Mkuu wa Wilaya ya Same Mheshimiwa Kasilda Mgeni amewataka wananchi wa Same kujitokeza kwa wingi kuulaki Mwenge wa Uhuru na kujipanga vema ili kuweza kutumia vema fursa za kiuchumi wakati Mwenge wa Uhuru utakapowasili Wilayani Same Juni 30 mwaka huu.
Mkuu wa Wilaya amesema Mwenge wa Uhuru unapofika katika maeneo mbalimbali hapa nchini hufungua fursa za kiuchumi kwa wananchi wa eneo hilo hivyo ni vema wananchi wakatumia fursa hizo kukuza uchumi wao.
Amesema Mwenge wa Uhuru utapokelewa Juni 30 mwaka huu kwenye Kata ya Njoro na utakimbizwa kwenye maeneo mbalimba ambapo utaweka mawe ya msingi,kuzindua miradi na kutembelea miradi mbali mbali ya maendendeleo.
Ukiwa Wilayani Same Mwenge wa Uhuru unatarajia kufikia Miradi ya Maji, Barabara, Afya na Mradi wa Vijana Wajasiriamali ambapo Miradi yote ina thamani ya Shilingi Bilioni 2.2
Mwenge wa Uhuru utakesha kwenye uwanja wa Polisi Kata ya Maore.
Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Same.Haki zote zimehifadhiwa.