• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Same District Council
Same District Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala Za Mikoa na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Same

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idaraya Elimu Sekondari
      • Rasili Mali Watu na Utawala
      • Ardhi Maliasili na Utalii
      • Fedha Na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Kazi na Zimamoto
      • Maji
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi.
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo Cha TEHAMA
      • Kitengo Cha Nyuki
      • Kitengo Cha Uchaguzi
      • Kitengo Cha Manunuzi
      • Kitengo Cha Sheria
    • Kata
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Mipango
      • Elimu,Afya na Maji
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
      • TAMKO LA VIONGOZI WA UMMA KUHUSU RASILIMALI NA MADENI
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Stoo Ya Picha

DCEA YATOA MAFUNZO KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA.

Posted on: May 30th, 2025

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) Kanda ya Kaskazini imeendesha mafunzo maalum kwa Viongozi wa Serikali kuanzia ngazi ya Wilaya hadi Vitongoji, Wilayani  Same, mkoani Kilimanjaro kwa lengo la kudhibiti matumizi ya madawa ya kulevya.

Mafunzo hayo yamefanyika Mei 29, 2025, kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Same, yamelenga kuwawezesha viongozi hao kutambua, kuzuia na kushughulikia changamoto zinazotokana na matumizi na biashara haramu ya dawa za kulevya.

Viongozi hao pia wamehimizwa kuzingatia maadili, uwajibikaji na ushirikiano wa kijamii katika mapambano hayo.

Akifungua mafunzo hayo, Mkuu wa Wilaya ya Same, Mheshimiwa Kasilda Mgeni, alisema kuwa dawa za kulevya si tu kwamba zina madhara ya kiafya kwa binadamu, bali pia zinachangia kudhoofisha uchumi, kuvuruga familia, kuporomosha maadili, kupunguza nguvu kazi ya Taifa na kuongeza matukio ya uhalifu.

“Hili ni janga linalohitaji nguvu ya pamoja kuanzia kwa viongozi, wazazi, walimu na vijana wenyewe ambao ndio waathirika wakuu wa dawa za kulevya.

Hivyo nawahimiza kupitia mafunzo haya mkawe mabalozi na waelimishaji; muhamasishe na msimamie utekelezaji wa mikakati ya kupambana na dawa za kulevya katika maeneo yenu.”

Aidha, aliwataka viongozi wa serikali kuhakikisha kuwa wanakuwa wawajibikaji, waadilifu na kutofumbia macho biashara haramu ya dawa za kulevya katika maeneo yao.

Kwa upande wake, Afisa Elimu kutoka Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Kanda ya Kaskazini Bw. Shaban Miraji, alisema kuwa sababu kuu zinazochangia matumizi ya dawa za kulevya ni pamoja na malezi duni, ukosefu wa elimu sahihi kuhusu madhara ya dawa hizo, pamoja na hali ngumu ya kiuchumi.

Kwa mujibu wa Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ya mwaka 2015, mtu yeyote atakayekutwa akilima bangi au mirungi, kufanya biashara, kusafirisha au kumiliki kiasi cha bangi au mirungi kisichozidi kilo 100, atahukumiwa kifungo kisichopungua miaka 30. Iwapo kiasi hicho kitazidi kilo 100, adhabu ni kifungo cha maisha.@ortamisemi@maelezonews

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 31, 2021
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI May 06, 2025
  • Siku ya kufanya usafi mwezi Septemba September 08, 2021
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2020 August 21, 2020
  • Tazama Vyote

Habari Za Sasa

  • DC KASILDA ATAKA WANANCHU KUTUMIA FURSA ZA KIUCHUMI WAKATI WA ZIARA YA MWENGE WA UHURU

    June 10, 2025
  • WASHIRIKI UMISSETA WATAKIWA KUWAKILISHA VEMA WILAYA YA SAME

    June 09, 2025
  • WASHIRIKI UMISSETA WATAKIWA KUWAKILISHA VEMA WILAYA YA SAME

    June 09, 2025
  • SAME YAENDELEA KUTOA MAFUNZO KUHUSU MATUMIZI YA MFUMO WA NeST

    June 03, 2025
  • Tazama Vyote

Video

KARIBU MWENGE WA UHURU SAME KILIMANJARO 2022
Video Zaidi

Viunganishi Vya Haraka

  • Forms And Templates
  • Galleys
  • News
  • Events
  • Strategic Plan
  • Reports
  • Acts
  • Malalamiko

Viunganishi Vyenye Uhusiano

  • PO-Ralg
  • PO-Psm
  • e-Government Agency
  • Kilimanjaro Region
  • Employment
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Watembeleaji

free HitCounter

Ramani Ya Wilaya

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Same.Haki zote zimehifadhiwa.