• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Same District Council
Same District Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala Za Mikoa na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Same

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idaraya Elimu Sekondari
      • Rasili Mali Watu na Utawala
      • Ardhi Maliasili na Utalii
      • Fedha Na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Kazi na Zimamoto
      • Maji
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi.
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo Cha TEHAMA
      • Kitengo Cha Nyuki
      • Kitengo Cha Uchaguzi
      • Kitengo Cha Manunuzi
      • Kitengo Cha Sheria
    • Kata
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Mipango
      • Elimu,Afya na Maji
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
      • TAMKO LA VIONGOZI WA UMMA KUHUSU RASILIMALI NA MADENI
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Stoo Ya Picha

'TAIFISHENI MIFUGO INAYOKULA MITI INAYOPANDWA'-RC BABU

Posted on: March 19th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Nurdin Babu, amekemea tabia ya baadhi ya wafugaji kulisha mifugo yao  kwenye miti inayopandwa katika maeneo mbalimbali Mkoani humo ambapo ameagiza mamlaka za Serikali kutaifisha mifugo Yote itakayokamatwa ikila miti iliyooteshwa.

Mhe. Babu ametoa onyo hilo Machi 19, 2024 Wilayani Same, Mkoa wa Kilimanjaro wakati akifungua warsha kuhusu masuala ya uhifadhi wa rasilimali za misitu ikiwa ni sehemu ya matukio kuelekea kwenye maadhimisho ya Siku ya Misitu Duniani na Siku ya Upandaji Miti Kitaifa inayofanyika Machi 21 wilayani Same, Kilimanjaro.

"Sisi tunaotesha miti lakini wenzetu.wanakuja kulisha mifugo,naagiza Wilaya zote za mkoa wa Kilimanjaro kutaifisha mifugo yote itakayokutwa inakula miti iliyooteshwa"aliagiza Mhe.Babu

Amesema misitu imekuwa na manufaa mengi na kuwa fursa zake zimekuwa zikiongezeka ikiwamo teknolojia ya hewa ukaa na kuwa wananchi wakizitambua fursa hizo watahamasika katika utunzaji wa misitu kwa ajili ya fursa za kiuchumi.

“Misitu inachangia asilimia 3 ya pato la Taifa, inatupatia vifaa vya ujenzi,inasaidia upatikanaji wa mvua,miti inazuia mmomoyoko wa udongo na pia Misitu ni makazi ya wanyama hivyo hatuna budi ya kuhakikisha misitu inahifadhiwa.”alisema

Mkuu wa Mkoa alishauri Elimu kuhusu muhimu wa Misitu itolewe kwa wadau mara kwa mara  ili kuwezesha utunzaji wa misitu na upandaji Wa miti Kwa wingi.

Babu amesema Wilaya ya Same ni miongoni mwa wilaya zilizoathirika na ukataji holela wa miti na kilimo kisichofuata taratibu ya mazingira.

Katika kuirejesha Wilaya ya Same na Mkoa wa Kilimanjaro kwa ujumla kuwa ya kijani, Mhe. Babu alimuagiza Katibu Tawala Mkoa huo kusimamia kwa ukaribu kampeni za upandaji miti ili ipandwe ya kutosha.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Kasilda Mgeni alisema Wilaya ya Same imekuwa ikimuunga mkono Rais Mheshimiwa Rais Dkt. Samia kwa kuhakikisha wanahifadhi mazingira kwa kupanda miti ili kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

"Wilaya yetu imezindua kampeni ya upandaji miti ili kuifanya Same ya Kijani na tayari tumepanda miti kandokando ya barabara kuanzia mwanzo hadi mwisho wa wilaya na mpaka sasa zaidi ya miti laki tano imeshapandwa"alisema Mkuu wa Wilaya.

Akizungumza katika hafla hiyo, Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Ufugaji Nyuki, Bw. Daniel Pancras amesema Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii inajukumu kubwa la kuhamasisha upandaji miti pamoja na kuelimisha juu ya upandaji miti ili watanzania wajue namna bora ya kupanda na kutunza miti

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 31, 2021
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI May 06, 2025
  • Siku ya kufanya usafi mwezi Septemba September 08, 2021
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2020 August 21, 2020
  • Tazama Vyote

Habari Za Sasa

  • WANANCHI WAONYWA KUTOJIUNGANISHIA MAJI KWA NJIA ZISIZO RASMI

    June 18, 2025
  • WANANCHI WAONYWA KUTOJIUNGANISHIA MAJI KWA NJIA ZISIZO RASMI

    June 18, 2025
  • DC KASILDA ATAKA WANANCHU KUTUMIA FURSA ZA KIUCHUMI WAKATI WA ZIARA YA MWENGE WA UHURU

    June 10, 2025
  • WASHIRIKI UMISSETA WATAKIWA KUWAKILISHA VEMA WILAYA YA SAME

    June 09, 2025
  • Tazama Vyote

Video

KARIBU MWENGE WA UHURU SAME KILIMANJARO 2022
Video Zaidi

Viunganishi Vya Haraka

  • Forms And Templates
  • Galleys
  • News
  • Events
  • Strategic Plan
  • Reports
  • Acts
  • Malalamiko

Viunganishi Vyenye Uhusiano

  • PO-Ralg
  • PO-Psm
  • e-Government Agency
  • Kilimanjaro Region
  • Employment
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Watembeleaji

free HitCounter

Ramani Ya Wilaya

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Same.Haki zote zimehifadhiwa.