• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Same District Council
Same District Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala Za Mikoa na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Same

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idaraya Elimu Sekondari
      • Rasili Mali Watu na Utawala
      • Ardhi Maliasili na Utalii
      • Fedha Na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Kazi na Zimamoto
      • Maji
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi.
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo Cha TEHAMA
      • Kitengo Cha Nyuki
      • Kitengo Cha Uchaguzi
      • Kitengo Cha Manunuzi
      • Kitengo Cha Sheria
    • Kata
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Mipango
      • Elimu,Afya na Maji
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
      • TAMKO LA VIONGOZI WA UMMA KUHUSU RASILIMALI NA MADENI
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Stoo Ya Picha

MKUU WA WILAYA ATAKA MADARASA KUKAMILIKA KWA WAKATI

Posted on: October 26th, 2022

Mkuu wa Wilaya ya Same Mhe: Edward Mpogolo amewaagiza mafundi Ujenzi walioshinda zabuni ya ujenzi wa Madarasa kwaajili ya kidato cha kwanza 2023 kuhakikisha kuwa wanakamilisha kazi hiyo kwa muda waliopewa.

Mkuu wa Wilaya alitoa gizo hilo wakati alipoitisha kikao na Wadau wote wa usimamizi wa Ujenzi huo kwa lengo la kuwapa maelekezo muhimu ili kuhakikisha kuwa madarasa hayo yanakamilika kwa wakati.

Kikao hicho kilihudhuriwa na Waheshimiwa Madiwani, wakuu wa Idara na Vitengo,Watendaji Kata,Maafisa Elimu Kata,Wakuu wa shule na Mafundi walioshinda zabuni hizo za ujenzi.

Mkuu huyo alisema Wilaya ya Same imepokea kiasi cha shilingi milioni 640 kwaajili ya ujenzi wa madarasa 32 kwaajili ya kupokea kidato cha kwanza mwaka 2023 hivyo kila mmoja anapaswa kusimama vema kwenye nafasi yake  ili kufikia malengo,

“Lengo letu ni kuhakikisha kuwa haya madarasa yanakamilika mapema Mwezi Desemba,2022 ili Januari yaweze kupokea wanafunzi,kwahiyo niwasihi mafundi wafanye kila linalowezekana wakabidhi madarasa kwa wakati na fundi anayeona hataweza ajiondoe mapema” alisema Mhe:Mpogolo.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Same Mhe:Yusto Mapande amewataka waheshimiwa Madiwani kuhakikisha kuwa wanahamasisha mchango wa nguvu za wananchi katika kusawazisha maeneo ya ujenzi kwani maeneo mengi yana miinuko.

Mhe: Mapande amewataka Wakuu wa shule kusimamia vema ujenzi huo ili ikifika mwezi Januari wanafunzi wote watakaochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza waingie shule.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Same,Anastazia Tutuba ameahidi kufanya ufuatiliaji wa karibu katika kuhakikisha kuwa madarasa yote yanakamilika kwa wakati uliopangwa.

“Fedha hizi zimegawanywa kwa shule 17 ambazo ndizo zilizokuwa na uhitaji wa madarasa na yatakapokamilika yatatosheleza wanafunzi wanaotarajia kuanza kidato cha kwanza”alisema Tutuba.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 31, 2021
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI May 06, 2025
  • Siku ya kufanya usafi mwezi Septemba September 08, 2021
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2020 August 21, 2020
  • Tazama Vyote

Habari Za Sasa

  • MRADI WA SWASH ULIVYONUFAISHA WILAYA YA SAME

    April 03, 2025
  • WANANCHI WA MAKEI,SAME WAONDOKANA NA ADHA YA MAJI

    March 23, 2025
  • SAME YATOA ELIMU YA TAHADHARI YA MPOX MASHULENI

    March 18, 2025
  • MAAFISA UTUMISHI SIMAMIENI STAHIKI ZA WATUMISHI-DC SAME

    March 13, 2025
  • Tazama Vyote

Video

KARIBU MWENGE WA UHURU SAME KILIMANJARO 2022
Video Zaidi

Viunganishi Vya Haraka

  • Forms And Templates
  • Galleys
  • News
  • Events
  • Strategic Plan
  • Reports
  • Acts
  • Malalamiko

Viunganishi Vyenye Uhusiano

  • PO-Ralg
  • PO-Psm
  • e-Government Agency
  • Kilimanjaro Region
  • Employment
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Watembeleaji

free HitCounter

Ramani Ya Wilaya

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Same.Haki zote zimehifadhiwa.