• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Same District Council
Same District Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala Za Mikoa na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Same

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idaraya Elimu Sekondari
      • Rasili Mali Watu na Utawala
      • Ardhi Maliasili na Utalii
      • Fedha Na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Kazi na Zimamoto
      • Maji
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi.
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo Cha TEHAMA
      • Kitengo Cha Nyuki
      • Kitengo Cha Uchaguzi
      • Kitengo Cha Manunuzi
      • Kitengo Cha Sheria
    • Kata
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Mipango
      • Elimu,Afya na Maji
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
      • TAMKO LA VIONGOZI WA UMMA KUHUSU RASILIMALI NA MADENI
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Stoo Ya Picha

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE 2024 ATAKA MRADI WA SMK KUKAMILISHWA JUNI MWAKA HUU

Posted on: April 8th, 2024


Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ndg.Godfrey Mnzava ameagiza Wizara ya Maji kuhakikisha kuwa Mradi mkubwa wa Maji wa wa Same-Mwanga-Korogwe (SMK) unakamilika ifikapo mwezi Juni 2024 kama alivyoagiza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Philip Mpango.

Kiongozi huyo alitoa agizo kufuatia maombi ya Mbunge wa Same Magharibi Mhe.David Mathayo ambaye aliwakilisha changamoto ya upatikanaji wa Maji ya uhakika kwa wakazi wa Same.

"Tunashukuru tangu alipofika Makamu wa Rais Mhe.Philip Mpango tumechimbiwa visima kadhaa ambavyo vimesaidia kwa kiasi kupunguza changamoto ya Maji,lakini bado tunahitaji Maji ya kutosha"alisema Dkt Mathayo.

Kufuatia maombi hayo Kiongozi wa Mbio za Mwenge 2024 Ndg Mnzava aliagiza Mradi mkubwa wa Maji wa SMK kukamilika mwezi Juni 2024 kama alivyoagiza Makamu wa Rais Mhe.Philip Mpango.

Mwenge wa Uhuru umewasili Wilayani Same April 8 na umeweka jiwe la Msingi kwenye Mradi wa Ujenzi wa Barabara Km 1.4 za kiwango cha lami nyepesi ambayo imegharimu shilingi milioni 980.9.

Mwenge wa Uhuru umetembelea Kituo cha watoto wenye mahitaji maalum cha Mother Kevina kilichopo Kata ya Kisima ambacho kinalea watoto 44 wakiwemo watoto wadogo wa Shule za Msingi, Sekondari na wa vyuo.

Kwenye Kituo cha Mother Kevina Kiongozi wa Mwenge wa Uhuru Ndg.Mnzava amekabidhi hundi ya shilingi milioni tatu fedha zilizotokana na michango ya Mwenge kwaajili ya kuwezesha ununuzi wa viti mwendo viwili.

Mwenge wa Uhuru umetembelea pia Kikundi cha Wajasiriamali cha Wandeme ambacho kinajishughulisha na kutengeneza samani za majumbani na za Ofisini.

Kikundi hicho kina mtaji wa milioni 10 na kilipatiwa mkopo wa milioni mbili kutoka mapato ya ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Same.

Akizungumza katika ziara hiyo Mkuu wa Wilaya ya Same Mheshimiwa Kasilda Mgeni ameitaja Miradi mingine itakayofikiwa na Mwenge wa Uhuru 2024 kuwa ni Mradi wa Kitalu cha Miti Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) ambao umegharimu Shilingi milioni 79.

Mwenge wa Uhuru 2024 umezindua pia Klabu ya Wapinga Rushwa Shule ya Sekondari Makanya.

Ukiwa Wilayani Same Mwenge wa Uhuru umezindua Mradi wa Maji wa Kijomu- Mabilioni ambao umegharimu shilingi milioni  447.7

Mradi wa Maji Kijomu-Mabilioni umesaidia kuondoa Kero ya upatikanaji Maji kwa zaidi ya wananchi 2,000 

Mwenge wa Uhuru utazindua jengo la mama na Mtoto kwenye Kituo cha Afya Hedaru,jengo ambalo Ujenzi wake umegharimu shilingi milioni 528 ambapo milioni 8 kati ya fedha hizo zinatokana na nguvu za wananchi.

Katika Wilaya ya Same Mwenge wa Uhuru umefikia Miradi nane yenye thamani ya Tsh.Bil.3.6

Baada ya kukamilisha ziara yake Wilayani Same,Mwenge wa Uhuru utakabidhiwa Mkoani Tanga April 9 katika eneo la Mazinde.

Kaulimbiu ya Mwenge wa Uhuru 2024 "Tunza Mazingira na Shiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa Ujenzi wa Taifa Endelevu"




Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 31, 2021
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI May 06, 2025
  • Siku ya kufanya usafi mwezi Septemba September 08, 2021
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2020 August 21, 2020
  • Tazama Vyote

Habari Za Sasa

  • WANANCHI WAONYWA KUTOJIUNGANISHIA MAJI KWA NJIA ZISIZO RASMI

    June 18, 2025
  • WANANCHI WAONYWA KUTOJIUNGANISHIA MAJI KWA NJIA ZISIZO RASMI

    June 18, 2025
  • DC KASILDA ATAKA WANANCHU KUTUMIA FURSA ZA KIUCHUMI WAKATI WA ZIARA YA MWENGE WA UHURU

    June 10, 2025
  • WASHIRIKI UMISSETA WATAKIWA KUWAKILISHA VEMA WILAYA YA SAME

    June 09, 2025
  • Tazama Vyote

Video

KARIBU MWENGE WA UHURU SAME KILIMANJARO 2022
Video Zaidi

Viunganishi Vya Haraka

  • Forms And Templates
  • Galleys
  • News
  • Events
  • Strategic Plan
  • Reports
  • Acts
  • Malalamiko

Viunganishi Vyenye Uhusiano

  • PO-Ralg
  • PO-Psm
  • e-Government Agency
  • Kilimanjaro Region
  • Employment
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Watembeleaji

free HitCounter

Ramani Ya Wilaya

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Same.Haki zote zimehifadhiwa.