ni kutangaza bidhaa yetu ya Tangawizi ambayo inatoka Mamba-Myamba, ambapo Tangawizi yetu ina ubora wa hali ya juu”

Bw.Eliniokoa Joseph ambaye ni Mkazi wa Arusha anasema" Nimekuja kwenye Banda la Maonesho la Same mahususi kwa ajili ya kununua Tangawizi ya Same, nimeshaitumia,ni nzuri sana na  inaponya mafua na magonjwa madogo madogo ni nzuri".

Maonesho ya Nane nane ya mwaka 2023 yamebebwa na kaulimbiu isemayo “Vijana na Wanawake ni Msingi Imara wa Mifumo Endelevu wa Chakula”

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 31, 2021
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI May 06, 2025
  • Siku ya kufanya usafi mwezi Septemba September 08, 2021
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2020 August 21, 2020
  • Tazama Vyote

Habari Za Sasa

  • MRADI WA SWASH ULIVYONUFAISHA WILAYA YA SAME

    April 03, 2025
  • WANANCHI WA MAKEI,SAME WAONDOKANA NA ADHA YA MAJI

    March 23, 2025
  • SAME YATOA ELIMU YA TAHADHARI YA MPOX MASHULENI

    March 18, 2025
  • MAAFISA UTUMISHI SIMAMIENI STAHIKI ZA WATUMISHI-DC SAME

    March 13, 2025
  • Tazama Vyote

Video

KARIBU MWENGE WA UHURU SAME KILIMANJARO 2022
Video Zaidi

Viunganishi Vya Haraka

  • Forms And Templates
  • Galleys
  • News
  • Events
  • Strategic Plan
  • Reports
  • Acts
  • Malalamiko

Viunganishi Vyenye Uhusiano

  • PO-Ralg
  • PO-Psm
  • e-Government Agency
  • Kilimanjaro Region
  • Employment
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Watembeleaji

free HitCounter

Ramani Ya Wilaya

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Same.Haki zote zimehifadhiwa.