• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Same District Council
Same District Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala Za Mikoa na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Same

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idaraya Elimu Sekondari
      • Rasili Mali Watu na Utawala
      • Ardhi Maliasili na Utalii
      • Fedha Na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Kazi na Zimamoto
      • Maji
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi.
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo Cha TEHAMA
      • Kitengo Cha Nyuki
      • Kitengo Cha Uchaguzi
      • Kitengo Cha Manunuzi
      • Kitengo Cha Sheria
    • Kata
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Mipango
      • Elimu,Afya na Maji
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
      • TAMKO LA VIONGOZI WA UMMA KUHUSU RASILIMALI NA MADENI
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Stoo Ya Picha

MKUU WA WILAYA ATOA ANGALIZO MVUA ZA ELNINO

Posted on: October 7th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Same Mheshimiwa Kasilda Mgeni amewataka wananchi wanaoishi maeneo hatarishi ambayo hupata athari za Mafuriko au maporomoko ya miamba (landslides) kuhama maeneo hayo kwa muda ili kupisha mvua za Elnino zinazotarajiwa kunyesha mwezi huu wa Oktoba 2023.

Agizo hilo la Mkuu wa Wilaya linakuja kufuatia taarifa iliyotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kuwa Wilaya ya Same iliyopo Mkoani Kilimanjaro ni Miongoni mwa Wilaya zilizotabiriwa kuwa na mvua kubwa za Elnino kuanzia wiki ya pili ya mwezi Oktoba 2023.

Amesema kutokana na Utabiri huo tayari Wilaya ya Same imeshaunda Kamati za Maafa za Wilaya (Kamati Elekezi na Kamati ya Wataalam) Kamati za Kata na za Vijiji kwaajili ya kujiandaa kwa njia mbalimbali ili kukabiliana na athari zinazoweza kusababishwa na mvua hiyo ambapo kwasasa Kamati hizo zinaendelea kutoa elimu kwa Wananchi katika Maeneo mbalimbali.

Ameyataja maeneo ambayo yamekuwa yakiathiriwa na maporomoko ya miamba (landslides) wakati mvua zinapokuwa nyingi katika Wilaya ya Same ni baadhi ya vijiji katika Kata za Myamba,Msindo,Kirangare,Mpinji,Chome na Vunta.

Maeneo ya tambarare ambayo huwa yanaathiriwa na mvua ni maeneo ya Kata za Same,Njoro,Makanya,Hedaru,Ruvu,Maore na Kihurio ambapo maeneo haya hupokea maji yanayotoka katika maeneo ya milimani na hivyo kusababisha mafuriko.

Mkuu wa Wilaya ameziagiza  Kamati za maafa za Wilaya,Kata na Vijiji kuendelea kutoa elimu na kuwashauri wananchi kuhama kwa muda katika maeneo hatarishi ili kupisha Mvua zilizotabiriwa kunyesha mwezi Oktoba  2023.

Ameitaka hatua nyingine zinazoendelea kuchukuliwa na Wilaya ili kupunguza athari za Mafuriko ni pamoja na kuzibua mitaro na kuchimba njia za dharura za kupitisha maji katika maeneo yote hatarishi ili kuruhusu maji kupita kwa urahisi.

Katika kukabiliana na magonjwa ya mlipuko tayari Wilaya imeshaandaa dawa mbalimbali pamoja na kuainisha hospitali,vituo vya afya na zahanati ambazo zipo katika maeneo yanayoonekana kuwa salama ambazo zitakuwa zinatoa huduma kwa wahanga.

"Nawasihi Wananchi wa Wilaya ya Same kuendelea kufuatilia na kuzingatia taarifa za Mamlaka ya Hali ya hewa Tanzania(TMA) ili kuweza kuchukua hatua kabla madhara hayajatokea

Aidha Wananchi waepuke kukaa chini ya miti, kutembea sehemu hatarishi kama kwenye mikondo ya maji na umeme hasa wakati Mvua ikiwa inanyesha kwani ni hatari kwa maisha yao.

Nitoe angalizo pia kwa wanaotumia vyombo vya Moto waepuke kabisa kupita sehemu ambapo maji ni mengi,waepuke kupita maeneno ambayo maji yamefunika madaraja.

Pia wakati wote wananchi wanapaswa kuwa na akiba ya chakula, fedha, maji, na vifaa vya huduma ya kwanza majumbani mwao kwa kipindi chote cha matarajio ya mvua kwa mujibu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa.

Kila mwananchi ahakikishe anakuwa na namba ya simu kiongozi wake katika eneo analoishi iwe ni wa Kijiji au Kata ili aweze kutoa taarifa kunapokuwa na tatizo.



Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 31, 2021
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI May 06, 2025
  • Siku ya kufanya usafi mwezi Septemba September 08, 2021
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2020 August 21, 2020
  • Tazama Vyote

Habari Za Sasa

  • MRADI WA SWASH ULIVYONUFAISHA WILAYA YA SAME

    April 03, 2025
  • WANANCHI WA MAKEI,SAME WAONDOKANA NA ADHA YA MAJI

    March 23, 2025
  • SAME YATOA ELIMU YA TAHADHARI YA MPOX MASHULENI

    March 18, 2025
  • MAAFISA UTUMISHI SIMAMIENI STAHIKI ZA WATUMISHI-DC SAME

    March 13, 2025
  • Tazama Vyote

Video

KARIBU MWENGE WA UHURU SAME KILIMANJARO 2022
Video Zaidi

Viunganishi Vya Haraka

  • Forms And Templates
  • Galleys
  • News
  • Events
  • Strategic Plan
  • Reports
  • Acts
  • Malalamiko

Viunganishi Vyenye Uhusiano

  • PO-Ralg
  • PO-Psm
  • e-Government Agency
  • Kilimanjaro Region
  • Employment
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Watembeleaji

free HitCounter

Ramani Ya Wilaya

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Same.Haki zote zimehifadhiwa.