• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Same District Council
Same District Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala Za Mikoa na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Same

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idaraya Elimu Sekondari
      • Rasili Mali Watu na Utawala
      • Ardhi Maliasili na Utalii
      • Fedha Na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Kazi na Zimamoto
      • Maji
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi.
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo Cha TEHAMA
      • Kitengo Cha Nyuki
      • Kitengo Cha Uchaguzi
      • Kitengo Cha Manunuzi
      • Kitengo Cha Sheria
    • Kata
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Mipango
      • Elimu,Afya na Maji
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
      • TAMKO LA VIONGOZI WA UMMA KUHUSU RASILIMALI NA MADENI
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Stoo Ya Picha

'HAKIKISHENI MITI YOTE INAYOOTESHWA INAKUWA'-DC KASILDA

Posted on: November 20th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Same Mheshimiwa Kasilda Mgeni  amezitaka taasisi mbalimbali za serikali na zisizo za serikali kuhakikisha kwamba miti yote inayooteshwa kipindi hiki cha mvua inastawi.

Ameyasema hayo wakati akizindua zoezi la upandaji miti kwenye Wilaya ya Same kwa msimu wa 2023/24 ambapo alisema ni vema miti yote inayooteshwa ikasimamiwa vema iweze kuota na kukua.

“Tunaotesha miti mingi sana kila mwaka lakini tujiulize katika miti tunayootesha ni mingapi inayostawi na kukua vizuri,katika eneo hili tunapaswa kuwa makini” alisema Mheshimiwa Kasilda

Mkuu huyo wa Wilaya alisema mabadiliko ya tabia nchi yanayosababishwa na uharibifu wa mazingira ni makubwa mno kutokana na kuongezeka kwa shughuli za kibinadamu ambazo zinasababisha mitiu mingi kukatwa hivyo hatuna budi kukabiliana na hili kwa kuotesha miti kwa wingi na kuhakikisha miti hiyo inakua.

Akizungumza katika uzinduzi huo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Same Bi.Anastazia Tutuba alisema kwa upande wa taasisi za Serikali miti yote inayooteshwa inasimamiwa vema ambapo Zaidi ya asilimia 95 ya miti inayooteshwa hukua vema.

“Kila mwaka tunalengo la kuotesha miti mil.1.5 ambapo miti hugawanywa kwenye taasisi za serikali,taasisi binafsi na kwa mtu mmojammoja kwaajili ya kuotesha na imeshaanza kuleta tija” alisema Bi.Anastazia.

Alisema katika maeneo ya shule zote za  Msingi na Sekondari zikiwemo za Serikali na binafsi zimezungukwa na miti mingi na bado wanaendelea kupewa miti ili waweze kuotesha.

Katika Uzinduzi huo jumla ya miti 1,000 ilioteshwa katika eneo linalozunguka Hospitali mpya ya Wilaya ya Same ambapo miti mingine 99,000 iligawanywa kwaajili ya kuoteshwa kwenye taasisi nyingine za serikali.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Utalii ya Tanzania Footmark Safaris ambao ndio waliofadhili miti hiyo Bi.Rehema Mghamba alisema wamekuwa wakishirikiana na Serikali kuotesha miti ili kuendeleza vivutio vya utalii.

“Sisi tunafanya biashara ya Utalii na unapozungumzia utalii kwa kiasi kikubwa tunamaanisha uwepo wa wanyama na viumbe hai vingine, sasa ili hivi vyote viwepo ni lazima tuendelee kuotesha miti tena kwa wingi”alisema Bi.Rehema.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 31, 2021
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI May 06, 2025
  • Siku ya kufanya usafi mwezi Septemba September 08, 2021
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2020 August 21, 2020
  • Tazama Vyote

Habari Za Sasa

  • WANANCHI WAONYWA KUTOJIUNGANISHIA MAJI KWA NJIA ZISIZO RASMI

    June 18, 2025
  • WANANCHI WAONYWA KUTOJIUNGANISHIA MAJI KWA NJIA ZISIZO RASMI

    June 18, 2025
  • DC KASILDA ATAKA WANANCHU KUTUMIA FURSA ZA KIUCHUMI WAKATI WA ZIARA YA MWENGE WA UHURU

    June 10, 2025
  • WASHIRIKI UMISSETA WATAKIWA KUWAKILISHA VEMA WILAYA YA SAME

    June 09, 2025
  • Tazama Vyote

Video

KARIBU MWENGE WA UHURU SAME KILIMANJARO 2022
Video Zaidi

Viunganishi Vya Haraka

  • Forms And Templates
  • Galleys
  • News
  • Events
  • Strategic Plan
  • Reports
  • Acts
  • Malalamiko

Viunganishi Vyenye Uhusiano

  • PO-Ralg
  • PO-Psm
  • e-Government Agency
  • Kilimanjaro Region
  • Employment
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Watembeleaji

free HitCounter

Ramani Ya Wilaya

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Hakimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Same.Haki zote zimehifadhiwa.