• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Same District Council
Same District Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala Za Mikoa na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Same

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idaraya Elimu Sekondari
      • Rasili Mali Watu na Utawala
      • Ardhi Maliasili na Utalii
      • Fedha Na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Kazi na Zimamoto
      • Maji
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi.
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo Cha TEHAMA
      • Kitengo Cha Nyuki
      • Kitengo Cha Uchaguzi
      • Kitengo Cha Manunuzi
      • Kitengo Cha Sheria
    • Kata
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Mipango
      • Elimu,Afya na Maji
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
      • TAMKO LA VIONGOZI WA UMMA KUHUSU RASILIMALI NA MADENI
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Stoo Ya Picha

DC SAME AISHUKURU MTABE GROUP KUFADHILI HUDUMA ZA AFYA

Posted on: December 1st, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Same Mheshimiwa Kasilda Mgeni ameishukuru Kampuni ya Mtabe Group kwa kufadhili huduma ya uchunguzi kwa wananchi wa Kata ya Hedaru Wilayani Same na amewataka wananchi kutumia fursa hiyo vizuri ili waweze kujua hali zao kiafya.

Mheshimiwa Kasilda ametoa pongezi hizo wakati akizindua utoaji wa huduma hizo kwenye kituo cha Afya Hedaru ambapo alisema Kampuni hiyo imefanya jambo kubwa sana la kufadhili huduma hizo kwa wananchi wa Hedaru.

“Niwapongeze sana Mtabe Group kwa kujali afya za watanzania na kuamua kuja kufadhili huduma hii hapa Hedaru ili wananchi waweze kujua hali zao za afya” alisema Mhe.Kasilda

Aliwataka wananchi wa Hedaru kutumia vizuri fursa hiyo kwa kujitokeza na kupata huduma za uchunguzi bure na iwapo watagundulika na tatizo lolote waanze matibabu mapema.

Akizungumza kwenye uzinduzi huo Katibu wa Chama Cha Madaktari Tanzania (MAT) Dkt. Nashivai Kivuyo alisema lengo la huduma hizo ni kusaidia kutambua mapema magonjwa yasiyoambukiza ili wananchi waweze kupata huduma mapema.

Alisema uchunguzi utakaofanyika ni wa magonjwa yasiyoambukiza lakini yamekuwa yakiathiri jamii kubwa ambayo ni  Saratani, Shinikizo la damu na Kisukari .

“Tunatambua kuwa mtu ni afya na bila afya hakuna lolote litakaloweza kuendelea hivyo tumekuja kufanya uchunguzi wa magonjwa hayo kwani yanapogundulika mapema inakuwa ni rahisi kuyadhibiti”alisema Dkt. Kivuyo

Nae Mkurugenzi wa Mtabe Group Tanzania Bw.Gerald Aggrey alisema Kampuni yao imeamua kufadhili huduma ya uchunguzi kwa wananchi wa Hedaru ili waweze kujua hali zao kiafya na pia wapate elimu ya kutunza afya zao dhidi ya magonjwa mbalimbali.

Akitoa taarifa za hali ya magonjwa yasiyoambukiza, Mganga Mkuu wa Wilaya ya Same, Dkt Alex Alexander amesema kwamba kwa mwaka huu 2024 hadi kufikia tarehe 30 Octoba, kati ya Wagonjwa wa Nje (OPD) 200,391 waliohudumiwa katika Vituo mbalimbali vya kutolea huduma za Afya ndani ya Wilaya ya Same, Wateja 10,089 sawa na 5.03% walikuwa na Shinikizo la juu la damu (Hypertension), Wateja 3,885 sawa na 1.9% walikuwa na Ugonjwa wa Kisukari (Diabetes Mellitus) na Wateja 124 sawa na 0.01% walikua na Saratani za aina mbalimbali (Cancer).

Hivyo amewaasa wananchi wote wa Hedaru na Wilaya ya Same kwa ujumla kuzingatia namna bora ya maisha kwani magonjwa mengi yasiyoambukiza yanazuilika kwa kuwa na mtindo bora wa maisha kama kufanya mazoezi, kuzingatia lishe bora na kuepuka msongo wa mawazo.

 

Baada ya zoezi la uzinduzi wa huduma hizo kufanyika wananchi zaidi ya 50 walikuwa wamejiorodhesha kufanyiwa uchunguzi wa  afya zao.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 31, 2021
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI May 06, 2025
  • Siku ya kufanya usafi mwezi Septemba September 08, 2021
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2020 August 21, 2020
  • Tazama Vyote

Habari Za Sasa

  • WACHIMBA MADINI SAME WATAKIWA KUTUNZA MAZINGIRA

    May 19, 2025
  • SAME YAPANIA KUONGEZA UZALISHAJI WA MKONGE

    May 05, 2025
  • SAME YAPANIA KUONGEZA UZALISHAJI WA MKONGE

    May 05, 2025
  • SAME YAOMBA WIZARA YA KILIMO KUIPATAIA MICHE YA PARACHICHI

    May 01, 2025
  • Tazama Vyote

Video

KARIBU MWENGE WA UHURU SAME KILIMANJARO 2022
Video Zaidi

Viunganishi Vya Haraka

  • Forms And Templates
  • Galleys
  • News
  • Events
  • Strategic Plan
  • Reports
  • Acts
  • Malalamiko

Viunganishi Vyenye Uhusiano

  • PO-Ralg
  • PO-Psm
  • e-Government Agency
  • Kilimanjaro Region
  • Employment
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Watembeleaji

free HitCounter

Ramani Ya Wilaya

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Same.Haki zote zimehifadhiwa.