• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Same District Council
Same District Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala Za Mikoa na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Same

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idaraya Elimu Sekondari
      • Rasili Mali Watu na Utawala
      • Ardhi Maliasili na Utalii
      • Fedha Na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Kazi na Zimamoto
      • Maji
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi.
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo Cha TEHAMA
      • Kitengo Cha Nyuki
      • Kitengo Cha Uchaguzi
      • Kitengo Cha Manunuzi
      • Kitengo Cha Sheria
    • Kata
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Mipango
      • Elimu,Afya na Maji
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
      • TAMKO LA VIONGOZI WA UMMA KUHUSU RASILIMALI NA MADENI
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Stoo Ya Picha

MWENYEKITI WA HALMASHAURI SAME APONGEZA USIMAMIZI BOOST

Posted on: September 4th, 2023

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Same Mhe.Yusto Mapande amepongeza usimamizi wa utekelezaji wa Miradi ya Ujenzi wa Madarasa na matundu ya vyoo unaotekelezwa na Mradi wa BOOST katika Wilaya ya Same.

 Mhe. Mapande ametoa pongezi hizo wakati Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango ilipotembelea na kukagua miradi ya BOOST  inayotekelezwa katika shule 10 za Msingi ambayo inagharimu shilingi bil. 1.8.

Mwenyekiti amempongeza  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo  Bi Anastazia Tutuba pamoja na timu yake ya Wataalam kwa usimamizi mzuri wa Miradi hiyo  kwani imejengwa kwa kiwango kinachostahili  na thamani ya fedha imeweza kuonekana" Mmefanya kazi nzuri, kazi inavutia, inafaa kuonyeshwa kwa kila mtu naye atatamani kujifunza kutoka kwenu"amesema Mhe.Mapande.

Mradi wa BOOST katika Halmashauri ya Wilaya ya Same unajenga shule mbili mpya za msingi ambazo ni Kisima na Mgandu pamoja na madarasa thelathini na nne (34) katika shule nane (8) za msingi pamoja na matundu ya vyoo.

Shule nane zilizonufaika na ujenzi wa madarasa ni Mbono na Ndolwa ambazo kila moja imepata madarasa saba,Kwesasu,Turiani na Mpirani kila moja madarasa matano,Kikwete madarasa sita,Dimwi madasrasa matatu na Mbuyuni madarasa mawili.  

Mkurugenzi Mtendaji  wa Halmashauri ya Wilaya ya Same Bi. Anastazia Tutuba ameishukuru Serikali ya Awamu ya sita kwa kuwaletea miradi mbalimbali hususani kwenye sekta ya  Elimu  ambapo imesaidia kupunguza tatizo la upungufu wa madarasa kwa wanafunzi pamoja na kuepusha wanafunzi kutembea umbali mrefu kwenda shuleni.

"Tumepokea fedha nyingi za miradi tunamshukuru sana Mhe. Rais,  Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuwajali wananchi wa Wilaya ya Same” amesema Bi.Tutuba.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo Mwenyekiti wa Kijiji cha Mgandu inapojengwa shule mpya ya Msingi, Bw. Amiri Dongo amemwomba Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Same Bi. Anastazia Tutuba kumsaidia kupata waalimu wenye uweledi wa kufundisha ambao watasaidia shule hiyo kuwa na ufaulu mzuri.

 Pia Diwani wa Kata ya Bendera Mhe. Mhina Mmasa ameishukuru Serikali kwa kuwapatia Mradi wa ujenzi wa shule hiyo mpya kwani itasaidia kupunguza changamoto ya umbali kwa wanafunzi kwenda shuleni kwani walikuwa wanaenda kusoma Kata ya jirani ambapo ni mbali.

"Ujenzi wa shule hii umepunguza changamoto kwa sababu watoto walikuwa wanasoma mbali  ambapo wakati wa mafuriko wanakaa hadi mwezi bila kufika shuleni kwani daraja wanalolitegemea kuvuka hujaa maji” amesema Mhe.Mmasa.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 31, 2021
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI May 06, 2025
  • Siku ya kufanya usafi mwezi Septemba September 08, 2021
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2020 August 21, 2020
  • Tazama Vyote

Habari Za Sasa

  • MRADI WA SWASH ULIVYONUFAISHA WILAYA YA SAME

    April 03, 2025
  • WANANCHI WA MAKEI,SAME WAONDOKANA NA ADHA YA MAJI

    March 23, 2025
  • SAME YATOA ELIMU YA TAHADHARI YA MPOX MASHULENI

    March 18, 2025
  • MAAFISA UTUMISHI SIMAMIENI STAHIKI ZA WATUMISHI-DC SAME

    March 13, 2025
  • Tazama Vyote

Video

KARIBU MWENGE WA UHURU SAME KILIMANJARO 2022
Video Zaidi

Viunganishi Vya Haraka

  • Forms And Templates
  • Galleys
  • News
  • Events
  • Strategic Plan
  • Reports
  • Acts
  • Malalamiko

Viunganishi Vyenye Uhusiano

  • PO-Ralg
  • PO-Psm
  • e-Government Agency
  • Kilimanjaro Region
  • Employment
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Watembeleaji

free HitCounter

Ramani Ya Wilaya

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Same.Haki zote zimehifadhiwa.